"Ujenzi wa choo nao hadi umsubiri Rais"; Kauli hii ya Mh. Magufuli imenitafakarisha sana

ALWATAN KIZIGO

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
539
642
Jana siku ya Tarehe 5/5/2018 wakati Mh. Rais Magufuli akiendela na Ziara yake Mkoani Morogoro alisimamishwa na wananchi katika Kijiji cha Mang'ula, na hapo ndipo akajitokeza kijana mdogo wa kidato cha kwanza aitwaye Mlindoka Msangi akaelezea changamoto ya vyoo inayoikabili shule yao ya Mang'ula Secondary.

Mh. Rais akatoa Shillingi million 3 na kukamkabidhi kijana huyo azipeleke shuleni chini ya ulinzi wa Polisi. Pamoja na kutatua changamoto hiyo lakini bado Mh Rais alijiuliza maswali mengi sana na ndio maana hata alipokua anahutubia katika uzinduzi wa Daraja la Magufuli ilimbidi aelezee tukio hilo na akasisitiza kwa kusema kwamba "hivi hata ujenzi wa vyoo nao mpaka umsubiri Rais"

Hii ni kauli nzito sana yenye ujumbe mzito kwa wasaidizi wake Serikalini kwa maana ya wakuu wa Mikoa ,wakuu wa Wilaya , Wakurugenzi na wasaidizi wake kwenye Chama kuanzia Wenyeviti wa Mikoa na Wilaya na Kamati za Siasa za Mikoa na Wilaya.

Kiukweli kuna baadhi ya kero ndogondogo ambazo hazihitaji kiasi kikubwa cha pesa ili kuziondoa bali zinahitaji utashi na uwajibikaji tu, lakini zimeendelea kuwa changamoto sugu kwa wananchi.

Sasa hapo ndipo unajiuliza maswali iwapo baadhi ya wasaidizi wa Rais katika ngazi tajwa hapo juu wanatimiza majukumu yao kisawa sawa? Ujenzi wa kitu kama choo haukupaswa kusubri ziara ya Mh.Rais ili kumalizwa ni aibu.

Tatizo hili linasababishwa na baadhi ya wasaidizi Mikoani na Wilayani kutofanya ziara za mara kwa mara ili kubaini kero mbalimbali na kuzitafutia namna ya kuzimaliza badala yake wanapendelea kukaa maofisini kupuliziwa na ubaridi wa viyoyozi.

Rais hawezi kufika katika kila Kata au kijiji Tanzania nzima na ndio maana akawateua wasaidizi wake ili wakamsaidie kuwahudumia wananchi huko kwenye ngazi za chini.

Sasa inapofikia mahali wananchi wanaendelea kusumbuliwa na vikero vidogovidogo ambavyo vinaweza kumalizwa na ngazi ya Mkoa au Wilaya basi tunapata jibu kuwa kuna baadhi ya watumishi hawamtendei haki Rais aliyewateua.

Rais anahangaika huku na kule kuinyoosha nchi anasema kila siku kwamba watumishi aliowateua waache uvivu na uzembe lakini bado baadhi yao maskini ya MUNGU bado wamelala usingizi wa pono.

Mathalani kuna baadhi ya Wilaya utakuta wananchi wamejitolea kwa nguvu zao kujenga kituo cha afya mpaka ngazi ya rinta na nguvu zimewaishia hivyo basi wanapoenda kuomba msaada wa umaliziaji katika Halmshauri unakuta wanapigwa danadana.Hii inasikitisha sana.

Pia kwa wanasiasa hususani Wabunge nao wana fedha za maendeleo ya Jimbo. Fedha hizi wanapewa na Serikali ili kusaidia kusukuma maendeleo katika majimbo yao.

Lakini kwa bahati mbaya sio wabunge wote wanaofanya hivyo na ndio maana hadi leo ukitembelea majimboni utakutana na kero ndogo ndogo ambazo kama kungekuwa na Sera ya uwazi ya matumizi ya fedha za maendeleo ya jimbo basi kero hizo zingeweza kutatuliwa maramoja.

Rais ana majukumu mengi wasaidizi wake Serikalini ifike mahali wamuonee huruma jinsi alivyojitoa ili kusukuma gurudumu la maendeleo ya watu wake, "li nchi hili ni likubwa" tukisema kila kitu tumuachie Rais tutakua tunamuonea kiukweli ,ni vyema wakaendana na kasi yake kwa kuwajibika kwa nguvu na kuwa wabunifu katika maeneo yao.

Muda wa kuwa na watumishi mangimeza umeshaisha huu ni wakati wa kuchapa kazi. Haingii akilini Serikali inampa mtu gari , inamlipa mshahara na stahiki zake nyingine lakini bado mtu huyo anakua mzito katika kutimiza majukumu yake.

Na viongozi wa chama nao kupitia Kamati za siasa wamsaidie Mwenyekiti wetu katika kuisimamia Serikali kwenye ngazi husika hususani katika kuziwasilisha kero za kipaumbele Serikalini ili zipatiwe ufumbuzi wa haraka.

Uzembe wa namna hiyo ndio unaochangia kupunguza kura za CCM katika uchaguzi hivyo watu wa namna hiyo inabidi wabadilike, ili CCM iendelee kupeta kwa sababu mwisho wa siku wananchi wanakiadhibu chama na sio wao na katika hili sidhani kama Mwenyekiti atakua radhi kuona chama chake kinaadhibiwa kutokana na uzembe na uvivu wa baadhi ya wasaidizi nafikiri ataanza kuwaadhibu wao kwanza kabla chama hakijaadhibiwa.

Wao ndio wanaokaa na wananchi na ni wao ambao wanazijua kero mbalimbali za wananchi hivyo kwa kutumia mamlaka waliyonayo ya Kuisimamia Serikali wanaweza kusaidia katika kutatua changamoto hizo haswa ikizingatiwa kwamba CCM sasa hivi inashika hatamu katika kuisimamia Serikali.

Wasalaam,
Augustino Chiwinga.
0659438889.
 
m n mpinzan kwa asil
lakin bro hapa umeeleza ukwel huwa cwaelew kabisa
mf ishu ya madarasa mashulen utakuta wazaz wapo tayar kufyatua tofali za ujenz wa madarasa lakn hawana pesa ya kujenga wakienda kuomba wanazungushwaaaaa
wakat hela yenyewe n million 2 au 3 tu
 
Hilo tukio mimi naliona ni sawa! Si tumeaminishwa kua wananchi huwa wanazuia msafara wa rais na kueleza changamoto zao? Mbona ya yule mama aliotolewa kizazi haikuonwa ni mbaya? Mwacheni aone shule zake zilivyo na matatizo hata kama ni madogo ndio hayo hayo yanayoshusha elimu!
 
m n mpinzan kwa asil
lakin bro hapa umeeleza ukwel huwa cwaelew kabisa
mf ishu ya madarasa mashulen utakuta wazaz wapo tayar kufyatua tofali za ujenz wa madarasa lakn hawana pesa ya kujenga wakienda kuomba wanazungushwaaaaa
wakat hela yenyewe n million 2 au 3 tu
Unataka Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wawe wanachukua za mifukoni mwao sivyo?
 
Labda tatizo ni fedha....

Na itabidi rais akafanye uzinduzi yeye mwenyewe siku ujenzi ukikamilika.

Mtazamo wangu, unapokuwa na bosi ambaye kila kitu anataka mkono wake uwepo, na kila kikifanyika bila yeye kuweka mkono wake anakosoa, analalamika ubora wa kilichofanyika, kuna muda watendaji wanaona ni bora tu wasubiri bosi mwenyewe aamue.
 
Ningekuwa magufuri ningekuja kutoa tamko hili

"nasema hivi wakurugenzi, wakuu wa wilaya afisa tawala mkoa, na mafisa elimu, waratibu elimu kata na wakuu wa shule naomba mnisike nasema tena naomba mnisikie, sitaki kusikia eti shule haina vyoo vya wanafunzi nawapa mienzi minne kuanzia leo hii baada ya hapo wazazi na wanafunzi naomba mje mniambie shule gani haina vyoo nimemaliza"

Nakwambia mh akisema hivyo mwezi mmoja tu inchi nzima shule zitakuwa na vyoo

Nasema hivi kwa sababu watendaji wengi waserikali ubunifu zero wanataka amri tu hata kwa vitu ambavyo vipo ndani ya uwezo wao, wakipewa amri wapo radhi watoto wao walale njaa ili watimize hiyo amri kulinda vyeo vyao ila kufanya hiyo kazi kwa utashi bila amri hawawezi.
 
Jana siku ya Tarehe 5/5/2018 wakati Mh.Rais Magufuli akiendela na Ziara yake Mkoani Morogoro alisimamishwa na wananchi katika Kijiji cha Mang'ula, na hapo ndipo akajitokeza kijana mdogo wa kidato cha kwanza aitwaye Mlindoka Msangi akaelezea changamoto ya vyoo inayoikabili shule yao ya Mang'ula Secondary.

Mh.Rais akatoa Shillingi million 3 na kukamkabidhi kijana huyo azipeleke shuleni chini ya ulinzi wa Polisi.
Pamoja na kutatua changamoto hiyo lakini bado Mh Rais alijiuliza maswali mengi sana na ndio maana hata alipokua anahutubia katika uzinduzi wa Daraja la Magufuli ilimbidi aelezee tukio hilo na akasisitiza kwa kusema kwamba "hivi hata ujenzi wa vyoo nao mpaka umsubiri Rais"

Hii ni kauli nzito sana yenye ujumbe mzito kwa wasaidizi wake Serikalini kwa maana ya wakuu wa Mikoa ,wakuu wa Wilaya , Wakurugenzi na wasaidizi wake kwenye Chama kuanzia Wenyeviti wa Mikoa na Wilaya na Kamati za Siasa za Mikoa na Wilaya.

Kiukweli kuna baadhi ya kero ndogondogo ambazo hazihitaji kiasi kikubwa cha pesa ili kuziondoa bali zinahitaji utashi na uwajibikaji tu, lakini zimeendelea kuwa changamoto sugu kwa wananchi.
Sasa hapo ndipo unajiuliza maswali iwapo baadhi ya wasaidizi wa Rais katika ngazi tajwa hapo juu wanatimiza majukumu yao kisawa sawa?
Ujenzi wa kitu kama choo haukupaswa kusubri ziara ya Mh.Rais ili kumalizwa ni aibu.

Tatizo hili linasababishwa na baadhi ya wasaidizi Mikoani na Wilayani kutofanya ziara za mara kwa mara ili kubaini kero mbalimbali na kuzitafutia namna ya kuzimaliza badala yake wanapendelea kukaa maofisini kupuliziwa na ubaridi wa viyoyozi.
Rais hawezi kufika katika kila Kata au kijiji Tanzania nzima na ndio maana akawateua wasaidizi wake ili wakamsaidie kuwahudumia wananchi huko kwenye ngazi za chini.
Sasa inapofikia mahali wananchi wanaendelea kusumbuliwa na vikero vidogovidogo ambavyo vinaweza kumalizwa na ngazi ya Mkoa au Wilaya basi tunapata jibu kuwa kuna baadhi ya watumishi hawamtendei haki Rais aliyewateua.
Rais anahangaika huku na kule kuinyoosha nchi anasema kila siku kwamba watumishi aliowateua waache uvivu na uzembe lakini bado baadhi yao maskini ya MUNGU bado wamelala usingizi wa pono.

Mathalani kuna baadhi ya Wilaya utakuta wananchi wamejitolea kwa nguvu zao kujenga kituo cha afya mpaka ngazi ya rinta na nguvu zimewaishia hivyo basi wanapoenda kuomba msaada wa umaliziaji katika Halmshauri unakuta wanapigwa danadana.Hii inasikitisha sana.

Pia kwa wanasiasa hususani Wabunge nao wana fedha za maendeleo ya Jimbo .Fedha hizi wanapewa na Serikali ili kusaidia kusukuma maendeleo katika majimbo yao.
Lakini kwa bahati mbaya sio wabunge wote wanaofanya hivyo na ndio maana hadi leo ukitembelea majimboni utakutana na kero ndogo ndogo ambazo kama kungekuwa na Sera ya uwazi ya matumizi ya fedha za maendeleo ya jimbo basi kero hizo zingeweza kutatuliwa maramoja.

Rais ana majukumu mengi wasaidizi wake Serikalini ifike mahali wamuonee huruma jinsi alivyojitoa ili kusukuma gurudumu la maendeleo ya watu wake, "li nchi hili ni likubwa" tukisema kila kitu tumuachie Rais tutakua tunamuonea kiukweli ,ni vyema wakaendana na kasi yake kwa kuwajibika kwa nguvu na kuwa wabunifu katika maeneo yao.

Muda wa kuwa na watumishi mangimeza umeshaisha huu ni wakati wa kuchapa kazi.
Haingii akilini Serikali inampa mtu gari , inamlipa mshahara na stahiki zake nyingine lakini bado mtu huyo anakua mzito katika kutimiza majukumu yake.

Na viongozi wa chama nao kupitia Kamati za siasa wamsaidie Mwenyekiti wetu katika kuisimamia Serikali kwenye ngazi husika hususani katika kuziwasilisha kero za kipaumbele Serikalini ili zipatiwe ufumbuzi wa haraka.
Uzembe wa namna hiyo ndio unaochangia kupunguza kura za CCM katika uchaguzi hivyo watu wa namna hiyo inabidi wabadilike, ili CCM iendelee kupeta kwa sababu mwisho wa siku wananchi wanakiadhibu chama na sio wao na katika hili sidhani kama Mwenyekiti atakua radhi kuona chama chake kinaadhibiwa kutokana na uzembe na uvivu wa baadhi ya wasaidizi nafikiri ataanza kuwaadhibu wao kwanza kabla chama hakijaadhibiwa.

Wao ndio wanaokaa na wananchi na ni wao ambao wanazijua kero mbalimbali za wananchi hivyo kwa kutumia mamlaka waliyonayo ya Kuisimamia Serikali wanaweza kusaidia katika kutatua changamoto hizo haswa ikizingatiwa kwamba CCM sasa hivi inashika hatamu katika kuisimamia Serikali.

Wasalaam,
Augustino Chiwinga.
0659438889.
Fedha za mfuko wa jimbo zinajenta ukuta wa private school na hiyo ndio mpenyo mpya wa kukwepa Kukaguliwa matumizi Na Kamati za Kata na Wilaya.
[HASHTAG]#Watuwabayaa[/HASHTAG]!
 
Pesa ya serikali ina utaratibu wake. Watumishi wa umma hawawezi kujiingiza kwenye matatizo kwa kubadilisha matumizi ya pesa za serikali.

Anyway, Rais kutoa million 3 siyo suruhisho la tatizo .... inabidi ashughulikie tatizo lenyewe. Kama hakuna pesa ambazo ziko allocated kwa ajili ya ujenzi wa vyoo mnategemea Wakurungezi wazitoe wapi!? Tatizo la vyoo linazikabili huenda zaidi ya 80 % ya shule zote nchini. Vyoo vyingi ni vya mashimo halafu haviko kwenye standard ya kuridhisha. may be fortunately, hakuna ajali zimetokea za watoto kutumbukia kwenye matundu ya vyoo.

Rais kama atakuwa anasikiliza kero na kutoa maburungutu papo kwa pao kuna siku ataingizwa mjini. I hope hayo maburungutu ni sehemu ya mshahara wake!!
 
nahisi mawaziri, ma RC, ma DC wake wanakula 'shushi' sana kwani kazi zao anafanya yeye. Raisi angejenga mfumo ili kila mwenye dhamana atimize wajibu wake. Tofauti na hapo hatufiki popote.
 
Fedha za mfuko wa jimbo zinajenta ukuta wa private school na hiyo ndio mpenyo mpya wa kukwepa Kukaguliwa matumizi Na Kamati za Kata na Wilaya.
[HASHTAG]#Watuwabayaa[/HASHTAG]!
unawajua signatories wa pesa ya mfuko wa jimbo?
 
Yajayo yanafurahisha,

Yeye Rais mwenyewe hajui majukumu yake hata yeye anachokifanya sio sahihi ni kama snema. Wakati ana baraza la mawaziri,wakuu wa mikoa,wilaya,wakurugenzi wote wako chini yake.

Hata ukikaa ikulu unaweza kujua shida zote zilizopo Tz. Nafikiri ameshindwa kuwatumia vizuri hao niliowataja sasa anafanya show.sifa aonekane ni mtetezi wa wanyonge.
 
Sasa hapo ndipo unajiuliza maswali iwapo baadhi ya wasaidizi wa Rais katika ngazi tajwa hapo juu wanatimiza majukumu yao kisawa sawa? Ujenzi wa kitu kama choo haukupaswa kusubri ziara ya Mh.Rais ili kumalizwa ni aibu.


Amini usiamini Mkuu, kuna viongozi wametoka kwenye jamii zisizotumia vyoo hata kama ni majumbani mwao, sasa unategemea watakumbuka kujenga kama hata vilivyopo hawavithamini? Kuna siku tulikuwa mochwari ya hospital ya mkoa hapo hapo Morogoro, kila aliyeingia pale choo cha public alitoka bila kujisaidia na kuamua kwenda mtaani kwenye choo za kulipia, kisa ni uchafu uliokithiri wa choo hicho cha hapo mochwari.
 
Jana siku ya Tarehe 5/5/2018 wakati Mh. Rais Magufuli akiendela na Ziara yake Mkoani Morogoro alisimamishwa na wananchi katika Kijiji cha Mang'ula, na hapo ndipo akajitokeza kijana mdogo wa kidato cha kwanza aitwaye Mlindoka Msangi akaelezea changamoto ya vyoo inayoikabili shule yao ya Mang'ula Secondary


Kuna hatari huyo Mkuu wa shule alikotoka mwanafunzi akaandamwa na viongozi wake wanaomzunguka
 
Mambo mengine yanahitaji ubunifu tu.

Mfano shule nyingi za mjini watoto wengi huenda na pesa za matumizi shuleni kwaajiri ya kununulia vyakula.
Kwanini zisitumike hizo fursa kwaajiri kupata pesa ndogo ndogo za kujenga vyoo.
 
Back
Top Bottom