Ujenzi wa barabara ya Kigogo - Tabata

Ujenzi wa barabara ya Kigogo - Tabata

SAUTI YAKO

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2014
Posts
2,947
Reaction score
2,032
Nimeanza kufikiria watoto wadogo wanaolivuta vumbi hili,wafanyabiashara ambao ofisi zao ziko kando ya barabara hii inayojengwa.

Wakuu nyumba za maeneo haya ukiangalia mapaa yake zimefunikwa na vumbi la kifusi kilichosambazwa barabarani.

Ina maana barabara hii haikutengewa bajeti ya kuimwagilia maji kupunguza vumbi.Mradi ni mzuri lakini kumbukeni wananchi wa maeneo haya ni masikini wasioweza kumudu kunywa maziwa kila siku.

Wahusika ninawaagiza ikiwezekana jioni ya leo muanze kumwagilia barabara hizi kwani vumbi hil linaingia hadi kwenye nyumba.

Kuna wakati nilikuwa Mbozi huko Mbeya kulikuwa na mradi ukiendelea wa barabara ya vumbi nilishuhudia ikimwagiwa maji asubuhi na jioni.Iweje miradi ya mjini iwe shida?

Watu wa afya msiishie tu kukagua mazingira machafu kagueni na vitu kama hivi,serikali ya mtaa wa Kigogo/Mkwajuni tuliitoa CCM ili msimamie vile vilivyowashinda tumieni uwezo wenu.

VUMBI HILI NI BAYA SANA
.
 
Nimependa ulipotumia neno 'ninawaagiza'...tukifanikiwa kuwa na mamlaka hayo nchini mwetu hakuna kitakacho shindikana.
Kwa sasa tuliowatuma na kuwapa kazi ndio wanatuagiza...shame!!

Otherwise concern yako ni ya msingi sana
 
Nimependa ulipotumia neno 'ninawaagiza'...tukifanikiwa kuwa na mamlaka hayo nchini mwetu hakuna kitakacho shindikana.
Kwa sasa tuliowatuma na kuwapa kazi ndio wanatuagiza...shame!!

Otherwise concern yako ni ya msingi sana

pamoja mkuu
 
Ni kwel kabisa hali ni mbaya sana na licha ya maji barabara ni fupi sana lkn muda uliotumika had sasa ilitosha kabisa kumaliza lkn had leo wanamwaga vumbi wasilolihudumia
 
Hiyo bajeti ipo na imepitishwa lakini bahati mbaya imepita kwenye mrija wa wenyewe wale wazee wa 40%
 
Hiyo bajeti ipo na imepitishwa lakini bahati mbaya imepita kwenye mrija wa wenyewe wale wazee wa 40%

mkuu kama ni kweli hela ilitengwa tutalifatilia swala haiwezekani wananchi tule vumbi wakati hela ilishatolewa
 
Daaah ile barabara ni disaster nimeipita juzi juzi ni majanga matupu yaani...
 
Daaah ile barabara ni disaster nimeipita juzi juzi ni majanga matupu yaani...
Kwa sasa imekamilika, lami tupu, mambo safi kabisa, naona ile presha ya makame mbarawa imefanya kazi, huu mchepuko ni shortcut ya kufa mtu, wakazi wengi Wa Tabata kwa sasa wana-enjoy mno maisha kwani wanaliepuka lile lifoleni la kishetani pale Buguruni mataa. Hongera JPM..!
 
Back
Top Bottom