Uhuru, Raila wameweza, sisi tunashindwa nini?

Uhuru, Raila wameweza, sisi tunashindwa nini?

Vyamavingi

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2014
Posts
5,983
Reaction score
5,801
Jana ilitolewa taarifa kuwa wapinzani wa siasa za Kenya; Uhuru na Raila walikutana na kumaliza tofauti zao kufuatia uchaguzi mkuu wa 2017.

Baada ya mkutano wao, Rais Uhuru alisema kuwa ni wakati wa kubadili mwelekeo wa siasa za Kenya na kuwa Kenya ni kubwa kuliko mtu yoyote na wao viongozi wanapaswa kukaa pamoja na kujadiliana kwa uhuru kero za nchi.

Kwa upande wake, Raila alisema wamekubaliana na Uhuru kuzima migawanyiko na kuwa pamoja.

Kwa upande wetu Tanzania naona migawanyiko inazidi, Rais naona kama anaamini sana juu ya matumizi ya nguvu ktk kuwadhibiti wenye maoni tofauti na yao na kusababisha msuguano na migawanyiko mkubwa baina ya Rais na wapinzani kiasi kwamba wapinzani wamebanwa sio kwa hoja wala sheria bali kwa kutumia mabavu. Hata vyombo vya habari navyo vinabanwa na kutishwa pale wapoonekana kukosea au kukosoa watawala.

Yanayotokea Ethiopia ambapo pia kwa muda mrefu wapinzani na wenye maoni tofauti na watawala wamebanwa, kutishwa na kufungwa jela naona hayatusaidii. Vurugu zimezozuka huko hazijatusaidia kutufundisha kuwa nguvu hazisaidii bali kujenga ufa miongoni mwa wananchi.

Mimi kama Mtanzania sioni kama hali ya kisiasa ni tete kama ambavyo dola na watawala wanavyosema kwenye kauli zao (Rejea hotuba ya Rais jana, Polisi na CDF). Kauli zao naona kama ndio zinaleta hofu na migongano badala ya umoja na utengemano.

Tujifunze kwa Uhuru na Raila, tuangalie yanayojiri Ethiopia kwa akili. Naomba nimnukuu Mzee Tupatupa : "Tunashindana kwa hoja, bunduki ni za nini? "

Vv
 
Sijasoma lakini si unajua misuguano ndani ya vyama vyetu, ndipo tutoke nje na kusalimiana
 
Watu wanao umiza kichwa kwahili taifa niwachache kuliko mbulula nyingi nyingi ambazo hazijui nyuma wala mbele.hivyo uvumilivu unahitajika sana.
 
Wale wameendelea. Sisi tumerudi nyuma miaka 50 kama alivyosema Ulimwengu!
 
Mimi nilipoona ule upatanisho wake kati ya Ruge na makonda mbele ya mseveni ndiyo nikajua vizuri aina ya Raisi tuliyenaye, uhusiano wenyewe ulikomea palepale baada ya upatanisho
 
Utamsimulia baba yako..
Kauli hizi zinatosha kuonyesha mwelekeo tulipo kama ni sahihi au tumeteleza, Uhuru Kenyatta aliwaambia polisi waacheni waandamane maana ni haki yao; na wangeandamana hadi wachoke. Nyerere pia aliwaambia watawala na Polisi wetu waliokuwa wakipiga na kukamata hovyo wafuasi wa Mtikila miaka ile ya 1990 kuwa wawaache wambebe mtu wao maana anapenda kubebwa kama jeneza na mwishowe walichoka.

Hivi sasa ni vitisho tu ndio vinatawala kana kwamba maandamano ni jambo jipya.

Vv
 
Utamsimulia baba yako..
Katika vijana wehu wewe bila shaka upo kwenye top ten.
Umesoma heading na content vizuri au kifaduro kinakusumbua?
Nyie ndo wale vijana mnaotuma barua za maombi ya kazi ilhali nafasi ni za miaka 2 iliyopita. Kuwa makini ndugu.
 
Jana ilitolewa taarifa kuwa wapinzani wa siasa za Kenya; Uhuru na Raila walikutana na kumaliza tofauti zao kufuatia uchaguzi mkuu wa 2017.

Baada ya mkutano wao, Rais Uhuru alisema kuwa ni wakati wa kubadili mwelekeo wa siasa za Kenya na kuwa Kenya ni kubwa kuliko mtu yoyote na wao viongozi wanapaswa kukaa pamoja na kujadiliana kwa uhuru kero za nchi.

Kwa upande wake, Raila alisema wamekubaliana na Uhuru kuzima migawanyiko na kuwa pamoja.

Kwa upande wetu Tanzania naona migawanyiko inazidi, Rais naona kama anaamini sana juu ya matumizi ya nguvu ktk kuwadhibiti wenye maoni tofauti na yao na kusababisha msuguano na migawanyiko mkubwa baina ya Rais na wapinzani kiasi kwamba wapinzani wamebanwa sio kwa hoja wala sheria bali kwa kutumia mabavu. Hata vyombo vya habari navyo vinabanwa na kutishwa pale wapoonekana kukosea au kukosoa watawala.

Yanayotokea Ethiopia ambapo pia kwa muda mrefu wapinzani na wenye maoni tofauti na watawala wamebanwa, kutishwa na kufungwa jela naona hayatusaidii. Vurugu zimezozuka huko hazijatusaidia kutufundisha kuwa nguvu hazisaidii bali kujenga ufa miongoni mwa wananchi.

Mimi kama Mtanzania sioni kama hali ya kisiasa ni tete kama ambavyo dola na watawala wanavyosema kwenye kauli zao (Rejea hotuba ya Rais jana, Polisi na CDF). Kauli zao naona kama ndio zinaleta hofu na migongano badala ya umoja na utengemano.

Tujifunze kwa Uhuru na Raila, tuangalie yanayojiri Ethiopia kwa akili. Naomba nimnukuu Mzee Tupatupa : "Tunashindana kwa hoja, bunduki ni za nini? "

Vv
Mzee Lowasa alijaribu akaambulia matusi ya nguoni!
 
Jana ilitolewa taarifa kuwa wapinzani wa siasa za Kenya; Uhuru na Raila walikutana na kumaliza tofauti zao kufuatia uchaguzi mkuu wa 2017.

Baada ya mkutano wao, Rais Uhuru alisema kuwa ni wakati wa kubadili mwelekeo wa siasa za Kenya na kuwa Kenya ni kubwa kuliko mtu yoyote na wao viongozi wanapaswa kukaa pamoja na kujadiliana kwa uhuru kero za nchi.

Kwa upande wake, Raila alisema wamekubaliana na Uhuru kuzima migawanyiko na kuwa pamoja.

Kwa upande wetu Tanzania naona migawanyiko inazidi, Rais naona kama anaamini sana juu ya matumizi ya nguvu ktk kuwadhibiti wenye maoni tofauti na yao na kusababisha msuguano na migawanyiko mkubwa baina ya Rais na wapinzani kiasi kwamba wapinzani wamebanwa sio kwa hoja wala sheria bali kwa kutumia mabavu. Hata vyombo vya habari navyo vinabanwa na kutishwa pale wapoonekana kukosea au kukosoa watawala.

Yanayotokea Ethiopia ambapo pia kwa muda mrefu wapinzani na wenye maoni tofauti na watawala wamebanwa, kutishwa na kufungwa jela naona hayatusaidii. Vurugu zimezozuka huko hazijatusaidia kutufundisha kuwa nguvu hazisaidii bali kujenga ufa miongoni mwa wananchi.

Mimi kama Mtanzania sioni kama hali ya kisiasa ni tete kama ambavyo dola na watawala wanavyosema kwenye kauli zao (Rejea hotuba ya Rais jana, Polisi na CDF). Kauli zao naona kama ndio zinaleta hofu na migongano badala ya umoja na utengemano.

Tujifunze kwa Uhuru na Raila, tuangalie yanayojiri Ethiopia kwa akili. Naomba nimnukuu Mzee Tupatupa : "Tunashindana kwa hoja, bunduki ni za nini? "

Vv
Hamu a kilichotokea Kenya, Raila kaufyata kwa kumtambua Rais na kumpa heshima yake. Sisi walishaufyata tangu zamani.
 
Mimi nashangaa sana watu kushikia bango mambo ya Uhuru na Raila ya huko Kenya eti wanalinganisha na mambo ya Tanzania.Ni sawa na kulinganisha kifo na usingizi.Matatizo ya Kenya ni suala ambalo kimataifa liliashaanza kuleta wasiwasi na ndiyo maana limefanyika punde tu kabla ya ziara ya waziri wa mambo ya nje ya Marekani.Hapa kwetu ni tofauti ,kuna vurugu za watu ambao walitaka iwe isiwe wakamate madaraka ili kuendeleza walichokitaka wao na ndio maana walitangaza kwamba wangepata ushindi mapema asubuhi kabla ya saa 4 wakati kura zenyewe zinapigwa mpaka jioni.Mwenyezi Mungu akatuepusha na shari hiyo.Toka wameshindwa wanataka kufanya kila wanaloweza kuichafua Tanzania lakini wanagonga mwamba.Nimemsikia hata Kubenea leo akisema eti Rais wetu anaona aibu kwa Uhuru na Raila kukutana ikulu jana wakati yeye hajafanya hivyo kwa wapinzani.Sasa nikajiuliza huyu kubenea huenda ikawa ana IQ ya kuku kwa sababu amesahau kwamba juzi kati hapa tu Kiongozi na mgombea wao wa urais 2015 Mh. Lowasa aliibukia ikulu bila taarifa yoyote na baada ya hapo alizungumza tena akiwa ikulu kuridhishwa na maendeleo anayoleta rais kwa wananchi wake.Hata huko Kenya hapakuwa na taarifa yoyote ya kukutana kwao ni jambo lililokuja ghafla.Kwa hiyo yaliyofanyika Kenya hapa yameshafanyika hapa kwetu juzi tu. Ajabu iko wapi ?
 
Back
Top Bottom