Uhalisia wa maisha Vs. mbwembwe za CCM

CHIMBULI WA CHIMBULI

JF-Expert Member
Jan 10, 2013
468
160
Habari wanajamvi,

Kwanza ningependa kudurusu maneno maarufu ya wimbo wetu tukufuuu wa " CCM mbele kwa mbele unasema, "CCM ni ile ile oooh! ni ile ile! wataisoma namba."

Sasa mwaka na kitu umepita maisha ya wananchi wengi ni magumu sana toka wapate ridhaa kwa mara nyingine. Kazi nyingi ni za kijungu jiko na ile kaulimbiu ya HAPA KAZI TU kwa sasa haitumiki kwani kazi zilianza tangu enzi za mababu zetu tatizo hapa ni tija katika kazi.

Mbele kwa mbele ya CCM haionekani badala yake kuisoma namba kwa wananchi ndiko kuko dhahiri na ukilalamika wewe ni mpiga dili hata kama hujui hizo dili. serikali imeshindwa kuajiri waalimu wapya Huku ikijaribu kuwanyanyasa wa Sanaa, ilhali wengi wa viongozi wamesoma hayo masomo, .madaktar, manes na kada zngne ajira ni kizungumkuti.

Uchumi wa viwanda hauwezi kufanikiwa kama kilimo bado hakitopewa kipaumbele kwani zaidi ya 80% wanategemea kilimo. CCM haionekani kuwa suluhisho la kweli. Hata zile takwimu za TRA hazionyeshi impact yake watu wanajiuliza serikali imekumbwa na nini? Mbona tunaenda mbele kama tunarudi nyuma? Tunaipenda Tanzania. CCM ijitafakri upya.

Karibuni kwa mjadala.
 
Habari wanajamvi, kwanza ningependa kudurusu maneno maarufu ya wimbo wetu tukufuuu wa " ccm mbele kwa mbele unasema, ccm ni ile ile oooh! ni ile ile! wataisoma NAMBA .
Sasa mwaka na kitu umepita maisha ya wananchi wengi ni magumu Sana toka wapate ridhaa kwa mara nyingine . kazi nyingi ni za kijungu jiko na ile kaulimbiu ya HAPA KAZI TU, kwa Sasa haitumiki kwani kazi zilianza tangu enzi za mababu zetu tatizo hapa ni tija katika kazi. mbele kwa mbele ya ccm haionekani badala yake kuisoma namba kwa wananchi ndiko kuko dhahiri na ukilalamika wewe ni mpiga dili hata kama hujui hizo dili. serikali imeshindwa kuajiri waalimu wapya Huku ikijaribu kuwanyanyasa wa Sanaa, ilhali wengi wa viongozi wamesoma hayo masomo, .madaktar, manes na kada zngne ajira ni kizungumkuti. uchumi wa viwanda hauwezi kufanikiwa kama kilimo bado hakitopewa kipaumbele kwani zaidi ya 80% wanategemea kilimo. ccm haionekani kuwa suluhisho la kweli. Hata zile takwimu za TRA hazionyeshi impact yake watu wanajiuliza serikali imekumbwa na nini? mbona tunaenda mbele Kama tunarudi nyuma? tunaipenda Tanzania. ccm ijitafakri upya. karibuni kwa mjadala.


Unalalamika maisha magumu wakati hakuna unachofanya.Ulidhani kila anayesoma wote anaajiriwa.Jifunze pia kwenye nchi za wengine,unategemea mabadiliko makubwa kwa kila raia kwa kuitegemea Serikali.

Naifananisha tabia hii na mtu mzima aliyekuwa anamtegemea mzazi wake,mzazi alipofariki akaanza kulalamika nitakulaje.

Fikiria kitu cha kufanya nje ya ajira unaposubiri kuajiriwa.Je unajua kuwa shule nyingi binafsi zinaajiri wageni kuliko watanzania.Kama unajua umejiuliza kwa nini? Chukua hatua.
 
Unalalamika maisha magumu wakati hakuna unachofanya.Ulidhani kila anayesoma wote anaajiriwa.Jifunze pia kwenye nchi za wengine,unategemea mabadiliko makubwa kwa kila raia kwa kuitegemea Serikali.

Naifananisha tabia hii na mtu mzima aliyekuwa anamtegemea mzazi wake,mzazi alipofariki akaanza kulalamika nitakulaje.

Fikiria kitu cha kufanya nje ya ajira unaposubiri kuajiriwa.Je unajua kuwa shule nyingi binafsi zinaajiri wageni kuliko watanzania.Kama unajua umejiuliza kwa nini? Chukua hatua.
serikali imefeli kutimiza malengo yake kusema ukweli si kulalamika ila ni kufikisha uhalisia, achana na wasomi wakulima mfno wa mazao ya mbaazi wameuza kilo Moja shilingi 500 Sasa unategemea uchumi wa Kati utafikiwa lini? zinanunuliwa ndege je zinanufaisha Vpi Maisha ya mtu wa chini ambaye anaishi chini ya dola Moja?
 
serikali imefeli kutimiza malengo yake kusema ukweli si kulalamika ila ni kufikisha uhalisia, achana na wasomi wakulima mfno wa mazao ya mbaazi wameuza kilo Moja shilingi 500 Sasa unategemea uchumi wa Kati utafikiwa lini? zinanunuliwa ndege je zinanufaisha Vpi Maisha ya mtu wa chini ambaye anaishi chini ya dola Moja?


Pole kama kiwango hiki cha hoja ni mbadala wa CCM,tunahitaji miaka 1000 mbele kupata mshindani wa CCM.Unaamini kuwa bila ununuzi wa ndege fedha hizo zingenunua mbaazi na kuongeza bei kwa wakulima.

Unaamini kuwa ni jukumu la serikali kuwatafutia masoko wakulima wanaolima bila kujua tutauza wapi na kwa bei gani.

Kweli BWM hakukosea alipowapa majina mnayofana nayo kwa kuambiwa zungusha mikono ,mkazungusha.Mabadiliko,mkaamini yapo mkononi mwa aliyewaambia.Kiongozi sahihi na makini huongoza hata akiwa nje ya madaraka ya nchi,elezeni mnaona serikali kila inachofanya ni hovyo mnaowaamini wanawaongoza kuelekea wapi? wameshinda baadhi ya miji mikubwa leteni mrejesho wa waliyoyafanya kwa kipindi hiki mnachoona tulikosea kutowapa serikali kuu.

Walalamikaji wakuu wapo mijini na mitandaoni,wapiga kura makini wapo shamba hawana muda wa kulalamika bali kutenda.
 
Back
Top Bottom