Uhakiki wa taarifa za mpiga kura

Uhakiki wa taarifa za mpiga kura

Ndalama

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2011
Posts
8,787
Reaction score
6,542
Habari zenu wana jamvi

Mimi nimekuwa nikifuatilia zoezi la uhakiki wa taarifa za mpiga kura maeneo mengi nchini, ninashanganzwa na mtu kwenda na kitambulisho ambacho kilikuwa printed na mashine halafu kwenye data base hakuna taarifa, hivi hii inawezekanaje? Ingekuwa jina halipo kwenye makaratasi tungesema huenda wakati wanayasort kulikuwa na shida lakini chakushangaza hata mtandaoni hayapo

Kwa jinsi hili zoezi linavyoendeshwa la uandikishwaji na kisha kuhakiki ni kama raia wanapewa hisani na sio haki yao kikatiba. Tume wana lengo gani? Mimi siamini kuwa ni mbinu za kuupa upande wowote ushindi lakini swala la kujiuliza ni kwamba hivi kweli sisi watanzania hatuwezi kufanya kwa ukamili jambo dogo kama hili?
 
Ina maana hata kwenye stystem halipo?
:bange:
 
Nashukuru kwa Mada Mimi pia ni muhanga na NEC wamekaa kimya hivi ukisambaza ujumbe fulani watasema Uchochezi sasa kwa Mara ya Pili Tunaomba NEC kutoa taarifa ya uhakiki
 
Naona aibu sana. Kweli katika ya WATZ milioni 47 tumeshindwa kupata watu wa kusaidia kuandikisha majina ya wapiga kura na kutunza hiyo orodh? Hatuwezi kuandika majina ya watu na kuhifadhi kwelii???? AIBU
 
jana nimeenda tegeta kituo nilichojiandikishia ila nikaambiwa kituo cha kuhakiki kipo salasala kilichopo zaidi ya km 5 toka nilipojiandikishia, hii imenifanya nihisi kuna namna nyuma ya pazia, kwanini isiwe kituoni nilipojiandikishia?
 
Back
Top Bottom