Swala la msingi ndugu yangu ni sisi vijana kuungana pamoja na kua na umoja wetu,ambao utakua na nguvu na kutambulika kisheria.
Hii itapaelekea sisi kupata nafasi kwa pamoja kama vijana kuiapproach serikali ambayo inapigia debe swala la KUJIARI hasa ktk kilimo,na kuwaambia haya sasa huu ndo umoja wetu na hii ni miongoni mwa miradi tunayo taka kufanya tunaomba support yenu kifedha,kiushauri,kirasilimali(mfano mashamba) na nk.
Tutambue fika kua kijana mmoja mmoja hana nguvu ya kuiapproach serikali na kukaa nayo meza moja ktk kutatua tatizo hili la ajira,na hata kupata support ya kifedha bila ya kua na umoja wetu.
Hapa nazungumzia mchakato ambao unaendelea hivi sasa ktk kulifikia hili na kuhakikisha linafanikia.Mchakato huu si mwingine ila ni ule wa kuunda UMOJA WA WAHITIMU TAZANIA,karibuni vijana pale mlimani kila jumamosi(saa nane mchana) ktk vikao vinavyo lenga kuwa na umoja huu imara na thabiti kimkakati na kiutendaji.
TUAMKE VIJANA!!!