Ugiriki, India wafanya mazoezi ya pamoja kwenye jeshi la wanamaji kusini mwa Crete

mkalamo

JF-Expert Member
Sep 7, 2013
324
347
Katika Kuimarisha Ushirikiano wao wa Kijeshi,Majeshi ya India na Ugiriki Jumamosi, Septemba 16,2023 walifanya mazoezi ya Pamoja

Mpango huo wa Mazoezi ya Pamoja umelenga kustawisha ushirikiano wao wa Kijeshi kati ya Jeshi la Ugirik (Hellenic Armed Forces) ikiwa ni sehemu ya mpango wake unaohusisha mazoezi ya Pamoja (PASSEX)

Mazoezi hayo yamefanyika kwa kutumia Melivita ya jeshi la wanamaji la Ugiriki na Meli za kivita za Sumedha ya jeshi la wanamaji la India,kwenyeb ukanda wa bahari Kusini mwa mji wa Crete.


Mazoezi ya Pamoja yamezua maswali kuhusu mawasiliano, na mazoezi ya kimedani ya ndege vita ambayo yamefanyika, miongoni mwa maswali hayo ni je huo ni muendelezo wa shughuli za Pamoja za ushirikiano kati ya Ugiriki na India wanazofanya Pamoja ama kuna jambo jengine.

Hata hivyo Ushiriki wa vikosi vya anga vya India kwa mara ya kwanza vilionekana katika mazoezi ya Kimataifa ya “INHIOHOS 23” ambapo ndegevita aina ya SU-30 ilionekana kuthibitisha ukaribu wa vyombo vya Ulinzi vya mataifa hayo mawili.

Shughuli hizo za kijeshi ni muendelezo wa jitihada za kuongeza ulinzi na utayari katika makabiliano Pamoja na kuhuisha ushirikiano na maelewano kati ya washirika hao wawili kwenye eneo la mahusiano ya kijeshi kati ya Ugiriki na India.
22_sep_01_003-696x464.jpg
22_sep_01_005-696x522.jpg
22_sep_01_008-696x458.jpg
380710378_294777866616413_5242649745161654345_n-696x439%20(1).jpg


Sent from my Infinix X683 using JamiiForums mobile app
 
Wana hofu gani mpaka wafanye mazoezi ya kijeshi pamoja? India na ugiriki zinapakana wapi wakati ziko mbali? Au ugiriki inatishiwa na uturiki na india inatishiwa na pakistan ndio wakaamua kufanya mazoezi pamoja ili kuwatiisha maadui zao?
 
Mtu upo kkoo, ndege ipo mbezi mtu unaanza kusikia kelele zake. Unategemea nini hapo? Ndege mmepewa kama msaada, ndege za miaka ya 60 sijui 70, unataka uje kuingie kwenye battle 2023? Acha ushabiki mkuu. Hamna ndege pale.
Ule mgogoro wetu na Malawi tulitumia hizo hizo kuwatishia inaonekana Malawi wapo nyuma zaidi maana zile ndege sio za kutoa vitisho
 
Umelewa kangara
Majuzi kati hivi, kuna ndege kati ya Congo au Rwanda, yupo mmoja aliipasua ndege ya mwenzie kwa RPG.

Sasa zike ndege zina tofauti gani na hizi mig zetu? Ni zilezile tu. Kama Russia mwenye jets za kisasa, jets zake zinashushwa na manpads stingers, sembuse huu unaoruka unapiga kelele kama honi ya meli.
 
Majuzi kati hivi, kuna ndege kati ya Congo au Rwanda, yupo mmoja aliipasua ndege ya mwenzie kwa RPG.

Sasa zike ndege zina tofauti gani na hizi mig zetu? Ni zilezile tu. Kama Russia mwenye jets za kisasa, jets zake zinashushwa na manpads stingers, sembuse huu unaoruka unapiga kelele kama honi ya meli.
Sema vita za mwanzo wanajeshi wa anga kidogo walikuwa na kausalama ila sasa hili battle la Ukraine na Russia wanajeshi wa anga wana kasheshe videge vyao vinashushwa kama mtu ana angua maembe hata vifaru navyo vinachakwazwa balaah
 
Sema vita za mwanzo wanajeshi wa anga kidogo walikuwa na kausalama ila sasa hili battle la Ukraine na Russia wanajeshi wa anga wana kasheshe videge vyao vinashushwa kama mtu ana angua maembe hata vifaru navyo vinachakwazwa balaah
Acha mzee vifaru, chopers, jets vyote havina usalama kwa vita ya sasa. Sasa hapo tunazungumzia chopers na jets ambazo ni advanced kwa majeshi ya wenzetu, unazungumziaje huu uchafu wa huku kwetu, askari 10 wakiwa na heavy machine gus, wanazidondosha vizuri tu hizi skrepa zetu.
 
Ule mgogoro wetu na Malawi tulitumia hizo hizo kuwatishia inaonekana Malawi wapo nyuma zaidi maana zile ndege sio za kutoa vitisho
Sasa kaka unazungumzia malawi nchi masikini kabisa, hata rasilimali hawana. Hawawezi kupewa misaada maana hawana kitu. Mbona hatukuzipeleka Rwanda pale tulipokuwa na mzozo nao mzito.
 
Back
Top Bottom