Uganga wa Tiba ni haramu?

Uganga wa Tiba ni haramu?

Mafanikio 07

Member
Joined
Jun 18, 2019
Posts
57
Reaction score
37
Wanajamvi kongole ziende kwenu kwa kufanikisha JamiiForums iendelee kuwepo bila nyie basi maarifa mtaani hayatapatikana.

Naomba niende mazima kwenye mada yangu ujue siku zote Waafrika kuacha mila zao ni ngumu mno sasa kwa muda huu tuna kitu linaitwa dini ambacho kinatufanya tuishi kupitia tamaduni za Dini ambazo tunaziamini na kuzifata lakn kama ilivyo utofauti wa mawazo basi hata kwenye Dini ipo hii kwamba je ni halali KWA dini mfano usilamu kwenda kwa waganga ambao wanatumia majini na hcho kitabu Cha Qur'an na vengine katika Tiba?

Pia inavyosemekana wengi hutumia majini katika tiba, sasa swali langu pia kukuamini Jini katika upande wa kutoa tiba ni haramu? Kwa kuitakidi Jini ni kiumbe Kama wewe na mpo kwa ajili ya kushirikiana tu na sio kumshirikisha mungu au kumfanya Jini ni mkubwa.

Nimejaribu kufatilia kwa baadhi ya watu lakini sijapata jibu sahihi mipaka Sasa kwani bado madhehebu na mitazamo ya watu hutofautiana lakini mtaani bado.

Nililete kwenu hili.
 
Mtu yeyote akimwacha Mungu wa kweli aliye hai na kwenda kwa mganga, mchawi, wapiga-ramli, wapiga-bao, wabashiri, watazama nyota, nk ili kutafuta tiba ama mafanikio, ni sawa na kuacha kunywa maji safi & salama then akanywa yenye vijidudu vya maradhi all the while akitegemea swift and complete recovery.
 
Uganga ndio tiba sahihi kwa mwanadamu hizo nyingine ni mbadala tu, mfano mtu amelogwa hiv hospital ya kawaida anaweza tibiwa? utapigwa masindano mpaka unauwa figo na ini, na katika kitu wazungu walituweza ni kutuambia kuwa vyakwetu vyote havifai na ni ushirikina. Dini ya asili ya mwafrika ni tambiko. Mtu yeyote anafuata mila na desturi hata kwa mganga huendi maana hakuna anaeweza kukuchezea
 
Uganga ndio tiba sahihi kwa mwanadamu hizo nyingine ni mbadala tu, mfano mtu amelogwa hiv hospital ya kawaida anaweza tibiwa? utapigwa masindano mpaka unauwa figo na ini, na katika kitu wazungu walituweza ni kutuambia kuwa vyakwetu vyote havifai na ni ushirikina. Dini ya asili ya mwafrika ni tambiko. Mtu yeyote anafuata mila na desturi hata kwa mganga huendi maana hakuna anaeweza kukuchezea
Kinga ni bora kuliko kumezeshwa matapishi ya maiti na kuchanjiwa majivu ya mazagazaga. Ukimweka Mungu kibindoni lazima tu akili na mwili wanga wazifukunyue na kutia mafingofingo yao. Ukienda kwa mganga mwingine anafanya kubadilisha spea tu ila ngoma iko palepale.
 
Back
Top Bottom