UGANDA : Mwanamume azikwa na dola 5,700 akamhonge Mungu asimpe hukumu kali siku ya kiyama

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,267
3240cec76a0ef5b735fbcf41a43e7fb7.jpg
Mutumishi wa umma alizikwa na zaidi ya Sh200 milioni za Uganda (Sh5.7 milioni za Kenya) ili akamhonge Mungu asipewe hukumu kali atakapokutana na muumba wake

Bw. Charles Obong mwenye umri wa miaka 52 aliyefanya kazi katika Wizara ya Utumishi wa Umma tangu 2006 hadi 2016, alisemekana alichanga pesa hizo na kuzihifadhi kwa minajili hiyo alipokuwa hai

Alifariki Desemba 17 mwaka uliopita baada ya kuugua kwa muda mrefu akazikwa bomani kwake katika kijiji cha Adag-ani, Kaunti ndogo ya Aromo ilivyo wilayani Lira mkesha wa krismasi

Alizikwa kwa jeneza la chuma linalokadiriwa kugharibu Sh 20 milioni za Uganda

Shemeji yake, Bw David Elic alisema marehemu aliacha wosia na kusema atakapofariki, mke wake Bi. Margaret Obong aweke kiasi kikubwa cha pesa ya jeneza lake

Alipanga kupeleka pesa hizo kwa Mungu ili amsamehe dhambi zake na kumwepusha kwenda kuteketea jahannamu bali apate uzima wa milele

Ilisemekana alimwambia kaka yake, Bw. Justin Ngole na dadake, Bi Hellen Aber wawe mashahidi kuhakikisha mke wake atatimiza agizo hilo lake kikamilifu

Wizara alimofanya kazi ni miongoni mwa zinazokumbwa na sakata kubwa za ufisadi nchini humo mabilioni ya pesa zimewahi kupotelea mifukoni mwa watumishi wa umma

Hata hivyo, Mzee wa ukoo wa Okaba Bw Mike Gulu aliagiza mwili ufukuliwe wiki iliyopita na pesa hizo zikatolewa na kuhifadhiwa kwingine kwa sababu kulingana naye, ni mwiko kuzika watu na pesa pamoja na jeneza.
 
Yaani Nchii yenye watu angali wana kipato cha chini kamà ug huwezi ukazikwa na fetha nyingi kiasihiko....
Bora angesema fetha hizo zisaidi jamii yakee angepata dhawabu kwa mwanyezi MUNGU.
 
Aliyemuambia kuwa aliyemuumba anaitaji apewe pesa ili asitoe adhabu ni nani?

Huenda anajijua ana madhambi mengi ila badala ya kutuubia akalimbikiza pesa.

Wakati wa uhai hatutaki kumuabudu na kutumia muda wetu kama kumshukuru kwa kutuumba kwetu hali ya kuwa tunajua na kuutambua uwepo wake, ona sasa mmoja wetu anavyotaabika na adha ya kuteketeza pesa kwa ujinga alionao, bora angetoa sadaka katika kiasi kidogo cha hayo mamilioni kuliko kuteketea.

Je ikitokea kufukuliwa mwili wake na watu watumie mwanya huo kuchukua hizo pesa ni faida ya nani?
 
Alijijua ni mwizi na mtoa rushwa aliyekubuhu, sijui kwanini hakua na wazo la kumhonga muumba kwa kutubu na kutenda mema.
 
jamani maisha baada y kifo yanatemea umeishije n mungu wk enzi y uhai wako tengeneza njia zako ndg
 
Wana bahati yule mwizi wa majeneza huko Kenya angepata habari hizi wasingekuta chochote...(mwizo huyo kwa sasa ni mlokole!
 
Muendelezo wa kibwetere huo sishangai kama mtu aliwaaminisha watu akawachoma moto huyo nae washa washa wamepita hapo wamedanganya familia wamechukua chao pungufu ndio wamemzika nacho
 
Hana tofauti na wale hujilipua kusudi wakapate mabikira.
 
Back
Top Bottom