Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267

Bw. Charles Obong mwenye umri wa miaka 52 aliyefanya kazi katika Wizara ya Utumishi wa Umma tangu 2006 hadi 2016, alisemekana alichanga pesa hizo na kuzihifadhi kwa minajili hiyo alipokuwa hai
Alifariki Desemba 17 mwaka uliopita baada ya kuugua kwa muda mrefu akazikwa bomani kwake katika kijiji cha Adag-ani, Kaunti ndogo ya Aromo ilivyo wilayani Lira mkesha wa krismasi
Alizikwa kwa jeneza la chuma linalokadiriwa kugharibu Sh 20 milioni za Uganda
Shemeji yake, Bw David Elic alisema marehemu aliacha wosia na kusema atakapofariki, mke wake Bi. Margaret Obong aweke kiasi kikubwa cha pesa ya jeneza lake
Alipanga kupeleka pesa hizo kwa Mungu ili amsamehe dhambi zake na kumwepusha kwenda kuteketea jahannamu bali apate uzima wa milele
Ilisemekana alimwambia kaka yake, Bw. Justin Ngole na dadake, Bi Hellen Aber wawe mashahidi kuhakikisha mke wake atatimiza agizo hilo lake kikamilifu
Wizara alimofanya kazi ni miongoni mwa zinazokumbwa na sakata kubwa za ufisadi nchini humo mabilioni ya pesa zimewahi kupotelea mifukoni mwa watumishi wa umma
Hata hivyo, Mzee wa ukoo wa Okaba Bw Mike Gulu aliagiza mwili ufukuliwe wiki iliyopita na pesa hizo zikatolewa na kuhifadhiwa kwingine kwa sababu kulingana naye, ni mwiko kuzika watu na pesa pamoja na jeneza.