Teleshkova
Member
- Feb 14, 2017
- 76
- 136
Kufuatia ongezeko kubwa la bei ya unga Jijini Dar es Salaam na labda sehemu zingine za nchi, sasa ni bayana kuwa ni rahisi mtu kumudu kula wali kuliko kula ugali. Kilo ya unga katika baadhi ya mitaa inauzwa hadi Sh. 2,200/= ilhali kilo ya mchele inaweza kupatikana kwa Sh. 2,000/=.
Kufuatia hali hii tujiandae kwa yafuatayo:
-ugali kuwa chakula cha sherehe, harusi na matukio mengine maalumu maana si chakula cha gharama?
-wanafunzi na wafungwa kuanza kutumia wali kama chakula kikuu na ugali kama chakula cha anasa
-nyumba kuu yaani familia kufurahia wali huku michepuko wakigeukia ugali maana si ndio chakula cha anasa?
-wataalamu wa mapishi na lishe watalazimika kubuni pilau ya ugali ili ichukue pahala pa pilau ya wali ambayo sasa si chakula aghali na special tena
-kula ugali kila siku kunaweza kupelekea kuikosa mbingu maana ni kupenda anasa za dunia.
NK
[HASHTAG]#liferealities[/HASHTAG]
Kufuatia hali hii tujiandae kwa yafuatayo:
-ugali kuwa chakula cha sherehe, harusi na matukio mengine maalumu maana si chakula cha gharama?
-wanafunzi na wafungwa kuanza kutumia wali kama chakula kikuu na ugali kama chakula cha anasa
-nyumba kuu yaani familia kufurahia wali huku michepuko wakigeukia ugali maana si ndio chakula cha anasa?
-wataalamu wa mapishi na lishe watalazimika kubuni pilau ya ugali ili ichukue pahala pa pilau ya wali ambayo sasa si chakula aghali na special tena
-kula ugali kila siku kunaweza kupelekea kuikosa mbingu maana ni kupenda anasa za dunia.
NK
[HASHTAG]#liferealities[/HASHTAG]