Wakuu huu ufukwe wa seaview yaani barabara ya Obama umeuzwa? Kwa sawa huruhusiwi kuegesha Gari hata kwa sekunde na Kuna kampuni inazunguka zunguka na minyororo kufunga Magari ili ulipishwe faini. Cha ajabu hakuna alama ya katazo la kuegesha maeneo hayo. Hata Kama Kuna katazo sidhani Ni sahihi kuzuia fukwe hizi kwa watu kupumzika ukizingatia eneo lenyewe halina hata maegesho. Cha ajabu ufukwe wa agha khani hospitali Magari yanaegeshwa bila bugudha na hata pembeni ya uwanja wa basketball. Serikali iingilie Kati maana sawa imekuwa kukomoana ili mradi wapata faini.