Ufukwe wa Sea View nani kanunua?

mezanane

Senior Member
Apr 11, 2011
116
185
Wakuu huu ufukwe wa seaview yaani barabara ya Obama umeuzwa? Kwa sawa huruhusiwi kuegesha Gari hata kwa sekunde na Kuna kampuni inazunguka zunguka na minyororo kufunga Magari ili ulipishwe faini. Cha ajabu hakuna alama ya katazo la kuegesha maeneo hayo. Hata Kama Kuna katazo sidhani Ni sahihi kuzuia fukwe hizi kwa watu kupumzika ukizingatia eneo lenyewe halina hata maegesho. Cha ajabu ufukwe wa agha khani hospitali Magari yanaegeshwa bila bugudha na hata pembeni ya uwanja wa basketball. Serikali iingilie Kati maana sawa imekuwa kukomoana ili mradi wapata faini.
 
Maeneo kama yale yanapaswa kuwa maeneo ya wazi kwa ajili ya wananchi wote
 
Si kuna ujenzi pale Mkuu? Au upande gani hasa? Lakini, taarifa yako imefika na itafanyiwa kazi Mkuu
 
Back
Top Bottom