babalao 2
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 5,425
- 3,300
Katika kitabu "AFRICA'S ODIOUS DEBTS": HOW FOREIGN LOANS AND CAPITAL FLIGHT BLED A CONTNENT.
Kimeweza kuweka wazi ni jinsi gani UFISADI umedidimiza taifa letu. Kwa kifupi ni kwamba kati ya mwaka 1970 - 2010 kiasi cha Dola za kimarekani 11.4/ bilioni zimetoroshwa nje kutoka Tanzania. Hii ni pesa ambayo imetoroshwa kwa njia mbalimbali na wahusika ni Wawekezaji, wanasiasa, watendaji, maofisa wa jeshi, Usalama wa Taifa na Wafanyabiashara.
Kiasi hicho kingeweza kujenga km 800 za barabara za lami kwa kila mwaka mmoja na kwa gharama za sasa kwa tanzania yenye mtandao wa barabara wa km 85000 tungekuwa tumesogea mbali. Au angalau kuweka umeme kwa vijiji 1300 kwa mwaka tena kwa mikoa iliyo mbali na grid ya taifa kwa kila mwaka mmoja na hyo ni 10% ya vijiji vyote tanzania.
Kwa mtindo huu umepelekea kuwa na watu wachache yapata 30% kumiliki 75% ya pato la taifa. Je hawa 70% ambao ni mafukara kumiliki 25% ya pato la taifa ni haki au yote hii ni kufukarishana tu. Watunga sera za madini gesi na mafuta wote hawa wamegeuka wanyonyaji kwa kuweka sera zinazowajali matajiri na kuwasahau wananchi wa kawaida.
Kumbuka ufisadi mkubwa umefanyika baada ya tafiti za uranium, gesi na mafuta kuanza. Tuache uwoga tutetee rasilimali zetu wenzetu siera leone wametoa amri kurejeshwa kwa mali na fedha zilizofichwa nje ya nchi yao na wameanza utekelezaji wenye mafanikio makubwa. WOGA NDIYO UFUKARA WETU.
Kimeweza kuweka wazi ni jinsi gani UFISADI umedidimiza taifa letu. Kwa kifupi ni kwamba kati ya mwaka 1970 - 2010 kiasi cha Dola za kimarekani 11.4/ bilioni zimetoroshwa nje kutoka Tanzania. Hii ni pesa ambayo imetoroshwa kwa njia mbalimbali na wahusika ni Wawekezaji, wanasiasa, watendaji, maofisa wa jeshi, Usalama wa Taifa na Wafanyabiashara.
Kiasi hicho kingeweza kujenga km 800 za barabara za lami kwa kila mwaka mmoja na kwa gharama za sasa kwa tanzania yenye mtandao wa barabara wa km 85000 tungekuwa tumesogea mbali. Au angalau kuweka umeme kwa vijiji 1300 kwa mwaka tena kwa mikoa iliyo mbali na grid ya taifa kwa kila mwaka mmoja na hyo ni 10% ya vijiji vyote tanzania.
Kwa mtindo huu umepelekea kuwa na watu wachache yapata 30% kumiliki 75% ya pato la taifa. Je hawa 70% ambao ni mafukara kumiliki 25% ya pato la taifa ni haki au yote hii ni kufukarishana tu. Watunga sera za madini gesi na mafuta wote hawa wamegeuka wanyonyaji kwa kuweka sera zinazowajali matajiri na kuwasahau wananchi wa kawaida.
Kumbuka ufisadi mkubwa umefanyika baada ya tafiti za uranium, gesi na mafuta kuanza. Tuache uwoga tutetee rasilimali zetu wenzetu siera leone wametoa amri kurejeshwa kwa mali na fedha zilizofichwa nje ya nchi yao na wameanza utekelezaji wenye mafanikio makubwa. WOGA NDIYO UFUKARA WETU.