doktamathew
Member
- Mar 12, 2013
- 22
- 43
UGONJWA WA TINEA VESICOLOR (PITYRIASIS VERSICOLOR
Imeandaliwa na @doktamathew
Huu ni ugonjwa wa fangasi ya ngozi ambao hupelekea mgonjwa kuwa na mabaka mabaka meupe, meusi na maeneo mekundu mekundu katika ngozi yake, ugonjwa huu hushambulia sana maeneo ya mgongo ,mabegani na mikono juu ya kiwiko(proximal upper extrimities). Ugonjwa huu upo sana na maarufu miongoni mwa watu wengi tu na wengine huiona hali hii kama kawaida
Ugonjwa huu husababishwa na hamira mpenda mafuta aitwae Malasezzia furfur, Malasezzia globosa na Malasezzia sympodialis,hamira huyu hupenda sana kuwashambulia vijana na watu wenye umri wa kati.ugonjwa huu hauhusiani na uchafu ama usafi wa mtu
WALIO KWENYE HATARI YA KUPATA UGONJWA HUU
1) Kuwa kijana au mtu mwenye umri wa kati
2) Utapiamlo
3) Wenye kisukari,saratani na HIV
4) Walio kwenye maeneo ya joto
5) Walio kwenye maeneo yenye unyevu unyevu
6) Ujauzito
7) Watu wenye mvurujiko wa homoni
8) Watu wenye ngozi zenye mafuta
.
Sent using Jamii Forums mobile app
Imeandaliwa na @doktamathew
Huu ni ugonjwa wa fangasi ya ngozi ambao hupelekea mgonjwa kuwa na mabaka mabaka meupe, meusi na maeneo mekundu mekundu katika ngozi yake, ugonjwa huu hushambulia sana maeneo ya mgongo ,mabegani na mikono juu ya kiwiko(proximal upper extrimities). Ugonjwa huu upo sana na maarufu miongoni mwa watu wengi tu na wengine huiona hali hii kama kawaida
Ugonjwa huu husababishwa na hamira mpenda mafuta aitwae Malasezzia furfur, Malasezzia globosa na Malasezzia sympodialis,hamira huyu hupenda sana kuwashambulia vijana na watu wenye umri wa kati.ugonjwa huu hauhusiani na uchafu ama usafi wa mtu
WALIO KWENYE HATARI YA KUPATA UGONJWA HUU
1) Kuwa kijana au mtu mwenye umri wa kati
2) Utapiamlo
3) Wenye kisukari,saratani na HIV
4) Walio kwenye maeneo ya joto
5) Walio kwenye maeneo yenye unyevu unyevu
6) Ujauzito
7) Watu wenye mvurujiko wa homoni
8) Watu wenye ngozi zenye mafuta
.
ITAENDELEA POST IJAYO
Sent using Jamii Forums mobile app