Ufafanuzi kuhusu habari ya fedha mtanda Pi.

Nedd Ludd

Senior Member
May 16, 2023
135
242
Kama ilivyo kawaida JamiiCheck imekuwa ikifuatilia mambo mbalimbali na kuleta mrejesho kama ni kweli au si kweli.

Mimi leo nina jambo ambalo naomba lifuatiliwe na kuleta majibu kama ni sahihi.

Kuna jambo ambalo limekuwa likizunguka kuhusiana na sarafu ya kimtandao, wanadai kwamba sarafu hiyo imeanzishwa hivyo kwa sasa inatafuta watumiaji wengi zaidi duniani, sarafu hiyo inatwa Pi.

Na pia wanadai kwamba watu ambao watajiunga kwa sasa watafaidika kwa kuipata sarafu hiyo bure, kwani wanadai sarafu moja ni sawa na fedha ya kitanzania milioni 768 yaani dollar 314,159.

Soma maelezo yao hapa chini


Pi ni nini

Pi ni sarafu mpya ya kidigitali ambayo unaweza kuipata kupitia simu yako ya mkononi.

Kwasasa sarafu hii inapatikana bure. Inatolewa bure ili kuieneza kwa watu wengi zaidi. Kwahiyo ipo katika kipindi cha kutafuta watumiaji wengi zaidi wa sarafu hii duniani kote.

.Kwa kawaida kila sarafu ya kidigitali inapoanza hutolewa bure kabisa, lengo ikiwa ni kupata jamii kubwa ( kupata watumiaji wengi).

*Nanufaika vipi na sarafu hii ya Pi?

Pi ni Fedha kama Fedha zingine.
Isipokuwa kwa sasa fedha hii bado haijazinduliwa rasmi, inazindiliwa ndani ya mwaka huu 2024. Ndipo itaanza kutumika rasmi duniani kote kwa Manunuzi.

Thamani ya Pi 1 ambayo imepitishwa duniani kote (GCV) ni 1Pi = dollar 314,159. Kwa maana ya Pi moja kuwa na kuwa na thamani ya zaidi ya milioni 786 za Tanzania. Thamani hiyo ndiyo inatazamiwa kutumika pi itakapozinduliwa rasmi.

(1) Utaipata sarafu hii kwa kufungua Account ya pi na kuichimba (mining) mara moja kila baada ya masaa 24.

(2) Unaweza kuipata sarafu hii kwa kualika wengine pia.

(3) Utaipata sarafu hii kwa kuwa Ambassador wa pi.

(4) Utaipata sarafu hii kwa kuimarisha security circle ya account yako.
IMG-20240227-WA0001.jpg
 
Back
Top Bottom