Uelewa wa Mambo kwa watangazaji wa hizi FM Radio ni finyu mno

MURUSI

JF-Expert Member
Jun 25, 2013
4,496
8,734
Uwezo wa Ufahamu kwa watangazaji wengi wa hizi FM ni mdogo sana, Mtangazaji anatakiwa kuwa mtu mwenye uelewa mpana sana wa mambo mbali mbali ya Dunia si kwa kusoma habari bali kuyajua kabisa.

Watangazaji wengi ni weupe sana vichwani na asilimia 90 ya vipindi vyao ni ya Udaku mtupu, kama sio kipindi cha Mziki basi ni mambo ya Majungu, Umbea, vipindi ya maana kwao ni labda taarifa za habari basi.

Niliwahi shangaa siku moja mtangazaji wa Radio moja kubwa kabisa ya FM walimuelezea Angela Merkel Chancellor wa Ujerumani kwamba ni Waziri Mkuu wa Ujerumani si kwamba alikosea bali hajui na inaonekana studio nzima walikuwa hawajui kwamba yule ni Chancellor na sio Waziri Mkuu wa Ujerumani.

Ukitaka kujua hili fuatilia vipindi vyao vya kila siku, huwezi wafananisha na watangazaji nguli enzi zile kama wa Radio One au Radio Free Africa, Watangazaji walikuwa full equipped na Dunia.

Hawa wa sasa ni udaku umejaa vichwani mwao
 
Aisee Kuna mmoja alikuwa analazimisha kunihoji ,afu maswali yake Sasa! Mungu ndio anajua!
Siku nyingine Radio Fulani ya Mkoani...kipindi Cha Michezo😃
Mtangazi ,(alikuwa anasoma habari kumhusu Kocha was Namungo ..Hemed Morocco) wakati imecheza na Nkana nafikiri! Basi alichanganya madesa akafikri aliyeandika ile habari alikosea ...khakujua kuwa Morocco n Kocha wa Namungo.Yeye akataka arekebishe haabari azungumzie Morroco Kama Nchi na Nkana imetoka huko!
Alichokiwasilisha ....niliona aibu Mimi!
 
Tatizo umri...
Hapa majuzi tu alipofariki Diego maradonna wachambuzi wa football tena kipindi na redio maarufu kweli walishindwa kumchambua na kumuelezea kwa upana nguli huyo
Wakadai alivyocheza mpira wao walikua bado wadogo,wakategemea zaidi wasikilizaji wachangie uelewa wao
Nikajiuliza hivi mtu kama Dk Riki yu wapi siku hizi?
Bora tubakie na wachache lakini waelewa pongezi kwako mwalimu kashasha

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Nakuunga Mkono Mkuu...

Wengine hatuna taaluma ya Habari,ila tukienda studio nahisi hata wenye Taaluma tunawabwaga chini tuu.

Kumbe haya mambo ni kupata Cheti tuu,Kuna karedio kamoja ka hapa kwetu kalinikera siku moja,sijawahi ifungulia tena.
 
Back
Top Bottom