Uelewa please kuhusu hii interview

Uelewa please kuhusu hii interview

delly

Member
Joined
Mar 24, 2010
Posts
55
Reaction score
6
Habari,-Tunakuhitaji kwenye usaili na mafunzo ya kazi kwa ajili ya nafasi ya kazi uliyoomba.Unatakiwa kuchangia gharama ya Malazi na chakula wakati wa usaili na mafunzo ya kazi ambayo yatafanyika kwa muda wa siku 4 kwa maana ya siku moja(1) ya usaili wa kufahamiana na siku tatu(3) za mafunzo na maelekezo ya kazi,kiasi ni Tsh. 65,000/- kwa muda wote- na unatakiwa kutuma malipo hayo kwa njia ya Airtel Money kwa namba hii 0783438478,malipo hayo yanalipwa mara moja tu na yanatakiwa kutufikia mapema jumapili kabla ya wewe kuanza safari jumatatu ili tuweze kufanya maandalizi kwa ajili ya malazi na chakula chako wakati wa usaili na mafunzo ya kazi kwa muda huo wa siku nne(4).Tafadhali unatakiwa kufika mtwara siku ya jumatatu ili kupokelewe na kufika ofisini kwetu.Usaili na mafunzo ya kazi utafanyika;-Mahali: Ofisini Adexec Oil & Gas MtwaraTarehe: Jumanne 22/09/2014Muda: Jumanne- Kuanzia Saa 02:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni hii ni kwa siku moja(1) ya usaili wa kufahamiana na kuangalia vigezo vya muombaji kaziMuda: Jumatano,Alhamisi kuanzia saa 04:00 asubuhi mpaka saa 11:00 jioni hii ni kwa siku tatu (3) za mafunzo ya kazi kwa vitendo.-Kwa maelezo zaidi wasiliana kwa namba hapo juu. -RegardsKelvin Mabwe. Adexec Oil & Gas-Sent:-friday, sept 19, 2014 at 8:40 AM. From:-" :-"mabwe@adexec.com" <mabwe@adexec.com>Subject:-call for interview
 
Ndugu kimbiza pua yako hapo,ni wizi huo usidhubutu wala kujaribu kutuma hizo pesa,hamna kitu kama hiyo,jamani hz shida za ajira zitatupeleka mbali hadi utu unayeyuka mh! Majanga.
 
unaanzaje kumtumia pesa mtu usiemjua?
umeuliza mtu aliye mtwara akasema hiyo kampuni kama kweli ipo?unajua physical address yao?wana website?na siku zote kampuni inatakiwa kumgharamia mfanyakazi kila kitu,au waambie watumie pesa zao then wakukate kwenye mshahara wako wa kwanza
 
Watu wanapigwa sana na hizi fake jobs... Hakuna company inauoweza kukuhire bila oral face-face interview.
Na kama kuna malipo, say ya visa, transport, malazi nk, wengi hua wanasema ujihudumie then wataku-refund kwenye mshahara...
Usithubutu, utapigwa.
 
kwanza hiyo tarehe 22 ni J3 na wala sio J4! Hao hawatofautiana na wale wa Graduate International Program (GIO)! Mkuu chapa rapa fasterr!
 
Achana nao matapeli wakubwa hao ndugu yang
 
Ha ha ha ha
Nice observation and well put.
How do you send money to a person completely stranger to you?
Is it desparation for employment?
Kumbuka, people who are clever will find a way to get rich through other peoples' desperation.
Don't fall into a trap

Follow hii link uone: https://www.google.co.tz/search?q=s...hannel=sb&gws_rd=cr&ei=5-IbVNOkOovT7Abw6oDoCA

Brother, hizo ni scam tu wanataka kukupiga hela. Nigeria ndio wanaongoza ila sasa na Tanzania naona wasomi wenye modem na Laptop wamekua wengi, ukichukulia vifurushi bei ndogo.
 
Wimbi la ukosefu wa ajira na wasomi kuendelea kua wengi mitaani sasa wameamua kujiajili katika biashara haramu ya utapeli! Wito wangu kwenu: Muwe makini mnaotafuta ajira matapeli wamegundua njia rahisi ya kupata pesa kupitia tatizo la ukosefu wa ajira nchini.
 
Asanten kwa ushaur mana alinipigia nikahoji kuhusu hizo cost kama Nina ndugu mtwara ntatoaje hela akadai ni utaratibu wa kampuni yao ya kichina.
 
kampuni yenye kuhitaji wafanyakazi huwa inajitosa kugharamikia malazi&chakula+posho siku za mwanzo...matapeli wamezagaa mjini kuwa makini wanaibiwaga hadi nguo ulizovaa...!
 
Asante kw kunipatia namba za kumalizia dk. zangu kila siku .......

Grand PA
 
Back
Top Bottom