Gaudensia Kabaka aeleza sababu za kuzuia Ujenzi wa Msikiti UDOM na kuhamisha wafanyakazi wa hapo

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,502
51,098


MY TAKE:

1. Profesa, amesema upo utaratibu ambao wanafunzi husali Mabwenini na madarasani, Japo utaratibu huu ni mzuri lakini ni Convenient zaidi kwa Wanafunzi wa Kikristo kuliko waislamu ambao husali swala tano na pia hujumuika na Staff wengine katika kusali, Je inawezekana vipi Staff na Wanafunzi wakajumuika pamoja mabwenini au madarasani kusali?

2. Siyo convenient kuempty darasa five time a day kupisha Waislamu kufanya ibada zao, Je Chuo kitawaacommodate vipi zaidi ya kuwaruhusu Waislamu kuwa na chumba/nyumba yao ya Ibada ambayo Inawatosheleza kufanya Congregation ya Sala zao tano na Ile ya Ijumaa ambayo wanakuwa wengi sana?

3. Profesa nimeona kwenye hii video huku ukijifanya kuvungavunga kwa maneno umeonekana kustaajabishwa kwa uwepo wa hali ya watu wenye imani ya Kiislamu kwamba walikuwa wamekalia nafasi nyeti kama vile Manager wa Estate, HR n.k, Lakini hebu tusemezane Profesa, Laiti hao watu wote wangekuwa wa imani ya Kikristo ungeona hiyo ni ishu kweli?.

Hivi Profesa unaweza kwa ushahidi kabisakabisa pasipo na chembe ya shaka kuthibitisha kuwa hao watu waliwekwa hapo kwa sababu ya dini yao?

Hivi Profesa tukija katika taasisi zote za umma, tukaanalyse haki bin haki kabisa ni taasisi ngapi ambazo vyeo vimekaliwa na watu wa mrengo wa dini moja?, Je umewahi kuumizwa roho au kuumwa na kichwa kwamba nyingi zinakaliwa na Wakiristo? Sasa ikitokea taasisi moja walioshika hivyo vyeo wengi ni Waislamu kwako inakupa shida?. Au mathalan tukiangalia teuzi za mara kwa mara za taasisi za uteuzi hivi ni watu wa mrengo wa dini ipi wanapata hizo teuzi?, au labda mentality hiyo ya kwako ndiyo msingi mzima wa hizi teuzi zilizolalia watu wa dini moja?

5. Profesa , Ukiwahamisha hao watumishi katika nafasi zao za awali lazima nafasi hizo zitajazwa na watu wengine, na kwa kuwa umeshaonyesha kushangazwa kuwa waliozikalia hizo nafasi huko awali ni Waislamu basi itabidi zijazwe na watu wa dini nyingine most likely kwa nature ya demography ya nchi yetu hao watakaowekwa hapo watakuwa ni Wakiristo maana tayari umeshaonyesha kuwa ni ajabu waislamu kukalia hizo nafasi, Hebu Jiulize Umewahamisha Waislamu unawareplace na Wakiristo, Je kwako hii itakuwa ni sawasawa?, kwamba mahali hapo walipo waislamu wakikalia hizo nafasi ni udini lakini zikikaliwa na Wakiristo haina shida, hivi huoni reverse discrimnation hapo?. Au Profesa unataka tubalance dini za watumishi makazini, lakini Profesa hebu tusaidie tangu lini nchi hii ikapanga post za kazi za watumishi kwa kubalance dini zao makazini?

5. Profesa na wenzako mliofanya huu Uamuzi MUOGOPENI MUNGU ANAWAONA HADI NDANI YA MIOYO YENU

KILICHOPELEKEA MJADALA HUU soma > Uonevu dhidi ya Waislam UDOM: Msikiti wavunjwa, wafanyakazi wanataaluma 11 wahamishwa
 
Chuoni kwetu kulitengwa kaeneo kadogo pengine upana ni futi nne na urefu futi sita kwa ajili ya waislamu. Kalikua kadogo kiasi kwamba kwa pamoja waliweza kusali watu wawili wengine walikua wanasubiri.

Na hakuna aliyewahi kulalamika.

Siku ya Ijumaa walienda kwenye misikiti ya makazi ya watu.

Naona hili swala linataka kua nongwa na halipaswi kua.
 
Kina Mshana Jr. nao wakitaka wapatiwe eneo lao la kuabudia mbona mtakoma!

Na wengine wakipewa mbona haina shida, shida ni pale ambapo hutaki kuwapa wenye kuhitaji eti kwa kisingizio kuwa nikikupa basi na mwingine naye itabidi nimpe. Naye mpe tu kwani shida iko wapi?

UDSM kuna Msikiti na Kanisa, hata Magufuli alifungia ndoa yake katika kanisa la UDSM, uwepo wa kanisa haijawahi kuwa tatizo kwa chuo, Tena basi Msikiti na Kanisa pale main campus viko side by side

Kumbuka, UDOM ina eneo kubwa sana mara nyingi kuliko UDSM lakini UDSM nyumba za ibada zipo
 
Too much hatred against Muslims, hii Islamophobia sijui imetokea wapi katika nchi hii, I trully don't understand.

Hata comment za watu humu zinaonyesha chuki kweli dhidi ya waislamu. That is is very sad!. Na chuki hii nadhani ndo inatrickle hadi kwa watu walioshika nafasi za maamuzi, that is why tunaona maamuzi kama haya yaliyotokea UDOM!
 
Yah hata leo wakikataza serikali kuuza pombe lazima upinge
Kila lazima atetee upande wake bila kuathiri upande mwingine
Duh....mimi mambo ya dini nko nutro
Sipendagi ku base upande fulani licha ya kuwa ni mkristo!
Any sahv nko kwenye I bada ya kupiga mitungiii
Acha nkuache mkuuu

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Japo mimi sio muislamu naomba nitoe neno..

Taasisi kubwa kama UDOM ilipaswa na inapaswa iwe na maeneo maalum ya watu kuabudu kwa sababu ya idadi ya watu waliopo pamoja na ukubwa wa taasisi.

Chuo kikongwe cha Udsm ambacho ni kidogo kwa eneo na uwezo kuchukua watu kulinganisha na UDOM kimeweza kuwa na maeneo ya watu kuabudu iweje taasisi kubwa kama UDOM ishindwe au izuiliwe!.

Je ingekuwa ni kanisa limetoa pesa za ufadhili kanisa lijengwe lingezuiwa.!

Nchi yetu haina dini ila lazima tukubali wanachi tuna imani tofauti ndio maana hata mkuu wa nchi huwa anaomba aombewe..

Ingependeza sana kama wangetenga eneo ambalo msikiti mkubwa na kanisa kubwa litajengwa ili kuwezesha idadi kubwa ya watu waliopo hapo kusali na uzoefu unaonyesha licha kuwa na madhehebu tofauti upo uwezekano wa mkubwa sana wa kanisa moja kubwa kutumika kwa kugawanywa kama inavyofanyika pale Udsm na mambo yakaenda vizuri bila kufukuzana kazi au maneno maneno..

Yote yanawezekana ikiwa tuu utaratibu maalumu ukawekwa na kuzingatiwa.
 
Japo mimi sio muislamu naomba nitoe neno..

Taasisi kubwa kama UDOM ilipaswa na inapaswa iwe na maeneo maalum ya watu kuabudu kwa sababu ya idadi ya watu waliopo pamoja na ukubwa wa taasisi.

Chuo kikongwe cha Udsm ambacho ni kidogo kwa eneo na uwezo kuchukua watu kulinganisha na UDOM kimeweza kuwa na maeneo ya watu kuabudu iweje taasisi kubwa kama UDOM ishindwe au izuiliwe!.

Je ingekuwa ni kanisa limetoa pesa za ufadhili kanisa lijengwe lingezuiwa.!

Nchi yetu haina dini ila lazima tukubali wanachi tuna imani tofauti ndio maana hata mkuu wa nchi huwa anaomba aombewe..

Ingependeza sana kama wangetenga eneo ambalo msikiti mkubwa na kanisa kubwa litajengwa ili kuwezesha idadi kubwa ya watu waliopo hapo kusali na uzoefu unaonyesha licha kuwa na madhehebu tofauti upo uwezekano wa mkubwa sana wa kanisa moja kubwa kutumika kwa kugawanywa kama inavyofanyika pale Udsm na mambo yakaenda vizuri bila kufukuzana kazi au maneno maneno..

Yote yanawezekana ikiwa tuu utaratibu maalumu ukawekwa na kuzingatiwa.
Naunga mkono hoja mkuu,wamekosea sana,yaani ramani ya chuo kama udom hakuna sehemu za ibada?
 
Back
Top Bottom