Der Spiegel
Member
- Aug 4, 2016
- 20
- 9
Wakati wa mchakato wa kutengeneza mya, tuliona jinsi utawala wa Kikwete ulivyokatisha ndoto kubwa ya watanzania wengi wenye uelewa kupata Katiba ya Warioba iliyokuwa na maudhui mengi yaliyokuwa yakipendelewa sana na ''ma-elites'' nchi nzima. Hata hivyo, wengi walifurahia sana baada ya mchakato wa kuipigia kura katiba hiyo pendekezwa uliposhindikana.
Hata hivyo ukichunguza kwa makini kampeni za vyama vya upinzani katika kipindi kile cha kuhamasisha umma cha 2014, utagundua kuwa masuala mengi ambayo vyama vya upinzani hasa CHADEMA, vilivyokuwa vikiyapigania, yameanza kushughulikiwa na Rais John Pombe Magufuli kwa namna ambayo si mimi, wala mwana-CCM ama mpinzani aliyetarajia huyu jamaa angeyafanya yote hayo na ndani ya kipindi kifupi sana.
Kwa ajili ya kupanua mjadala, tushirikiane tuyajadili vyema ili tumhukumu kwa haki Rais huyu.
Hivi tunaifahamu vyema nchi yetu, je ni haki tumhukumu Rais wetu kwa sababu hataki bunge liwe live, au kwa sababu sukari imepanda bei? Uwezo wetu wa kufikiri ndio umeishia hapo ama?
Nikiri wazi mi ni mpenzi mkubwa sana wa plurality katika siasa ambapo hakuna Chama kinacho-dominate vyama vingine. Mwenye uelewa mzuri wa Comparative Politics atakiri kuwa, kati ya CCM na CHADEMA/UKAWA, anayepaswa kushangilia kwa anayoyafanya Rais Magufuli ni CHADEMA/UKAWA kwa sababu anawasomesha namba vibaya sana wana-CCM, huku akitekeleza yale ambayo wapinzani waliyataka.
Nani atasumbuka kuangalia bunge live wakati Rais anaonekana moja kwa moja akitekeleza watu wanayoyataka na hivyo kupelekea bunge kupitisha kila kitu.
Jamani wapinzani nyie ndio mlio win kuliko wana-CCM, fikirieni mara mbili mbili
Binafsi sipingi mipango ya maendelo ya mukulu.. Ila tatizo kuna maamuzi anatoa ambayo hayana tija.. Kuna vitu hivi tunasema uchochezi lakini vnaanzia mikononi mwake.
Kwa mfano hili suala la ukawa kuanzisha kampeni ya ukuta isingekuwepo iwapo raisi angeendelea kuheshimu katiba/sheria , kwa nn rais asilitolee tamko hilo wazo lake wazo lake la kuzuia mikutano, je mikutano kipindi cha utawala wa baba ridhiwani ilizuia juhudi zake za maendeleo??
Suala la kuhamia dodoma. N.k.
Mtazamo wangu
Hapo kweli umesema..Sawa hata mimi ninaamini suala la siasa aliache liendelee bila kubughudhiwa. Ni vizuri vyama viwe huru kufanya siasa lakini ninavyomuona ni kwamba anasumbuka kutokana na kuzunhukwa na watu wengi wasio waaminifu huku wengi wao wakiwa na majeraha ya mirija ya madili yao kukata ghafula.
Ndiyo maana naomba tumsaidie Rais huyu maana ukichambua kwa makini utagundua kuwa ni bahati sana kuwa na Rais wa aina yake - yaani mtu ametokea ndani ya Chama tawala halafu akafanya mageuzi makubwa kiasi hicho? Tujiulize alikuwa na shida hiyo ya kujipendekeza kiasi hicho kiasi cha kutishia nafasi yake ya uenyekiti ndani ya Chama chake.
Hivi kwani vipaumbele vyetu kama taifa ni nini, kwa nini tusimhukumu kwa kuangalia jinsi anavyotumia rasilimali za umma? kuna kigezo kikubwa zaidi ya hicho?
Ukimuita Magufuli dikteta kwani nani anaweza kutudanganya kuwa demokrasia ni nzuri
muda wote? Kati ya Benevolent Dictator na laissez-faire democrat nani mzuri katika nchi za dunia ya tatu?
Jamani wote tunatamani abadilisha baadhi ya masuala kama la uhuru wa kisiasa lakini huyu jamaa bado ni mzuri ile mbaya. Tusisahau kuwa katika jamii za kiafrika, furaha ya wengi (japokuwa hawana ufahamu mzuri) ni zaidi ya furaha ya wachache, na hiyo ndiyo demokrasia.
Binafsi sipingi mipango ya maendelo ya mukulu.. Ila tatizo kuna maamuzi anatoa ambayo hayana tija.. Kuna vitu hivi tunasema uchochezi lakini vnaanzia mikononi mwake.
Kwa mfano hili suala la ukawa kuanzisha kampeni ya ukuta isingekuwepo iwapo raisi angeendelea kuheshimu katiba/sheria , kwa nn rais asilitolee tamko hilo wazo lake wazo lake la kuzuia mikutano, je mikutano kipindi cha utawala wa baba ridhiwani ilizuia juhudi zake za maendeleo??
Suala la kuhamia dodoma. N.k.
Mtazamo wangu
Mkuu unaweza ukaniambia tathmin ya kuhamia dom interms of gharama?Hata suala kuhamia Dodoma kwa wenye uelewa watakubali siyo gumu kihivyo endapo kuna ''will''. Mwaka 1998, wakati Chancellor wa Unermani Gerhard Schroeder ameapishwa madarakani aliharakisha pia kwa namna ya ajabu Makao Makuu kutoka Bonn kwenda Berlin ndani ya muda mfupi (usiseme kuwa ni nchi tajiri) japokuwa Helmut Kohl aliyeiunganisha Ujerumani 1990, alikaa miaka nane zaidi (1990 - 97) bila kuhamishia huko - why? Kwa nini wajerumani walikubali kupeleka Makao Makuu katika eneo masikini nchini humo?
Tunakimbilia kudai mji wa Dodoma hauna miundombinu ya kutosha, sijui nini, wala hiki lakini angalia hizi nk changamoto zilizokumba nchi zote walikohamisha miji mikuu yao - Brazil (Rio to Brasilia), Australia (Sydney to Canberra), India (Delhi to New Delhi), Nigeria (Lagos to Abuja) na mingine mingi.
Hivyo kwenye changamoto na utatuzi wake ndio kipimo kizuri cha kumpima Rais huyu na kum-rank kwa usahihi nafasi yake miongoni mwa marais waliopata kuiongoza nchi yetu.
Nina hamu tu kusikia kauli yetu akitamka kuwa tutaanza upya mchakato wa Katiba mpya. Otherwise hadi sasa mambo yanaenda vizuri tena vizuri sana.
Kwenye Kauli, matamko na matendo yake.
Kasome Katiba ya Nchi utaelewa.
Chadema wanajua ni chama cha msimu kwa nini wajenge ofisi mikoani na wilayani? Wao wanachohitaji ni kupiga hela yote ya ruzuku. Wanakulaje hela yote ya ruzuku...Kwa kufanya maandamano ya fujo ili zipayikane kesi waweze kupiga hela kupitia wanasheria.Vyama vya upinzani hasa Chama kikuu CHADEMA, jifunzeni misingi ya kukubalika kwa wananchi siyo kung'ang'ania watu wa mijini ambao ni obvious huwa ni wafuasi wa mageuzi na wala huwa hawasubiri swagga zenu. Nendeni vijijini muanzishe ofisi zinazofanya kazi la sivyo, vyama hivi vitalazimika kusubiri bahati kama ya Kenya kwamba Chama tawala kisambaratike kwanza ndio kipate wafuasi. Watanzania wengi bado wako vijijini, kwa nini vyama hivi visiende kujenga ofisi za wilaya (kwa kuanzia).
Kuvunja katiba haijawahi kuwa sera ya CHADEMA. Hatukumwambia JPM anyakue sera zetu na sisi atufunge midomo!!! Hata mwanafunzi anayeibia majibu Darasani hawezi kufanya kwa ufanisi kuliko yule anayeibiwa. Angeruhusu akakosolewa angetekeleza vizuri zaidi hizo sera alizoibia.No No NO. I will be the last person to support dictatorship.Wakati wa mchakato wa kutengeneza katiba mpya, tuliona jinsi utawala wa Kikwete ulivyokatisha ndoto kubwa ya watanzania wengi wenye uelewa kupata Katiba ya Warioba iliyokuwa na maudhui mengi yaliyokuwa yakipendelewa sana na ''ma-elites'' nchi nzima. Hata hivyo, wengi walifurahia sana baada ya mchakato wa kuipigia kura katiba hiyo pendekezwa uliposhindikana.
Hata hivyo ukichunguza kwa makini kampeni za vyama vya upinzani katika kipindi kile cha kuhamasisha umma cha 2014, utagundua kuwa masuala mengi ambayo vyama vya upinzani hasa CHADEMA, vilivyokuwa vikiyapigania, yameanza kushughulikiwa na Rais John Pombe Magufuli kwa namna ambayo si mimi, wala mwana-CCM ama mpinzani aliyetarajia huyu jamaa angeyafanya yote hayo na ndani ya kipindi kifupi sana.
Kwa ajili ya kupanua mjadala, tushirikiane tuyajadili vyema ili tumhukumu kwa haki Rais huyu.
Hivi tunaifahamu vyema nchi yetu, je ni haki tumhukumu Rais wetu kwa sababu hataki bunge liwe live, au kwa sababu sukari imepanda bei? Uwezo wetu wa kufikiri ndio umeishia hapo ama?
Nikiri wazi mi ni mpenzi mkubwa sana wa plurality katika siasa ambapo hakuna Chama kinacho-dominate vyama vingine. Mwenye uelewa mzuri wa Comparative Politics atakiri kuwa, kati ya CCM na CHADEMA/UKAWA, anayepaswa kushangilia kwa anayoyafanya Rais Magufuli ni CHADEMA/UKAWA kwa sababu anawasomesha namba vibaya sana wana-CCM, huku akitekeleza yale ambayo wapinzani waliyataka.
Nani atasumbuka kuangalia bunge live wakati Rais anaonekana moja kwa moja akitekeleza watu wanayoyataka na hivyo kupelekea bunge kupitisha kila kitu.
Jamani wapinzani nyie ndio mlio win kuliko wana-CCM, fikirieni mara mbili mbili.
Kwa kweli kwa suala la gharama kutakuwepo changamoto lakini nataka nikuhakikishie, ukifuatilia miradi yote mikubwa na yenye ufanisi nchini na hata nchi za wenzetu, utagundua mingi ilijengwa kwa ''kulazimishana''.Mkuu unaweza ukaniambia tathmin ya kuhamia dom interms of gharama?
Kwa kweli kwa suala la gharama kutakuwepo changamoto lakini nataka nikuhakikishie, ukifuatilia miradi yote mikubwa na yenye ufanisi nchini na hata nchi za wenzetu, utagundua mingi ilijengwa kwa ''kulazimishana''.
Angalia ujenzi wa reli nchini tangu wajerumani hadi wachina na TAZARA, vijiji vya ujamaa, shule za sekondari za kata, maabara za sayansi na hivi karibuni madawati.
Ulaya nako ni vivyo hivyo: Mussolin ndiye aliyejenga miradi mikubwa nchini Italia, Hitler ndiye aliyefundisha dunia namna ya kutengeneza barabara za kisasa za magari ''autobahn''. Simaanishi kuwa naunga mkono madikteta kwa dunia ya leo lakini ukiwa na kiongozi mwenye roho nzuri kwa wananchi suala halitakuwa shida. Suala la gharama litakuwepo tu, tuhamie tu huko tuanze upya nchi iliharibiwa na wachache.
Uwezo wetu wa kufikiri ndio umeishia hapo ama?
Ni aibu na Wendawazimu kumpinga JPM kama Rais, kwani yote anayoyafanya ndiyo ambayo yanamanufaa kwetu Watz, lakini ukimuona mtu tena Mtanzania anampinga Rais ujue kuna mawili; aidha ni Mgonjwa wa akili kama Lisu au ni mmoja wa ndugu wa Mafisadi ya Kaskazini ambayo hayataki kuona viongozi wa juu hususan Rais akitokea Kanda ya ziwa. Kuna ka SACCOS kamoja kamekuwa kakitafuta viongozi wake ambao lazima waoe kwa Muasisi wa SACCOS hiyo, Muasisi mwenyewe ni yule aliyewahi kumtaka Baba wa Taifa kufanya jambo kipumbavu la kushusha thamani ya shilingi ili kukidhi matakwa ya mabepari yaliyokuwa yamempa HONGO muasisi wa SACCOS hiyo.