Udalali huu maofisini utaisha lini?

Udalali huu maofisini utaisha lini?

kalaban

Member
Joined
Oct 21, 2015
Posts
11
Reaction score
0
Jana nilienda kwenye ofisi moja kwa lengo la kupata leseni ya udereva; nimeshapitia process nyingine zote kama inavyotakiwa, lakini nilipofika pale nilipokelewa na mtu aliyeonekana kuwa mhudumu kwa lengo la kunisaidia, mimi sikujali nikamweleza shida yangu, akachukua document zangu na kuanza kuzishughulikia.

Mara kaingia hapa mara katoka, baadae akaja na kuniambia nitoe hela. Mimi sikujali nikaingia mfukoni nkijua kuwa ile ndio gharama ya malipo ya leseni yangu, Kumbe haikuwa hivyo. Yaani ilikuwa ni hela mbali na malipo ya leseni anayogawana na wale wafanyakazi wa ofisi husika sababu amenipokea na kuingia kwenye zile ofisi badala yangu, mwishowe nkaingia gharama Mara mbili.

Inakera sana.
 
Kwa sheria nyote mpo matatani kwa kutoa rushwaa na huyo kupokea ingekua enzi zile mngeenda jela viboko 12 mkiingia 12 mkitoa mkawaonyeshe wake zenu
 
Mkuu chagua Lowassa akomeshe huu upuuzi ambao umelelewa kwa miaka 54 sasa
 
TRA wana entertain ujinga sana kwenye ofisi zao, ila kama hautaki vishoka, ukifika ulizia utaratibu
 
Mimi ht wakinipokea kwa tabasamu lipi...namwitikua salamu naendelea kutafuta huduma mwenyewe wajinga sana hawa vishoka
 
Kuwa na utaratibu wa kwenda fronti mwenyewe kwa kila kitu, usipende mteremko
 
Back
Top Bottom