Uchochezi: Prof. Lipumba 'kama Rais Magufuli'

Uchochezi: Prof. Lipumba 'kama Rais Magufuli'

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Tangu kuingia madarakani, Rais Magufuli hakusafiri kwenda Amerika, Ulaya au Asia. Kwa mujibu wake, 'anasafisha' kwanza nchi humuhumu ndani. Rais Magufuli amebaki nchini, achilia mbali kwenda Kenya, Uganda na Rwanda. Ni hapa hapa kwanza hadi kunyooke na kusafishika.

Kama alivyo Rais, Mwenyekiti-wa-Msajili wa CUF, Prof. Lipumba naye amekuwa wa kubaki Ofisi za CUF Buguruni tu. Tangu atambuliwe na Msajili kufuatia kujiuzulu na 'kurejea kwake madarakani', Prof. Lipumba hakuwahi kuvuka bahari na kwenda Zanzibar ambapo CUF ina nguvu hasa.

Ilitegemewa, kwakuwa ndiye Mwenyekiti-wa-Msajili halali, Prof. Lipumba angekwenda Zanzibar na mikoa mingine kutamba mikutanoni katika kujenga na kuimarisha CUF yake. Kwanini Mwenyekiti asitambe na CUF yake atakavyo? Au naye,kama Rais Mafuguli, bado anasafisha CUF yake akitokea Buguruni? Amakweli, ukistaajabu ya ACT-Wazalendo, utayaona na CUF!

Kupima mkojo na uchochezi wapi na wapi!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kibiti, Pwani)
 
Tangu kuingia madarakani, Rais Magufuli hakusafiri kwenda Amerika, Ulaya au Asia. Kwa mujibu wake, 'anasafisha' kwanza nchi humuhumu ndani. Rais Magufuli amebaki nchini, achilia mbali kwenda Kenya, Uganda na Rwanda. Ni hapa hapa kwanza hadi kunyooke na kusafishika.

Kama alivyo Rais, Mwenyekiti-wa-Msajili wa CUF, Prof. Lipumba naye amekuwa wa kubaki Ofisi za CUF Buguruni tu. Tangu atambuliwe na Msajili kufuatia kujiuzulu na 'kurejea kwake madarakani', Prof. Lipumba hakuwahi kuvuka bahari na kwenda Zanzibar ambapo CUF ina nguvu hasa.

Ilitegemewa, kwakuwa ndiye Mwenyekiti-wa-Msajili halali, Prof. Lipumba angekwenda Zanzibar na mikoa mingine kutamba mikutanoni katika kujenga na kuimarisha CUF yake. Kwanini Mwenyekiti asitambe na CUF yake atakavyo? Au naye,kama Rais Mafuguli, bado anasafisha CUF yake akitokea Buguruni? Amakweli, ukistaajabu ya ACT-Wazalendo, utayaona na CUF!

Kupima mkojo na uchochezi wapi na wapi!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kibiti, Pwani)

Tumeambiwa anafanya kazi ya CCM akimaliza atapewa uwaziri.Siye tupo tunajipiga wine taratibu tukisheherekea ushindi our Lissu the great yuko uraiani.

Najua Mjomba umechukia lakini kunywa chupa tu MNH ipo utapelekwa
 
Ikumbukwe prof Lipumba alikisaliti chama na kuingia mitini!Cha ajabu chama kikafanya vizuri tofauti na matarajio ya Lipumba na waliomtuma!Maalim akashinda Zanzibar na kufanyiwa zengwe!Ulimwengu unalijua hili!
Baada ya hapo wakaona wasipokuwa makini,Cuf itachukua zanzibar!Ukaanzishwa mkakati wa kuimaliza kabla ya 2020!Ndipo hapo Lipumba akarudishwa kwenye game!Akapata usaidizi wa Msajili na kufanikiwa kujipenyeza!Ndio maaba hata ujambazi wa waliotumwa na Lipumba,kushambulia viongozi na waandishi wa habari waliokuwa wanafanya press umekaliwa kimya na mpaka leo lipumba anadunda wakati mtuhumiwa aliyekamatwa kwenye tukio akikiri kutumwa na alikuwa mlinzi wa Lipumba!Hapa wenye akili wanajua ccm na serikali yake wapo nyuma ya Lipumba!
Limekuja sakata hili la lipumba kufukuza wabunge,mchakato umeenda very smooth utadhani hakukuwa na kesi mahakamani juu ya mgogoro wa uongozi!Msajili na Spika wameonesha moja kwa moja kuhusishwa na mpango wa ccm na serikali yake kumtumia lipumba kudhoofisha na kuimaliza CUF!Yote hii ni hofu ya zanzibar kuchukuliwa na CUF!Lipumba katumika kisawasawa na kuweka akili zake mfukoni,njaa imemfanya ageuke mjinga!
WanaCuf ni wakati wa kuchukua maamuzi magumu!Mpiganieni katibu wenu mkuu Maalim Seif ili kukinusuru chama!

NB:"sio kila mzee ana busara na hekima maana hata wapumbav na wajinga huzeeka"!
 
Back
Top Bottom