Uchawi na mafanikio

Uchawi na mafanikio

Emma M Bai

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2019
Posts
223
Reaction score
126
Kuna uhusiano gani kati ya mafanikio yako na uchawi ushirikina?

Mafanikio katika nyanja zote ni lazima nguvu za Giza zihusike ?

Kwa wale mnaotumia nguvu hizo naomba mtupe uzoefu wenu kulingana na eneo lako ulipo na the way uchawi unavyokusaidia

Mungu humlinda anaejilinda je utajilinda vip bila hiz nguvu uchawi lazima uuhusike

Utawezaje kuendesha biashara bila uchawi? Bila kuwa mchawi chuma ulete watakusumbua sana pambana

Kwanini maduka mengine wateja wanakuwa mpaka wanapanga foleni wakati maduka mengine yapo wazi na bidhaa hizo walizopanga folen kusubir zipo kwa maduka mengine sababu ni nini?

Naombeni tuchangie tuache ushabiki hili siyo jukwaa la dini hata me mungu namwamini na ninaamini yupo
 
Sasa mbona iko wazi biashara bila uchawi unajipotezea mda sipati picha rafiki yangu Morogoro alikuwa anafanya biashara inayofanana na frame inayofata ya spair za magari mtaa mmoja yeye hauzi mwenzie anauza kumbe jamaa kafanya mambo wateja wakija jamaa anaonekana anauza kitu chengine kabisa.

Juzi kati hapa nilikuwa Itigi Singida nikaingia lodge moja matata hivi ila kuingia tuuu nikakuta kitanda chini kimezungushiwa bangili pembe nne nikaona isiwe kasi machale yakanicheza nikacheki chini ya uvungu nikaona bakuli nyekundu nikalitoa lahaulaaa nikaona mapande ya damu ndani yake. Nikaona isiwe kesi nikapiga dua zangu nikalala
 
Sasa mbona iko wazi biashara bila uchawi unajipotezea mda sipati picha rafiki yangu Morogoro alikuwa anafanya biashara inayofanana na frame inayofata ya spair za magari mtaa mmoja yeye hauzi mwenzie anauza kumbe jamaa kafanya mambo wateja wakija jamaa anaonekana anauza kitu chengine kabisa.

Juzi kati hapa nilikuwa Itigi Singida nikaingia lodge moja matata hivi ila kuingia tuuu nikakuta kitanda chini kimezungushiwa bangili pembe nne nikaona isiwe kasi machale yakanicheza nikacheki chini ya uvungu nikaona bakuli nyekundu nikalitoa lahaulaaa nikaona mapande ya damu ndani yake. Nikaona isiwe kesi nikapiga dua zangu nikalala
 
Kwanza tofautisha uchawi na uganga.

Uchawi unahusu kuharibu, uganga unahusu kutibu.

Pili MUNGU, ana nguvu sana Tena hazina kipimo tatizo linakuja binadamu tu wadhaifu kufuata kile anachosema kwa 100% ni ngumu na ndipo wachawi wanapatia mwanya kuharibu mambo ya wacha Mungu biashara zikiwemo.

Ndipo unakuta watu wengi huamia kwa waganga.

Ni kweli waganga wanasaidia ila KAMWE usiende kwa mganga kuharibu mambo ya mfanyabiashara mwenzako, sababu kufanya hivyo unajiingiza kwenye Vita, Bali nenda katengeneze biashara yako.

Kuna uhusiano gani kati ya mafanikio yako na uchawi ushirikina?

Mafanikio katika nyanja zote ni lazima nguvu za Giza zihusike ?

Kwa wale mnaotumia nguvu hizo naomba mtupe uzoefu wenu kulingana na eneo lako ulipo na the way uchawi unavyokusaidia

Mungu humlinda anaejilinda je utajilinda vip bila hiz nguvu uchawi lazima uuhusike

Utawezaje kuendesha biashara bila uchawi? Bila kuwa mchawi chuma ulete watakusumbua sana pambana

Kwanini maduka mengine wateja wanakuwa mpaka wanapanga foleni wakati maduka mengine yapo wazi na bidhaa hizo walizopanga folen kusubir zipo kwa maduka mengine sababu ni nini?

Naombeni tuchangie tuache ushabiki hili siyo jukwaa la dini hata me mungu namwamini na ninaamini yupo
 
Kufanikiwa au kushindwa katika biashara ukiwa mtu huru bila kufungamana na nguvu ya kichawi au uganga ni jambo jema zaidi.
 
Hivi uchawi upo huku kwetu Afrika tu au Ulaya magharibi, Amerika kaskazini na Asia mashariki pia upo?

Maana maendeleo makubwa ya teknolojia na biashara yapo kwenye hayo maeneo ila stori za uchawi huwezi kuzisikia.

Kuna kitu hakipo sawa Afrika.
 
Back
Top Bottom