Uchaguzi wa Yanga, Jamal Malinzi sasa jipime.

Jacobus

JF-Expert Member
Mar 29, 2011
4,703
1,724
Jamal Malinzi, rais wa shirikisho la soka nchini, sasa inafaa ajipime. Tokea aingie madarakani kafanya mambo mengi ya kulalamikiwa na soka letu haliendi mbele kama Taifa.

Hivi karibuni tu kuna sakata la kupanga matokeo ya mechi za mwisho ligi daraja la kwanza ambalo pana tetesi yeye kuhusika, wakati hilo likiendelea akajipachika kuhakikisha klabu ya Yanga inafanya uchaguzi wa viongozi wake mwaka huu.

Hata hivo hakuna kilichoendelea mpaka serikali kuingilia kati na wao TFF kupanga utaratibu wa uchaguzi kupitia kamati yake ya uchaguzi. Hivi majuzi tu klabu yenyewe imeweka utaratibu wa uchaguzi ambao hauendani na wa TFF na rais wa klabu hiyo kutoa shutuma dhidi ya TFF kupanga njama za kuhakikisha hagombei nafasi hiyo.

Mambo ni mengi ila naona ni jambo la busara kwa mheshimiwa huyu Jamal Malinzi kama kiongozi wa TFF kuona umuhimu wa kuwajibika. Tukumbuke hata 'electronic ticketing' imeshindikana licha ya maagizo toka kwa Waziri Mkuu na Waziri mwenye dhamana ya michezo. Tafakari kaka.
 
Mvumilieni. Si mlikuwa mnamtetea wakati watu wanahangaika kumzuia?! Na Bado, hadi miaka minne iishe, mtaona dunia ya zambarau! Hata kuita maji hamtaweza, mtaita "mma!"
 
Mvumilieni. Si mlikuwa mnamtetea wakati watu wanahangaika kumzuia?! Na Bado, hadi miaka minne iishe, mtaona dunia ya zambarau! Hata kuita maji hamtaweza, mtaita "mma!"
Mkuu, ni aibu kwa watu waliochini ya taasisi yako kukaidi na kuwa wapo sahihi katika maamuzi na vitendo kuliko wewe!
 
Kwani malinzi Na kule Yanga ana cheo?
Mkuu ni suala la uelewa tu kuwa klabu ya Yanga ipo chini ya TFF hivo viongozi wa klabu hiyo na nyingine wanatakiwa kutii maagizo na miongozo toka TFF, kinyume chake na ikaonekana vilabu vipo sahihi sasa kama wewe ni rais wa TFF unafanya nini hapo?
 
Mkuu, ni aibu kwa watu waliochini ya taasisi yako kukaidi na kuwa wapo sahihi katika maamuzi na vitendo kuliko wewe!
Kwakweli ni aibu, ndio maana watu waliokuwa wanamfahamu Malinzi walijitahidi kumzuia kabla hajaingia ila wakatokea wa kumtetea. Na ndio tunalipishwa gharama ya unafki wetu. Mtu alichemsha kuiongoza klabu ataweza mpira wa nchi nzima?! Na hao yanga wanaujua udhaifu wake, maana ni mwanachama mwenzao. Sijawahi kusikia timu inakigomea chama au shirikisho la soka duniani, ila Tanzania ni kawaida! Alaf timu zikifanya vibaya tunaanza kulalamika! Heshima haipo katika mpira wa Tanzania! Ni uhuni tu, na mahaba ya kipuuzi tu! Na tangu umeanza mtindo wa kurekodi mazungumzo ya watu, ndio vurugu zinazidi! Nchi ya matukio! Baada ya sukari, chura, sasa ni mwendokasi!! Sisi tutaendelea kubutuliwa hadi tushike adabu! Shwain!
 
Back
Top Bottom