Uchaguzi vs Uchunguzi

Uchaguzi vs Uchunguzi

samsonp

Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
41
Reaction score
8
TULIKOTOKA NI MBALI SANA NA TUNAKOKWENDA NI MBALI SANA PIA.Wakati nikiwa mdogo niliamini kila anayeishi nje ya Tanzania maisha yake ni bora kuliko sisi waTanzania,niliposikia mtu anakwenda au anatoka Uganda,Sudan,Malawi niliamini maisha yake hayana matatizo hata kidogo.
Inawezekana kwa sababu ya ugumu wa maisha yetu ya kipindi hicho ya chini ya dola moja yalinifanya niamini kwamba matatizo ya maisha yako Tanzania pekee. Nilipoanza kusoma historia katika elimu ya msingi,ndipo nilipoanza kuamini kwamba tulikotoka ni mbali sana.Nilijaribu kutafakari kuhusu uhuru wa 1961 na muungano wa 1964 sikupata picha,niliendelea kuamini tulikotoka ni mbali hasa nikitazama jinsi taiga letu lilivyojengwa katika misingi ya utu,isiyo na ubaguzi wa dini wala kabila,niliamini tumetoka mbali. Kufuatia sera ya Rais Mkapa ya ubinafsishaji binafsi niliamini tunakokwenda ni mbali sana.Katika kipindi hicho ndipo niliposhuhudia Rais Mkapa akipewa koleo iliyojaa dhahabu pale Mgodi wa dhahabu Nzega.Niliamini tunakokwenda ni mbali sana. Mwaka 2005 ndio mwaka ambao nilibadilika na kuamini kwamba ile safari yetu imekaribia.Maisha bora kwa kila mtanzania,ari mpya nguvu mpya kasi mpya na pia ajira kwa vijana niliamini ndio wakombozi wamefika na muda umewadia.(Maisha bora kwa kila mtanzania PART 1). Baada ya miaka mi5 tu niliamini tumekosea njia na tumerudi nyuma hatua 1000,tunakokwenda ni mbali sana. Kuanzia mwaka 2005-2010 niliamini 100% kwamba hatukutumia kanuni za mabadiliko "principles of changes" na "uchunguzi" na badala yake tulifanya "uchaguzi" pekee.Niliamini "Changes do not happen because there is an announcement" ilikuwa ni muda wa kufanya "uchunguzi" yakinifu na si "uchaguzi pekee". Katika kipindi hicho cha ukubwa wangu niliamini kwamba kama Nyerere aliweza basi Mh Mbowe,Zitto,dkt Slaa na wengine wengi wasingeshindwa kutufikisha kanaani kwa kanuni safi "principles of changes".Ni viongozi shupavu waliohubiri tatizo kubwa linaloendelea kuitafuna Afrika na kusababisha machafuko makubwa mashariki ya kati Arab spring".Afrika nako watu wakizidi kuzikimbia nchi zao kuelekea ulaya. Changes move from what we had known and done through a period of transition to arrive at a desired new way.Mwaka 2015 hatimaye nashuhudia filamu yangu (Maisha bora kwa kila mtanzania part 2) ambayo Star ni Mh Edward Lowassa na washiriki wengine lukuki,naamini tena safari yetu ni ndefu na tumerudi nyuma hatua 2000 tena. Bado niko naiangalia ila ngoja nikusimukie kiduchu kinachoendelea katika Filamu hii. 1.Rushwa na ufisadi havikemewi wala kuhubiriwa tena zaidi ya ahadi za benki ya bodaboda na wakulima. 2.Ukigusia suala la rushwa na ufisadi Leo unaambiwa "lete ushahidi" na kama hauna "kaa kimya". 3.Naona pia kuomba kura kwenye nyumba za ibada sasa ni jambo la kawaida,ukiuliza unajibiwa "tunataka mabadiliko" ukiuliza mabadiliko yapi?..unatukanwa. 4.Namuona Said Kubenea aliyembana Sumaye siku ya kutangaza nia kuhusu kuuzwa nyumba za serikali na sakata zima huku akiachwa kinywa wazi kwa majibu mepesi,Leo jambo hilo kamsukumia magufuli. 5.Wakati naota hayo yote,Mara nashtuka kitandani kwangu lakini pembeni ya kitanda changu kuna TV,nakutana na mgombea amevaa nguo za kijani anasema "atapiga vita rushwa"........??????,nilishangaa TAFAKARI,CHUKUA HATUA
 
Dar es Salaam. Siku moja baada ya CCM
kutoa utafiti wake unaoonyesha
mgombea wao wa urais, Dk John
Magufuli atashinda kwa asilimia 69.3,
baadhi ya wasomi wamesema utafiti huo
umeibua maswali mengi kwa wananchi.
Juzi, chama hicho kilitoa matokeo ya
utafiti wake wa ndani uliofanyika katika
majimbo 246 na kuonyesha kuwa
mgombea wao atashinda kwa asilimia
zaidi ya 50 katika Uchaguzi Mkuu wa
Oktoba 25.
Hata hivyo, utafiti huo haukubainisha
sampuli wala methodolojia waliyotumia.
Walipotafutwa na Mwananchi jana
kutoa maoni yao kuhusu utafiti huo,
baadhi ya wasomi walisema matokeo ya
utafiti yameibua maswali na utata kwa
wananchi.
Dk Frank Tily, ambaye ni mhadhiri wa
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM),
alisema amepata wakati mgumu kuelewa
utafiti huo. “Nimejiuliza maswali mengi
ambayo sijapata majibu,”
“Inawezekana ukawa kweli, lakini
binafsi nina wasiwasi…Unaweza
kujitathimini mwenyewe, lakini vigezo
ulivyotumia visiwe sawa,” alisema.
Alisema ingependeza zaidi kama CCM
ingetumia taasisi nyingine kufanya
utafiti huo, majibu yake yasingeibua
maswali mengi kama ilivyo sasa.
Wakati Dk Tily akisema hayo Dk Hamidu
Shungu wa Chuo Kikuu Huria cha
Tanzania(OUT), alisema: “Tatifi zote
zina misingi yake kwa hivyo ni vyema
tukiheshimu matokeo ya utafiti wao.”
Lakini alisema ukiachilia mbali utafiti
huo, siasa pia zina mbinu nyingi za
kutafuta ushindi.
Alisema njia moja ni kuwafanya watu
waamini jambo fulani, hasa kama
walikuwa wamekata tamaa.
“Kwenye siasa kuna propaganda na
kama chama hakina propaganda basi
siyo chama cha siasa,”alisema.
Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali
(SIKIKA), Irene Kiria alisema utafiti huo
una utata.
“Hawaonyeshi wamefanyaje utafiti wao
na hata hiyo asilimia 69.3 wamepata
wapi,”alisema Kiria.
Alisema hoja zilizotolewa kwenye utafiti
huo hazina mashiko.
“Huwezi kutoa kitu cha kisomi kwa
namna hiyo…utafiti unataratibu
zake,”alisema.
Kiria alisema ni aibu hata mtu wa nje
akisoma utafiti huo, atajiuliza kama nchi
hii ina wasomi au la.
Mhadhiri wa mwingine wa OUT, Hamad
Salim alisema kipindi kama hiki, kila
chama kinatumia mbinu za kisiasa ili
kiungwe mkono na kumshinda mpinzani
wake.
Alisema kwa kawaida unapotoa utafiti
ni lazima ufuate mpangilio unaotakiwa
ikiwamo idadi ya watu, sampuli
uliotumia na lengo la utafiti wako.
“Lakini hawa wenzetu hawakutuambia
mpangalio huo na nani aliyefanya
utafiti, je, aliwahoji watu wa upande
gani CCM au Chadema wakati wa
kuandaa.
“Binafsi naona ni mchezo wa kisiasa wa
kuhakikisha upande wa pili unadhoofika
na ikija kuonekana wameshinda wasema
utafiti wetu wa awali ulionyesha hivyo,”
alisema.
Kwa upande, Mhadhiri wa Idara ya
Sayansi ya Siasa na Utawala wa Umma,
UDSM, Richard Mbunda alisema hizo ni
propaganda za kisiasa kwani utafiti una
kanuni zake hauwezi kukurupuka.
“Ukiweka asilimia 69.3 kwa vyuo, hii ni
sawa na alama ya A inaonyesha ufaulu.
Lakini nilichojiuliza hapa nchini kuna
taasisi huwa zinafanya utafiti kama
Twaweza na Redet, wameishia wapi hadi
vyama vinatoka na utafiti wao wenyewe.
“Hiki kipindi cha kampeni vyama au
chama kina mbinu kinafanya ili kiweze
kuungwa mkono na wananchi ,“ alisema
Mbunda.
Akizungumzia utafiti huo Mjumbe wa
kamati ya kampeni ya CCM, January
Makamba alisema wametumia sampuli
ya watu 400, kila jimbo kupata matokeo
ya utafiti huo, huku wakitumia
methodolojia ya kwenda nyumba kwa
nyumba katika maeneo tofauti kwenye
jimbo husika nchini.
 
Back
Top Bottom