stakehigh
JF-Expert Member
- Aug 9, 2019
- 18,912
- 14,689
Tumefika mwisho wa uchaguzi, baadhi ya ndugu zetu hatupo nao tena, kwa sababu adrenaline iliwaendesha na wao kutaka kuonekana walihusika kufanya fujo
CCM kwa muda mrefu imejulikana kutoa viongozi wenye maamuzi magumu, huenda kwa sasa anahitajika kiongozi shupavu kama Paul Kagame,
Wakati Rais Samia anachukua uongozi kutoka kwa Hayati Dkt. Magufuli, alikuta viongozi wengi wa upinzani wanaishi nje ya nchi, kwa moyo mmoja akaamua kukaa nao chini kuanza ukurasa mpya wa siasa za Tanzania, lakini kama tunavojua wapinzani wa nchi hii ni watu ambao ni waongo miaka yote, Rostam akatumika kama chambo, Kikwete nae akarushiwa kashfa, kwa moyo wa upole wa Dkt Samia leo hii mali nyingi zimechomwa kwa sababu ya taarifa zizizo na uthibitisho kutoka na baadhi ya viongozi wa upinzani
Yote yameshapita lakini napendekeza serikali na vyombo vyote ya usalama kutafakari upya upi mwenendo sahihi wa siasa za wapinzani nchini, wapo wafanyabiashara kama Shabiby walioanza biashara kabla hata hawajafanya siasa, leo hii magari yake yamebaki majivu
Napendekeza vyombo vyote vya usalama vianze uchunguzi pamoja na upelelezi wa chanzo za maadamano haya kufanyika, kila mmoja aliyehusika katika kurudisha nyuma maendeleo ya nchi basi apande mahakamani moja kwa moja, kuna damu mbaya inasambaa ya uzushi, uchochezi katika jamii isiposhuhulikiwa mapema nchi yetu haitakuwa kama mwanzo, Pia ukaribu wa wakenya na tanzania ufikiriwe tena, mimi ni kati ya watu tulioamini wakenya wanahusika asilimia kubwa sana kuchochea vurugu hizi, wapo baadhi waliandamana ili na wao waonekane na wao wameweza kufanya, nashauri wachukuliwe hatua kali kwao na kwa familia zao
Mwisho kabisa ni muda mwafaka wa kuulizana kama kweli tunahitaji hivi vyama vya upinzani ama Dkt. Samia aongeze ukali kidogo angalau kama Magu hatukusikia hizi kelele sijui tunaandamana
CCM kwa muda mrefu imejulikana kutoa viongozi wenye maamuzi magumu, huenda kwa sasa anahitajika kiongozi shupavu kama Paul Kagame,
Wakati Rais Samia anachukua uongozi kutoka kwa Hayati Dkt. Magufuli, alikuta viongozi wengi wa upinzani wanaishi nje ya nchi, kwa moyo mmoja akaamua kukaa nao chini kuanza ukurasa mpya wa siasa za Tanzania, lakini kama tunavojua wapinzani wa nchi hii ni watu ambao ni waongo miaka yote, Rostam akatumika kama chambo, Kikwete nae akarushiwa kashfa, kwa moyo wa upole wa Dkt Samia leo hii mali nyingi zimechomwa kwa sababu ya taarifa zizizo na uthibitisho kutoka na baadhi ya viongozi wa upinzani
Yote yameshapita lakini napendekeza serikali na vyombo vyote ya usalama kutafakari upya upi mwenendo sahihi wa siasa za wapinzani nchini, wapo wafanyabiashara kama Shabiby walioanza biashara kabla hata hawajafanya siasa, leo hii magari yake yamebaki majivu
Napendekeza vyombo vyote vya usalama vianze uchunguzi pamoja na upelelezi wa chanzo za maadamano haya kufanyika, kila mmoja aliyehusika katika kurudisha nyuma maendeleo ya nchi basi apande mahakamani moja kwa moja, kuna damu mbaya inasambaa ya uzushi, uchochezi katika jamii isiposhuhulikiwa mapema nchi yetu haitakuwa kama mwanzo, Pia ukaribu wa wakenya na tanzania ufikiriwe tena, mimi ni kati ya watu tulioamini wakenya wanahusika asilimia kubwa sana kuchochea vurugu hizi, wapo baadhi waliandamana ili na wao waonekane na wao wameweza kufanya, nashauri wachukuliwe hatua kali kwao na kwa familia zao
Mwisho kabisa ni muda mwafaka wa kuulizana kama kweli tunahitaji hivi vyama vya upinzani ama Dkt. Samia aongeze ukali kidogo angalau kama Magu hatukusikia hizi kelele sijui tunaandamana