Askari Kanzu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 4,598
- 1,233
Kenya kuandaa uchaguzi Machi 2013
| 13.01.2012 | 10:00 UTC
Mahakama kuu nchini Kenya imeamuru kuwa uchaguzi mkuu wa nchi hiyo utafanywa katika mwezi Machi mwaka 2013, labda tu kama serikali ya sasa ya muungano itavunjwa kabla ya wakati huo. Tarehe ya uchaguzi mkuu, wa kwanza tangu kuzuka kwa ghasia mbaya zaidi za baada ya uchaguzi miaka minne iliyopita, imeibua mjadala mkali baina ya wanasiasa hasimu wakipendekeza tarehe zinazotofautiana kutoka mwezi Agosti mwaak huu hadi Machi mwaka 2013.
Jaji Isaac Lenaola amesema bunge litamaliza muhula wake tarehe 14 Januari mwaka 2013, na uchaguzi utafanywa katika kipindi cha siku 60 kuanzia januari 15 mwaka 2013. Hata hivyo, aliongeza kuwa uchaguzi huo unaweza kuandaliwa mwaka huu katika siku 60 baada ya serikali ya muungano kuvunjwa kupitia mwafaka wa maandishi baina ya rais na waziri mkuu.
Deutche Welle
| 13.01.2012 | 10:00 UTC
Mahakama kuu nchini Kenya imeamuru kuwa uchaguzi mkuu wa nchi hiyo utafanywa katika mwezi Machi mwaka 2013, labda tu kama serikali ya sasa ya muungano itavunjwa kabla ya wakati huo. Tarehe ya uchaguzi mkuu, wa kwanza tangu kuzuka kwa ghasia mbaya zaidi za baada ya uchaguzi miaka minne iliyopita, imeibua mjadala mkali baina ya wanasiasa hasimu wakipendekeza tarehe zinazotofautiana kutoka mwezi Agosti mwaak huu hadi Machi mwaka 2013.
Jaji Isaac Lenaola amesema bunge litamaliza muhula wake tarehe 14 Januari mwaka 2013, na uchaguzi utafanywa katika kipindi cha siku 60 kuanzia januari 15 mwaka 2013. Hata hivyo, aliongeza kuwa uchaguzi huo unaweza kuandaliwa mwaka huu katika siku 60 baada ya serikali ya muungano kuvunjwa kupitia mwafaka wa maandishi baina ya rais na waziri mkuu.
Deutche Welle