Uchaguzi BAVICHA: Kwanini namuunga mkono Daniel Naftal?

Uchaguzi BAVICHA: Kwanini namuunga mkono Daniel Naftal?

BAN KIMOON

Member
Joined
Aug 28, 2014
Posts
7
Reaction score
1
Zikiwa zimebaki takribani siku 12 kuelekea uchaguzi mkuu BAVICHA, joto la uchaguzi limewapanda wengi wa wagombea na wapambe wao. Katika viunga vya mtaa wa Ufipa na maeneo mengi nchini, mjadala ni juu ya mgombea tishio katika nafasi ya Mwenyekiti ambaye ni ndugu Daniel Naftali, wengine wamefikia hatua ya kumuita "Bwana-ushindi" na wengine wanaonekana kama "wasindikizaji". Leo nadondosha sehemu ndogo ya hoja zangu tele kwanini namuunga mkono:

Kwanza
, anaifahamu vilivyo BAVICHA ukimlinganisha na washindani wake.Anajua BAVICHA imetoka wapi, iko wapi na inahitaji nini kusonga mbele.

Pili,
anakidhi mahitaji ya sasa ya kukipa chama mwenekano wa kutanuka zaidi kimaeneo.

Tatu
, si muumini wa siasa za visasi. Hatafuti Uenyekiti wa BAVICHA kama rungu la kuwagonga washindani wake wa ndani kisiasa, Wazungu wanasema "Hammering from the top".

Nne
, tayari amekuwa tested na chama na hana historia ya usaliti.

Tano
, ni mzoefu kwenye siasa na uongozi. Si mshamba wa siasa za kitaifa kama wengi wa washindani wake.

Sita
, ana maono mapana kwa baraza na chama.

Nitaendele...............................................
 
Tukisema umepokea chochote toka kwake utakataa?..tukisema unatumia uraifiki na kujuana ili kupata uongozi utakataa?...kwanini usikae ukasiliza wagombea wote kisha utajua kuna mgombea bora kuliko kwa hoja na itikadi na ukafanya maamuzi sasa haujasikiliza wengine unakuja na limsimamo lako,.....nyie ndio huwa mnakimbia vyama kisa mgombea wenu kakataliwa au mnahama nae kisa maslai yenu hayajapita......

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Tukisema umepokea chochote toka kwake utakataa?..tukisema unatumia uraifiki na kujuana ili kupata uongozi utakataa?...kwanini usikae ukasiliza wagombea wote kisha utajua kuna mgombea bora kuliko kwa hoja na itikadi na ukafanya maamuzi sasa haujasikiliza wengine unakuja na limsimamo lako,.....nyie ndio huwa mnakimbia vyama kisa mgombea wenu kakataliwa au mnahama nae kisa maslai yenu hayajapita......

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

Ni haki ya kila mtu kuelezea anachokiamini. Halafu ametaja sifa za msingi ambazo hata mimi naamini zinahitajika sana kwa kiongozi wa BAVICHA ajaye. Kosa lake nini? Hayo mawazo ya kuhama chama unayo wewe. Asemacho mtu ndicho kinaujaza moyo wake...!
 
Namuunga mkono BAN KIMOON 100% aona habari yake inaendana na utafiti wangu juu ya wengi waliotangaza nia. Wengi wa wagombea tunawajua uwezo na upungufu wao.Tofauti na WAPAMBE UCHWARA, BAN KIMOON ameeleza kwanini anamuunga mkono DAN, nyie wengine wenye wagombea wenu leteni hoja zenu kutushawishi juu ya uwezo wao si kuporomosha matusi, mind you: ili ni jukwaa la Great Thinkers, HOJA IJIBIWE KWA HOJA
 
Danny hana sifa ni mtandao ule wa kusafirisha videmu kwenda nje pasipo manufaa ya BAVICHA. Danny hatakiwi hata kidogo.........labda tuangalie watu wengine.

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Kila la kheri ila kwangu mimi mh.Ephata Nanyoro anafaa zaidi
 
Uchaguzi huu wa BAVICHA tunatazama zaidi hoja na uwezo wa mgombea.Wale wataalamu wa kuibua kashfa bila ushahidi huku CDM si kwao, tabia hizo wazipeleke kwao Lumumba. Ukimuibulia mgombea tuhuma, tutakuona KILAZA na MAMLUKI kama hutaleta ushahidi wa tuhuma zako.
 
Zikiwa zimebaki takribani siku 12 kuelekea uchaguzi mkuu BAVICHA, joto la uchaguzi limewapanda wengi wa wagombea na wapambe wao. Katika viunga vya mtaa wa Ufipa na maeneo mengi nchini, mjadala ni juu ya mgombea tishio katika nafasi ya Mwenyekiti ambaye ni ndugu Daniel Naftali, wengine wamefikia hatua ya kumuita "Bwana-ushindi" na wengine wanaonekana kama "wasindikizaji". Leo nadondosha sehemu ndogo ya hoja zangu tele kwanini namuunga mkono:

Kwanza
, anaifahamu vilivyo BAVICHA ukimlinganisha na washindani wake.Anajua BAVICHA imetoka wapi, iko wapi na inahitaji nini kusonga mbele.

Pili,
anakidhi mahitaji ya sasa ya kukipa chama mwenekano wa kutanuka zaidi kimaeneo.

Tatu
, si muumini wa siasa za visasi. Hatafuti Uenyekiti wa BAVICHA kama rungu la kuwagonga washindani wake wa ndani kisiasa, Wazungu wanasema "Hammering from the top".

Nne
, tayari amekuwa tested na chama na hana historia ya usaliti.

Tano
, ni mzoefu kwenye siasa na uongozi. Si mshamba wa siasa za kitaifa kama wengi wa washindani wake.

Sita
, ana maono mapana kwa baraza na chama.

Nitaendele...............................................

Inatia huruma sana.....!
 
Danny hana sifa ni mtandao ule wa kusafirisha videmu kwenda nje pasipo manufaa ya BAVICHA. Danny hatakiwi hata kidogo.........labda tuangalie watu wengine.

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums

Eti kwamba?....!
 
Team Wafia Chama Daniel Naftal ...Ndio Mtu Anayefaha Katika Kuendeleze Gurudumu Hili la BAVICHA kwa Sasa ....Naftal Tumaini Letu Kwa Sasa.
 
Danny hana sifa ni mtandao ule wa kusafirisha videmu kwenda nje pasipo manufaa ya BAVICHA. Danny hatakiwi hata kidogo.........labda tuangalie watu wengine

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums

Njoo na hoja, si vihoja na kashfa! Nani kakuambia tupo hapa kwa ajili ya kukashifu watu? Mimi ninazidi kuamini Danny ni jembe. Umeona huna uwezo wa kuchallenge sifa zake umerukia kukashfu. Wewe unatapatapa, huna lolote.
 
Back
Top Bottom