Mwana Mpotevu
Platinum Member
- Sep 7, 2011
- 3,295
- 2,505
Taarifa nilizozipata kutoka kwenye chanzo changu cha kuaminika zinaeleza kuwa kutokana na serikali kukumbwa na ukata mkali, imeamua kuchukua fedha zilizokuwa zipelekwe bodi ya mikopo, na badala yake fedha hizo zimeelekezwa Arumeru kugharamia uchaguzi mdogo wa ubunge.
Kutokana na uamuzi huo, sasa serikali imeamua kusitisha ufunguaji wa vyuo vya elimu ya juu kwasababu bodi ya mikopo haitakuwa na fedha za kuwalipa wanafunzi hao ili waweze kujikimu. Na kwa kuanzia, tayari wanafunzi wa UDSM ambao walikuwa wafungue chuo chao wiki ijayo wametangaziwa wasiripoti chuoni HADI HAPO ITAKAPOTANGAZWA TENA!
Hii inamaanisha kuwa serikali haijui lini itapata fungu jingine kwa ajili ya kulipeleka bodi ya mikopo na kuwawezesha wanafunzi hao kurejea vyuoni. Uamuni huu wa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kuendelea na likizo zao kwa lazima huenda ukavikumba pia vyuo vingine vya elimu ya juu hapa nchini kwa sababu hizohizo.
Narudia tena. Taarifa hizi nimezipata kutoka kwenye chanzo changu cha kuaminika sana ndani ya SERIKALI!
Kutokana na uamuzi huo, sasa serikali imeamua kusitisha ufunguaji wa vyuo vya elimu ya juu kwasababu bodi ya mikopo haitakuwa na fedha za kuwalipa wanafunzi hao ili waweze kujikimu. Na kwa kuanzia, tayari wanafunzi wa UDSM ambao walikuwa wafungue chuo chao wiki ijayo wametangaziwa wasiripoti chuoni HADI HAPO ITAKAPOTANGAZWA TENA!
Hii inamaanisha kuwa serikali haijui lini itapata fungu jingine kwa ajili ya kulipeleka bodi ya mikopo na kuwawezesha wanafunzi hao kurejea vyuoni. Uamuni huu wa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kuendelea na likizo zao kwa lazima huenda ukavikumba pia vyuo vingine vya elimu ya juu hapa nchini kwa sababu hizohizo.
Narudia tena. Taarifa hizi nimezipata kutoka kwenye chanzo changu cha kuaminika sana ndani ya SERIKALI!