Trust None
JF-Expert Member
- Feb 12, 2018
- 1,260
- 4,421
Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC), imetangaza kupokea rufaa ya Ngulangwa Mohamed Mshamu, wa CUF, akipinga kutangazwa kushinda bila kupingwa kwa Mgombea Ubunge wa Chama Cha Mapinduzi CCM, katika Jimbo la Temeke Abdallah Mtolea.
Kwa mujibu wa tume hiyo, walipokea taarifa ya kupingwa kwa ushindi wa Mtolea mara baada ya kutangazwa na msimamizi wa uchaguzi lakini wamedai suala hilo liko nje ya uwezo wao.
" Tume ilipokea malalamiko kwa Ngulangwa Mshamu (CUF) akipinga uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Temeke kumuondoa kwenye orodha ya wagombea Ubunge na kumtangaza mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Abdallah Ally Mtolea kuwa amepita bila kupingwa ."
Aidha taarifa hiyo imesema " kwa mujibu wa kifungu cha 44 cha Sheria ya taifa ya uchaguzi, mgombea akitangazwa kuwa amepita bila kupingwa NEC haina mamlaka juu ya uamuzi wa msimamizi wa uchaguzi ''.
Ubunge wa Mtolea Temeke wapingwa | East Africa Television
-------------
Ni vyema sheria za uchaguzi zikapitiwa upya.
—Msimamizi mkuu wa uchaguzi ni nani?
—Anayemtangaza mshindi ni nani?
—Je, hana uhusiano na NEC?
Niwaombe CUF wapeleke kesi mahakamani, (mtembea bure si sawa na mkaa bure)
Kwa mujibu wa tume hiyo, walipokea taarifa ya kupingwa kwa ushindi wa Mtolea mara baada ya kutangazwa na msimamizi wa uchaguzi lakini wamedai suala hilo liko nje ya uwezo wao.
" Tume ilipokea malalamiko kwa Ngulangwa Mshamu (CUF) akipinga uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Temeke kumuondoa kwenye orodha ya wagombea Ubunge na kumtangaza mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Abdallah Ally Mtolea kuwa amepita bila kupingwa ."
Aidha taarifa hiyo imesema " kwa mujibu wa kifungu cha 44 cha Sheria ya taifa ya uchaguzi, mgombea akitangazwa kuwa amepita bila kupingwa NEC haina mamlaka juu ya uamuzi wa msimamizi wa uchaguzi ''.
Ubunge wa Mtolea Temeke wapingwa | East Africa Television
-------------
Ni vyema sheria za uchaguzi zikapitiwa upya.
—Msimamizi mkuu wa uchaguzi ni nani?
—Anayemtangaza mshindi ni nani?
—Je, hana uhusiano na NEC?
Niwaombe CUF wapeleke kesi mahakamani, (mtembea bure si sawa na mkaa bure)