Two in one.(ndege wawili kwa wakati mmoja)

Two in one.(ndege wawili kwa wakati mmoja)

brytr Nichol

Member
Joined
Nov 10, 2019
Posts
80
Reaction score
84
Habari wajumbe wa jamvi hili kubwa la jamii forum hasa katika hichi kipengele chetu Cha mahusiano.
Nijikite Moja kwa Moja kwenye mada;:
MIMI mdau mwenzenu nipo kwenye michakato ya kutoa mahali ya mkewangu mtarajiwa katikati ya mwaka huu.mipango inaenda sawa kabisa.Kama mjuavyo wanaume tabia zetu tunajuana kwakweli.
kuna binti mmoja,tofauti na huyu ninayetarajia kuwa nae kimaisha nilikua na mahusiano nae Ni kwa muda mrefu lakini hatukua na mipango inayoeleweka kimaisha.Sasa mwanzoni mwa mwezi wa kwanza tulikutana Arusha mahala ambapo nilikua nafanya kazi Basi wadau tukajikuta tunapasha kiporo.sikuchukua tahadhari nikauza mechi na binti akashika mimba.sasa ikawa kimbebe mpk Sasa ninayetarajia kumuoa hajui kuwa nimesababisha tukio.na pia nawaza itakuaje familia ya Yule binti ikisikia pale wakati naenda kutoa mahali huku binti yao Ni mjamzito? Nikiahirisha huyu mkewangu to be itakuaje na ameshawataarifu ndugu zake? Naomba kidogo mawazo yenu wajumbe nafanyaje hapa japo Mimi Kama Mimi maamuzi yangu Ni kuendelea na mipango yangu Kama kawaida nilivyokuwa nimeipanga awali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushauri utapata ila kwa sasa lala kwa maana hautajipatia majibu


Kama unaoa wewe oa yule mwenye ujauzito si hauna mpango nae?! Mwache ajifungue kisha lea mwanao sijaona jambo gumu hapo
 
Badiri Dini kama wewe si Muslim..
Then Oa wote..

Kingine Acha tamaa..
Ridhika na hao hao..
Na Ukisha waoa Tumia uzazi wa Mpango..
 
Ulishalikoroga kamanda.

Hebu fikiria huyo uliyemtandika mimba atakavyojisikia baada ya kusikia kuwa unakwenda kuoa mwanamke mwingine? Ungekuwa ni wewe au kama ni dada yako ungejisikiaje? Yaani sisi wanaume kuna wakati tunakuwa katili sana.

Fanya utakavyofanya ila huko mbele ya safari kutakuwa na mtafaruku tu katika familia yako. Karma !!!
 
OA unaye mpenda zaidi kati ya hao wawili. Sikiliza moyo wako, mengine uta deal nayo mbele kwa mbele. Matatizo tumeumbiwa binadamu. Pole sana.

Mimi pia ilitokea situation kama yako. Sikuoa mwenye ujauzito nikaendelea na mipango ya harusi. Bahati nzuri wakati nakutana na huyu aliye pata ujauzito nilikuwa nimemweka wazi kuwa nina mchumba. I think lengo lake alijua akijipatisha mimba nitamuoa yeye.
 
Ulishalikoroga kamanda.

Hebu fikiria huyo uliyemtandika mimba atakavyojisikia baada ya kusikia kuwa unakwenda kuoa mwanamke mwingine? Ungekuwa ni wewe au kama ni dada yako ungejisikiaje? Yaani sisi wanaume kuna wakati tunakuwa katili sana.

Fanya utakavyofanya ila huko mbele ya safari kutakuwa na mtafaruku tu katika familia yako. Karma !!!
Ni sahihi kabisa mkuu nimeyakoroga sana.ndio maana niliomba ushauri wa mawazo.kwakweli nimekosea Sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
OA unaye mpenda zaidi kati ya hao wawili. Sikiliza moyo wako, mengine uta deal nayo mbele kwa mbele. Matatizo tumeumbiwa binadamu. Pole sana.

Mimi pia ilitokea situation kama yako. Sikuoa mwenye ujauzito nikaendelea na mipango ya harusi. Bahati nzuri wakati nakutana na huyu aliye pata ujauzito nilikuwa nimemweka wazi kuwa nina mchumba. I think lengo lake alijua akijipatisha mimba nitamuoa yeye.
Ooooh mkasa wetu unafanana pia maana nahisi Ni Kama alihitaji niwe na yeye japo na mm pia nilimuweka wazi kuwa kuna mtu Nina mahusiano naye.shida ikatokea ndio hivyo amenibebea mimba.mm kwangu Ni Kama mtihani lakini mwenzangu Ni Kama furaha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom