Mkuu with all due respect dhana ya usalama wa nchi ni kubwa na pana sana. Katika kumfuatilia mtu wakati fulani lazima watu wanafanya upelelezi wajue mpenzi wako ji nani, mnakutana wapi, mnatumia vyakula, au dawa gani na mnanunua wapi muda gani. Je una alama gani za mwilini ambazo zingine ni za faragha, wajue group la damu yako na mwenzio na nduguzo, ikilazimu DNA samples zako na watu wanaohusiana nawe. Una magonjwa gani ya kurithi, ya siri n.k. Huwezi kusanya hizi taarifa bila kuingilia haki ya faragha ya mtu. Lakini kwa sababu ya national security interests ni lazima haki hii iminywe kidogo. Wahalifu wengi wamekamatwa kwa kutumia vitu hivi, ambao wangekuja kuleta madhara makubwa kwa watu wengi labda mamia au maelefu kama pale WTC, Wall street Marekani, au Westgate na Garisa Kenya. Je huoni haki ya wengi kuishi au kutojeruhiwa au kupata ulemavu inazidi haki ya faragha ya few individual au many individuals? Maisha ya watu na faragha kipi kinatakiwa kipewe kipaumbele ktk mizania ya haki? Mambo haya ya kiupelelezi unaoingilia haki ya faragha ya mtu yamezuia matukio mengi mabaya kabla hayajatokea au kujirudia I am talking about preemtive measures using private informations of an individual person under the security radder(i.e.under investigation). Think Big. Kumbuka alivyopatikana Osama Bin Laden.