Tuzo point za Voda kichekesho

Basi mimi nilikuwa na kipindi hicho nina tunzo point 18 nikasema ngoja ninunue umeme wa Elf10 then maisha yasogee, nimefanya transaction naambiwa nina tuzo point 1,325 sina salio la kutosha from there sijawahi hata kuhangaika nao tena
 
Yaan aliyewauzia hii idea nafikiri aliwaza yale ya zimbabwe unamkuta mtu ana milioni 50 lkn iyo mili 50 inanunua mkate tu .ss ndio ya Tuzo point mtu ana lundo la point lkn inatosheleza kununua dak 15 tu au MB 200 tu
 
Achana na vya bure, havipo!
 
Voda wanadhani sisi wateja wao ni Mazezeta. Huwezi kuanzisha promotion ya kijinga kama hii kwa watu wenye akili timamu. Kwa taarifa yenu hata hayo matuzo point yenu siyataki.
Teh teh umeamua kuzira!
 
hivi hizi tuzo point ndizo zilizofanya kuondolewa kwa M pesa gawio? nijuzen mimi sijui chochote!
 
Nilifikiri ni mimi tu nawadiss kumbe ni wengi,nilitaka angalau m pesa elfu 5 nikakumbuka nina matuzo point 18,000+ nabadili naambiwa napata 1,090
Sikutaka kabisaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa nao sasa hivi michosho sana.
 
eti nilikuw ana tuzo point +15,000 nimezitafuta karibu miezi 3 nakuja kujaribu kuziconvert kwenda mpesa ni sawa na sh 1700 duu
 
Mimi nafanya transactions za m pesa over 5M per month alaf kucheki Nina tuzo point hizo elfu tatu pesa wallet cjui 300 nikasema du ni yule mkenya anafanya mambo
 
Unaweza kufanyaje ili wasikutumie mimeseji yao ya tuzo point?maana tunajaziana simu for nothing
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…