Tuyaheshimu majeshi yetu tusiyaogope

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
13,718
14,150
Majeshi yetu yako imara na yanasifiwa kimataifa kutokana na weledi wake lakini pia kutokana na uwezo wake wa kuweza kuchanganyika na raia wao. Hii inawarahisishia uharaka wa kupata habari njema na mbaya za adui.

Miaka yote raia huwa hawaogopi kupanda basi moja na askari wao na kupiga stori bila hofu yoyote. Hii ilituwezesha Tanzania kubaki kuwa kisiwa cha amani. Nadhani tuendelee na utamaduni wetu huu wa kuyaheshimu sana majeshi yetu bila ya kuyaogopa kupita kiasi, Rais Nyerere aliyafanya hivyo na matunda yake tumeyaona.
 
Majeshi yetu yako imara na yanasifiwa kimataifa kutokana na weledi wake lakini pia kutokana na uwezo wake wa kuweza kuchanganyika na raia wao. Hii inawarahisishia uharaka wa kupata habari njema na mbaya za adui.

Miaka yote raia huwa hawaogopi kupanda basi moja na askari wao na kupiga stori bila hofu yoyote. Hii ilituwezesha Tanzania kubaki kuwa kisiwa cha amani. Nadhani tuendelee na utamaduni wetu huu wa kuyaheshimu sana majeshi yetu bila ya kuyaogopa kupita kiasi, Rais Nyerere aliyafanya hivyo na matunda yake tumeyaona.
Hili linafahamika wazi ila kuna dalili za wazi magufuri analichonganisha jeshi na raia na hii ndiyo dalili za kuchezea amani yetu amesahau wengi wa wanajeshi na polisi ni ndugu zetu na tunaishi nao uraiani
 
Hamna hatari kubwa kama uwepo wa distance kati ya raia na jeshi. Ni hatari kubwa zaidi. Mambo mengi yanayotokea kama ni uhalifu raia ndo wanakuwa wa kwanza kufahamu kuna uovu unafanyika sehemu fulani, na kwa sababu kuna ukaribu na wa jeshi na raia ni rahisi sana taarifa kufika kwa wanausalama wetu kwa ajili kuchukua hatua stahili.

Sasa gap ikishakuwepo taarifa hizi kuzipata ni ngumu, maana ninani atakayempigia anayemuogopa na anayeonekana kama adui kwake. Unaanzaje kupeleka taarifa kwa mtu unayehisi kama hakupendi kabisa. Yale mahusiano.mazuri na askari wetu yaendelee kulindwa yasimomolewe.
 
Picha ya mheshimiwa huyu, raisi wa uhabeshi ni ya nchi inayotawaliwa kijeshi japo yeye ni raia. Anapenda sana mavazi ya kijeshi na anamiss zile nyota na medali tu. Anatamani kama angetawala akiwa anavaa hivyo na kupigisha raia kwata. Mambo yawe ni amriamri tu. Ndiyo ipo kichwani kwake. Jeshi likipindua utawala halali huingia mitaani na kuwapigisha kwata raia, wasiokuwa tayari huharakishwa peponi. Ndugu anapenda hali hiyo. Awamu zote nne hatukuona majeshi yakirandaranda mitaani na magari ya dereya kisa eti kuna tishio la UKUTA! Ndugu anatamani sana utawala wa kihivyo. Ikiwa hivyo, raia hawana uhuru na huwaona askari kama miunguwatu. Huyu ndugu hata amesema haoni mantiki ya Polisi jamii. Hataki mjadala kati ya askari na raia. Piga mabomu tu ya machozi. ebo! Tawala zilizopita zilifanya kazi kubwa ya kujenga mahusiano kati ya askari na raia na kwa upanda wa Polisi hicho ni kitu cha muhimu sana ila huyu ndugu anabomoa hilo daraja bila kutafakari madhara yake baada ya kubomoa. Hii mbegu anayopanda kama ikiota kutakuwa na shida kubwa sana katika nchi hiyo ya uhabeshi!!
 
Back
Top Bottom