Mello
Senior Member
- May 7, 2017
- 110
- 207
Nawasalimu Ndugu zangu,
Poleni na Majukumu lakini Hongereni kwa Sikukuu ya Pasaka.
Wiki Mbili zilizopita niliitwa kwenye Interview Katika Kampuni Moja ya Vinywaji Baridi na Bidhaa za Chakula Mkoa wa Pwani. Nikafanya Interview ya Kwanza Kwa Kiswahili, hii ilikua ni mara yangu ya kwanza kufanya Interview kwa Kiswahili, Baadae wakurugenzi wale wakanitaka niwape Mipango na Mikakati yangu ya Jinsi nitakavyo wakwamua hapo walipo kuhakikisha bidhaa zao zinafanya vizuri Sokoni. Wakanitaka niweke kwenye Proposal. Kwavile ni mtaalamu katika hiyo Sekta, sikuona tabu nikarudi Nyumbani nikakaa na laptop yangu, nikaandika Strategies and Action Plan kama walivyonitaka. Nikawatumia kwenye Email, Baadae wakanipigia simu kua wamependa nilichokiandika so wakanitaka Niende kufanya presentation kwa kile nilichowaandikia. Siku ya Tatu ikanibidi niende kufanya Presentation. Kweli nikafanya Vizuri, Japo wakaniomba niibadilishe niiweke kwa Kiswahili, Nikafanya hivyo. Ikabidi tufanye Makubaliano ya Mshahara, nakawatajia kiwango ambacho ningependa kulipwa, wakalialia hapo tukashuka mpaka 2.5M. Sasa mmoja wa wakurugenzi akanitaka niingie Field nione Soko lake likoje, Kwavile nilikua Nipo mtaani tu nikaona isiwe tabu kesho yake nikaingia Sokoni kuangalia Soko lake, Kiukweli halikua zuri kabisa, kuna kazi Ilihitajika. Nilifanya research ndogo tu nikagundua kuna kazi kubwa sana, Kesho yake nikampa Results. Siku ya Tano Nika report ofisini kwakua aliniita Tuongee. Akaanza kunipa Majukumu ya kufanya. Nikamwambia haya Majukumu mbona kama ndo nimeshaanza Kazi? Vipi Kuhusu Mkataba na makubaliano yetu inabidi tuyaweke kwenye Maandishi ili niwe comfortable na ww pia uwe Huru. Hapo ndo bla bla zilipoanza, Mara Mkataba siwezi Kukupa kwa sasa kwakua Mimi sijui uwezo wako, Mara inabidi Tuanze kwanza na Mwezi Mmoja nikuone, na Kwa kipindi hiki itabidi Ujigharamie kila kitu baada ya huo mwezi ndo Tuanze sasa kulipana. Wakati huo amenipa Target ya Mil.200 kwa mwezi. Wakuu sikuamini wale jamaa walivyonibadilikia dakika za mwisho. Ikanibidi niwe kimya nikarudi ofisini kwangu, Baadae nikaita Team yake ya Sales, Nikaanza kuongea nao, Mambo waliyonieleza Ni ya Ajabu sana, nikaenda mbali nikafanya Uchunguzi nikagundua Mimi nilikua ni Sales Manager wa Nne katika Kipindi cha November 2017 mpaka March 2018. Yaani Anachokifanya akigundua wewe ni Potential anakuita vzr kwa Interview, Anakuomba Plan zako una mwandikia kisha anakuita unamuelekeza utafanyaje hizo Plan, Kisha anakutibua ili Uondoke then zile Plan anazitumia yeye, Cha Kusikitisha Bado hafanyi vizuri Sokoni kwasababu hawezi Kuiba Akili zako huo Ndo Ujinga wake. Kingine ni Kwamba Halipi Mishahara Kabisa Vijana wake ukiwaona wanatia Huruma. Ambacho namsifia pamoja na huo Utapeli wake bado ana bidhaa nzuri lakini hawezi na Ameshindwa Kabisa kupenetrate kwenye Soko. So Tuwe Makini na Waajiri wa namna Hii, Ikiwezekana na wakati Sasa wa Kulipwa Commitment Fee. Maana Idea zetu zinatumika Kirahisi hivyo. Niliumia sana nilivyotoa Idea zangu kwa Mtu Mbabaishaji kama huyu.
Poleni na Majukumu lakini Hongereni kwa Sikukuu ya Pasaka.
Wiki Mbili zilizopita niliitwa kwenye Interview Katika Kampuni Moja ya Vinywaji Baridi na Bidhaa za Chakula Mkoa wa Pwani. Nikafanya Interview ya Kwanza Kwa Kiswahili, hii ilikua ni mara yangu ya kwanza kufanya Interview kwa Kiswahili, Baadae wakurugenzi wale wakanitaka niwape Mipango na Mikakati yangu ya Jinsi nitakavyo wakwamua hapo walipo kuhakikisha bidhaa zao zinafanya vizuri Sokoni. Wakanitaka niweke kwenye Proposal. Kwavile ni mtaalamu katika hiyo Sekta, sikuona tabu nikarudi Nyumbani nikakaa na laptop yangu, nikaandika Strategies and Action Plan kama walivyonitaka. Nikawatumia kwenye Email, Baadae wakanipigia simu kua wamependa nilichokiandika so wakanitaka Niende kufanya presentation kwa kile nilichowaandikia. Siku ya Tatu ikanibidi niende kufanya Presentation. Kweli nikafanya Vizuri, Japo wakaniomba niibadilishe niiweke kwa Kiswahili, Nikafanya hivyo. Ikabidi tufanye Makubaliano ya Mshahara, nakawatajia kiwango ambacho ningependa kulipwa, wakalialia hapo tukashuka mpaka 2.5M. Sasa mmoja wa wakurugenzi akanitaka niingie Field nione Soko lake likoje, Kwavile nilikua Nipo mtaani tu nikaona isiwe tabu kesho yake nikaingia Sokoni kuangalia Soko lake, Kiukweli halikua zuri kabisa, kuna kazi Ilihitajika. Nilifanya research ndogo tu nikagundua kuna kazi kubwa sana, Kesho yake nikampa Results. Siku ya Tano Nika report ofisini kwakua aliniita Tuongee. Akaanza kunipa Majukumu ya kufanya. Nikamwambia haya Majukumu mbona kama ndo nimeshaanza Kazi? Vipi Kuhusu Mkataba na makubaliano yetu inabidi tuyaweke kwenye Maandishi ili niwe comfortable na ww pia uwe Huru. Hapo ndo bla bla zilipoanza, Mara Mkataba siwezi Kukupa kwa sasa kwakua Mimi sijui uwezo wako, Mara inabidi Tuanze kwanza na Mwezi Mmoja nikuone, na Kwa kipindi hiki itabidi Ujigharamie kila kitu baada ya huo mwezi ndo Tuanze sasa kulipana. Wakati huo amenipa Target ya Mil.200 kwa mwezi. Wakuu sikuamini wale jamaa walivyonibadilikia dakika za mwisho. Ikanibidi niwe kimya nikarudi ofisini kwangu, Baadae nikaita Team yake ya Sales, Nikaanza kuongea nao, Mambo waliyonieleza Ni ya Ajabu sana, nikaenda mbali nikafanya Uchunguzi nikagundua Mimi nilikua ni Sales Manager wa Nne katika Kipindi cha November 2017 mpaka March 2018. Yaani Anachokifanya akigundua wewe ni Potential anakuita vzr kwa Interview, Anakuomba Plan zako una mwandikia kisha anakuita unamuelekeza utafanyaje hizo Plan, Kisha anakutibua ili Uondoke then zile Plan anazitumia yeye, Cha Kusikitisha Bado hafanyi vizuri Sokoni kwasababu hawezi Kuiba Akili zako huo Ndo Ujinga wake. Kingine ni Kwamba Halipi Mishahara Kabisa Vijana wake ukiwaona wanatia Huruma. Ambacho namsifia pamoja na huo Utapeli wake bado ana bidhaa nzuri lakini hawezi na Ameshindwa Kabisa kupenetrate kwenye Soko. So Tuwe Makini na Waajiri wa namna Hii, Ikiwezekana na wakati Sasa wa Kulipwa Commitment Fee. Maana Idea zetu zinatumika Kirahisi hivyo. Niliumia sana nilivyotoa Idea zangu kwa Mtu Mbabaishaji kama huyu.