Tuwapongeze Wahandisi wa ATCL kwa kuifufua ndege, tusiwabeze

Ngaliba Dume

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
1,710
3,677
Ndani ya siku hizi mbili kumekuwa na taarifa za kufufuka kwa ndege ya ATCL aina ya DH-8 Q300 inayofanya safari zake toka Dar na Kigoma.Tofauti na matarajio ya wengi kuwa tutawapa moyo wahandisi wetu wazawa kwa kitendo hicho,hali imekuwa tofauti...watu wanakashifu na kuwavunja moyo hawa wataalanu wetu wachache waliobaki ambao kwa kweli wamefanya kazi kubwa sana kuirudisha ndege hii angani.

Hali ya kudhoofu kwa shirika la ATCL sio matokeo ya kitengo cha Ufundi(Line Maintanance and Hangar Maintanance) bali ni matokeo ya sera na maamuzi mabovu ya wanasiasa ambao mara nyingi wamekuwa wakaidi kusikiliza ushauri wa Wataalamu.Hata mwaka 2002 wakati Serikali ya awamu ta tatu ilipokuwa inabinafsisha ATCL kwa SOUTH AFRICA AIRWAYS Wataalamu wengi sana walipinga lkn wanasiasa hawakusikia,mpaka SAA(Mkaburu) alipofanikisha "kuliuwa" shirika letu na kuturudishia likiwa taabani wakati la kwake likiwa motomoto.

Wahandisi wa ATCL wanapaswa kupongezwa kwa kutumia utaalamu wao wa ndani tena katika Hangar(Gereji ya ndege) iliyo Tanzania kuifumua ndege yote,kuifanyia matengenezo na baada ya ukaguzi wa kitaalamu toka TCAA ndege imeweza kurudi angani.Hii si kazi ndogo,ni kazi kubwa sana na yenye utaalamu mkubwa,Serikali yetu ingekuwa na sera nzuri juu ya Usafiri wa Anga,Tanzania ingekuwa kitovu cha "Maintanance" kwa ndege za nchi nyingi za jirani maana tuna wataalamu waliobobea ambao ni matokeo ya sera "rafiki" za Mwalimu JK Nyerere juu ya usafiri wa anga.Imefikia wakati mpaka kupaka rangi ndege zetu na kuweka "Location Indicator na flight Registration number" tunapeleka Wilson Airport-Nairobi.

Wataalamu wa anga tulio nao ni wale wa kizazi cha Nyerere,baada ya hapo Serikali zilizofuata hazikujiibidisha kusomesha wataalamu kwa kada za urubani na uhandisi,ukitazama hata ndege ndogo za "General Aviation" zinazotumika na watalii kama "Charter na Schedule flights" marubani wake ni kutoka Kenya,Botswana,Afrika Kusini na nchi za Ulaya,Watanzania hawazidi wanne au watano ambao wapo hapo kwa nguvu za familia zao na baba zao kuwa sehemu ya marubani wa enzi za Nyerere.Itafikia kipindi hata ndege za mashirika binafsi ya ndani kama Precision na Fastjet kuanzia "Cabin Crews,Engineers & Pilots" ni wageni...haka kanchi mchawi gani kakarogaaaaaaaa!!!!!!Miaka hiyo kuanzia ndege za ATCL na zile za Serikali (TANZANIA GVT FLIGHT AGENCY) zilifanyiwa matengenezo hapa hapa ndani ya nchi na watu hawakushangaa,ila leo sbb watu wamezoea kupeleka nje ili wale "per diem" basi hata kazi ya uweledi iliyofanywa na wahandisi wetu tunaibeza.

Ikumbukwe Wahandisi hawa wana leseni za ufundi zinazotambuliwa kimataifa,hivyo kazi wanayoifanya inatambuliwa kimataifa,na mpaka ndege inaruhusiwa kuruka manake imekaguliwa kwa viwango vya kimataifa,tuache kubeza wataalamu wetu wa ndani bali tuwatie moyo,kudorora kwa ATCL sio kwa sabb ya wataalamu bali ni kwasbb ya Wanasiasa-Wafanyabiashara wenye maslahi katika usafiri wa anga,walioamua kuipeleka ATCL ICU ili mashirika yao binafsi yapate kufanya kazi.

Inafikia mahali hata Mashirika makubwa ya kimataifa ya ndege kama Etihad,Emirates,KLM,SwissAir,Oman Air,Qatar nk yanashindwa kupata "Station Engineers" Watanzania wanaoishi Dsm na wanalazimika kuajiri wageni kutoka kwao wakati wangeweza kumuweka "Line Maintanance Engineers" mzawa ili kupunguza ghalama,lkn kwa vile hakuna basi wageni wanajaa ktk nafasi ambazo zilipaswa kuwa za wazawa,ndio wazawa watapatikana wapi wakati "National Career" ambayo ni ATCL wanasiasa-wafanyabiashara waibadirisha na PW???Hatujaandaa kizazi kingine cha wataalamu katika sekta ya usafiri wa anga,tuna vijana wengi wenye vipaji..wenzetu Rwanda na Kenya wanawekeza kwa kasi kwa vijana wao katika usafiri wa anga,leo vijana wengi wadogo katika ukanda wa Afrika mashariki na kati ktk utaalamu wa mambo ya anga wanatoka Rwanda na Kenya,sisi bado tunakimbizana na kuhakikisha kamati ya NISHATI NA MADINI anawekwa chini ya Mbunge wa chama dola wa Viti Maalumu na kamati ya PAC makamu wake ni mtu ambaye hata hesabu za kidato cha pili za Sequency and Series hakuzikokotoa.

Wakati huo ATCL ilichanja mbuga toka Dsm ya Mzizima mpaka Heathrow ya Malkia Elizabeth,tukachanja anga juu kwa juu mpaka Hungary..huko kote ulikuwa ukishuka ni lazima utaona nembo ya ATCL.Tuliazimisha wataalamu ktk nchi jirani kama Msumbiji,Zimbabwe na Namibia.Mwalimu alianzisha Chuo cha Usafari wa Anga (TANZANIA CIVIL AVIATION TRAINING CENTRE) mpaka leo Tunafundisha wataalamu kutoka nchi zote za kusini mwa Afrika,Kati,Mashariki mpaka Magaharibi ya Afrika katika mambo ya "Air Traffic Management,Aerodrome and Grounds Aid,Aviation Meteorology,Aeronautical Information Service and Aviation Security".....Tunafundisha watu wa Air Traffic Controllers kwa nchi nyingi za kimataifa..hii ni kazi ya JK Nyerere.

Tuwashukuru Wahandisi wetu kwa kurudisha DH-8 Q300,Welcome back ATCL "THE WING OF THE KILIMANJARO"....Now our Call Sign and Location Indicator will cross the winds and clouds of our beautiful Land......
 
Mara zote wanaotukwamisha ni wanasiasa, usishangae hiyo ndege itakaa angani wiki mbili tu ukifuatilia utaambiwa vipuri tulivyofunga tulilazimishwa kuvinunua India au China badala ya kuvinunua kwa aliyetengeneza ndege ambaye nadhani ni mkanada kama sijakosea sana, na lengo la mwanasiasa siku zote ni kufanikisha ulaji wake.
 
Hivi Magufuli amesema chochote kuhusu air Tanzania? ?

Anyway asanteni na hongereni kwa kuinyanyua
Ndege yetu.

Inawezekana amewatazama kwa jich:( kali:rolleyes: wakamshitukia wameamua kuchukua hatua wenyewe maana si unajua maumivu ya kukamuliwa bila ganzi na hasa kama huo uvimbe upo sehemu mbaya!!
 
ATCL mnakula kodi zetu bure. Ndege moja wafanyakazi 300 hahaaaaa mnachekesha kweli
 
Ndani ya siku hizi mbili kumekuwa na taarifa za kufufuka kwa ndege ya ATCL aina ya DH-8 Q300 inayofanya safari zake toka Dar na Kigoma.Tofauti na matarajio ya wengi kuwa tutawapa moyo wahandisi wetu wazawa kwa kitendo hicho,hali imekuwa tofauti...watu wanakashifu na kuwavunja moyo hawa wataalanu wetu wachache waliobaki ambao kwa kweli wamefanya kazi kubwa sana kuirudisha ndege hii angani.

Hali ya kudhoofu kwa shirika la ATCL sio matokeo ya kitengo cha Ufundi(Line Maintanance and Hangar Maintanance) bali ni matokeo ya sera na maamuzi mabovu ya wanasiasa ambao mara nyingi wamekuwa wakaidi kusikiliza ushauri wa Wataalamu.Hata mwaka 2002 wakati Serikali ya awamu ta tatu ilipokuwa inabinafsisha ATCL kwa SOUTH AFRICA AIRWAYS Wataalamu wengi sana walipinga lkn wanasiasa hawakusikia,mpaka SAA(Mkaburu) alipofanikisha "kuliuwa" shirika letu na kuturudishia likiwa taabani wakati la kwake likiwa motomoto.

Wahandisi wa ATCL wanapaswa kupongezwa kwa kutumia utaalamu wao wa ndani tena katika Hangar(Gereji ya ndege) iliyo Tanzania kuifumua ndege yote,kuifanyia matengenezo na baada ya ukaguzi wa kitaalamu toka TCAA ndege imeweza kurudi angani.Hii si kazi ndogo,ni kazi kubwa sana na yenye utaalamu mkubwa,Serikali yetu ingekuwa na sera nzuri juu ya Usafiri wa Anga,Tanzania ingekuwa kitovu cha "Maintanance" kwa ndege za nchi nyingi za jirani maana tuna wataalamu waliobobea ambao ni matokeo ya sera "rafiki" za Mwalimu JK Nyerere juu ya usafiri wa anga.Imefikia wakati mpaka kupaka rangi ndege zetu na kuweka "Location Indicator na flight Registration number" tunapeleka Wilson Airport-Nairobi.

Wataalamu wa anga tulio nao ni wale wa kizazi cha Nyerere,baada ya hapo Serikali zilizofuata hazikujiibidisha kusomesha wataalamu kwa kada za urubani na uhandisi,ukitazama hata ndege ndogo za "General Aviation" zinazotumika na watalii kama "Charter na Schedule flights" marubani wake ni kutoka Kenya,Botswana,Afrika Kusini na nchi za Ulaya,Watanzania hawazidi wanne au watano ambao wapo hapo kwa nguvu za familia zao na baba zao kuwa sehemu ya marubani wa enzi za Nyerere.Itafikia kipindi hata ndege za mashirika binafsi ya ndani kama Precision na Fastjet kuanzia "Cabin Crews,Engineers & Pilots" ni wageni...haka kanchi mchawi gani kakarogaaaaaaaa!!!!!!Miaka hiyo kuanzia ndege za ATCL na zile za Serikali (TANZANIA GVT FLIGHT AGENCY) zilifanyiwa matengenezo hapa hapa ndani ya nchi na watu hawakushangaa,ila leo sbb watu wamezoea kupeleka nje ili wale "per diem" basi hata kazi ya uweledi iliyofanywa na wahandisi wetu tunaibeza.

Ikumbukwe Wahandisi hawa wana leseni za ufundi zinazotambuliwa kimataifa,hivyo kazi wanayoifanya inatambuliwa kimataifa,na mpaka ndege inaruhusiwa kuruka manake imekaguliwa kwa viwango vya kimataifa,tuache kubeza wataalamu wetu wa ndani bali tuwatie moyo,kudorora kwa ATCL sio kwa sabb ya wataalamu bali ni kwasbb ya Wanasiasa-Wafanyabiashara wenye maslahi katika usafiri wa anga,walioamua kuipeleka ATCL ICU ili mashirika yao binafsi yapate kufanya kazi.

Inafikia mahali hata Mashirika makubwa ya kimataifa ya ndege kama Etihad,Emirates,KLM,SwissAir,Oman Air,Qatar nk yanashindwa kupata "Station Engineers" Watanzania wanaoishi Dsm na wanalazimika kuajiri wageni kutoka kwao wakati wangeweza kumuweka "Line Maintanance Engineers" mzawa ili kupunguza ghalama,lkn kwa vile hakuna basi wageni wanajaa ktk nafasi ambazo zilipaswa kuwa za wazawa,ndio wazawa watapatikana wapi wakati "National Career" ambayo ni ATCL wanasiasa-wafanyabiashara waibadirisha na PW???Hatujaandaa kizazi kingine cha wataalamu katika sekta ya usafiri wa anga,tuna vijana wengi wenye vipaji..wenzetu Rwanda na Kenya wanawekeza kwa kasi kwa vijana wao katika usafiri wa anga,leo vijana wengi wadogo katika ukanda wa Afrika mashariki na kati ktk utaalamu wa mambo ya anga wanatoka Rwanda na Kenya,sisi bado tunakimbizana na kuhakikisha kamati ya NISHATI NA MADINI anawekwa chini ya Mbunge wa chama dola wa Viti Maalumu na kamati ya PAC makamu wake ni mtu ambaye hata hesabu za kidato cha pili za Sequency and Series hakuzikokotoa.

Wakati huo ATCL ilichanja mbuga toka Dsm ya Mzizima mpaka Heathrow ya Malkia Elizabeth,tukachanja anga juu kwa juu mpaka Hungary..huko kote ulikuwa ukishuka ni lazima utaona nembo ya ATCL.Tuliazimisha wataalamu ktk nchi jirani kama Msumbiji,Zimbabwe na Namibia.Mwalimu alianzisha Chuo cha Usafari wa Anga (TANZANIA CIVIL AVIATION TRAINING CENTRE) mpaka leo Tunafundisha wataalamu kutoka nchi zote za kusini mwa Afrika,Kati,Mashariki mpaka Magaharibi ya Afrika katika mambo ya "Air Traffic Management,Aerodrome and Grounds Aid,Aviation Meteorology,Aeronautical Information Service and Aviation Security".....Tunafundisha watu wa Air Traffic Controllers kwa nchi nyingi za kimataifa..hii ni kazi ya JK Nyerere.

Tuwashukuru Wahandisi wetu kwa kurudisha DH-8 Q300,Welcome back ATCL "THE WING OF THE KILIMANJARO"....Now our Call Sign and Location Indicator will cross the winds and clouds of our beautiful Land......
Midege hii ndo haikawii kupolomoka
 
Natoa maoni katika point form
- Ma engineer wa ATCL waliobaki wako vizuri.Suala hapa lilikuwa ni hela za kununua vifaa vya kubadilisha (mwenye interest akasome zaid kuhusiana na Aircraft C check).Kwenye hangar ya Precision mtaona ndege kama tano hivi hazina injini .yote haya ni mambo ya C check na kukosa hela ya kuzigomboa toka huko Toulouse.
- TCAA wana utaratibu wa kusomesha waTanzania katika mambo ya aviation.Wamekuwa wakilifanya ingawa pia kuna suala la bajeti ya kuweza kufanya hivyo kwa WaTZ wengi zaidi
- Kupanga ni kuchagua.ATCL wamekodi bombadier CRJ 200 kwa utaratibu wa wet lease pale Dash 8 ilipoenda matengenezo.Ndege hizi zinalipiwa dola 450,000 kwa mwezi (USD 900,000/mo).Sioni sababu ya kukodi ndege hizi zenye limitation za ubebaji wa abiria kutokana na weight na distance na unaacha kukodi mfano Dash 8-Q300/200/100 nyingine zilizo sokoni ambazo ungetumika mtindo wa dry lease kwani una crew ambao wako rated ktk ndege hiyo.Crew wamekaa jobless mpaka wengine akiwemo Mkurugenzi wa uendeshaji wameenda Ghana Kuruka na wengine wanasoma vyuoni.Mwenye muda wa kuresearch aangalia kwa dola laki 9 utakodi Dash q 300 ngapi na utashangaa kwa jibu utakalopata
 
Aliyetuloga afufuliwe aje atusamehe ndio aende zake khaaaa. Kama mtu anakodi ndege moja kwa bei ambayo angeweza kupata ndege mbili au tatu ambazo zingeongeza kipato na idadi ya safari basi tuna shida na uwezo wa kuchambua mahesabu rahisi tunaweza magumu tuuuu
...
 
Inawezekana amewatazama kwa jich:( kali:rolleyes: wakamshitukia wameamua kuchukua hatua wenyewe maana si unajua maumivu ya kukamuliwa bila ganzi na hasa kama huo uvimbe upo sehemu mbaya!!

Natumaini ulichosema ndicho kinacho endelea.

Nchi yenye idadi ya watu milioni 46 . Haina
Shirika LA ndege ya kuaminika . Ni aibu Air Tanzania ni nembo ya Taifa.

Muheshimiwa Magufuli amsha ATCL. Watanzania
Tuwe nacha kujivunia.
 
Mkuu Mdudu Washasha
Kama waganga wasingekuwa wakiuliwa nilitaka kusema we n mganga mini umeona nachotaka kuandika.....

Kiuhalisia NA hali halisi kinachoua Atcl sio tu swala LA ndege NA utawala nalo ni tatizo...kama ulivyosema hapo juu hela tunayolipia ndeege ya Crj nikubwa sana kulinganisha NA Ku lease dash 8

Ndipo tunarudi pale kwenye 10%..inatumaliza kila kona ukiangalia hapo utakuta hizo hela kuna mlilongo mkubwa watu

Kingine kama ukuwa unajua like ndege linanyonya mafuta kama mchwa ...n hatari lakini kwakuwa kilakitu kinalipwa serikalin akunamwenye uchungu kamwe
 
hatuwezi sifia ujinga sifia peke yako haiwezekani kila siku tutumie kenya ethiopia south africa kwa vichwa vibovu kama tanzani hiyo haina maisha marefu watu walitaka kubiga washa piga
 
Ok inatakiwa kuwapongeza hao Mafundi kwa kuwa wazalendo..ila tukumbuke Ndege haiungwi ungwi sana kufail kwake inapokua angani ni madhara makubwa..ndege haina injini kwa muda wa zaidi ya miaka mitatu ipo tuu then tuje tuunge unge ndio ije ibebe abiria tena.tusifanye Masihara na vyombo vya Anga aisee..ikiwezekana zinunuliwe ndege zingine mbili kwa safari za ndani hao mafundi ni kuzicheki izo mpya pindi zinapokua na hitilafu kidogo lakini si kukarabati izo ambazo zipo garage kwa muda mrefu..
 
Hakuna cha kuwapongeza.....kwani siku zoote hizo ambazo ndege ilikuwa juu ya mawe walikuwa wapi yaani wameona kasi ya magufuli itawakumba wameona wajitete mapema...kwanini kipindi cha nyuma walikuwa wanapeleka ndege nje ya nchi kwaajili ya matengenezo
 
Back
Top Bottom