Jamani ugali iwe wa mahindi au wowote mwengine ni mtamu,lakini kwa kweli ugali wa mahindi ambao wengine huuita sembe au sima ni vyema kujizoesha kuwachana nao.Kabla kusikia hoja zangu nyinyi mwasemaje?.
masoud,hivi umewaza nini mpaka kutoa hii hoja? labda kidogo wahaya wanaweza wakakuelewa ila sio wasukuma,wakiacha ugali watakula nini kama chakula cha asili?
napata picha ya hii mada mada imetulia tusitegemee ugali pekee
Sasa wewe Masoud unachotaka kutuambia ni nini hasa? Mi naona unahangaika tu badala ya kutoa hoja ya kwa nini watu wasile ugali. Halafu unatushauri tule wali kama wewe! Sasa nini hii? Ulichotakiwa kutuambia labda ingekuwa ni kwamba tujifunze kuji-adapt na mazingira mageni pale tunapokuwa mbali na kwetu au pale tunapokuwe hatuwezi kupata vyakula tulivyovizoea. Na kwa hili sidhani kama kuna mtu ameshindwa. Lakini kusema categorically kabisa kwamba watu wasile ugali unashangaza sana Masoud.Kwa uzoefu nimegundua ya kuwa kile chakula mtu anachokula wakati wa utoto wake kuelekea ukubwa katika hali ya raha,yaani katika hali ya kupata na kuridhika kimazingira alipo ,hicho ndicho chakula atakachokiona ni kitamu kuliko vyote duniani.Hata ukimpeleka nchi gani basi bado atakitamani chakula hicho.
Watu huweza kuzoea vyakula kama viwili hivi kimoja zaidi na kingine chini yake.Wale waliozoea wali na kuku wataendelea hivyo mpaka uzeeni.Wa ndizi na muhogo nao ni hivyo hivyo,na kadhalika.Wazungu hakuna chakula bora kama viazi mbatata.Waarabu ni jamii ya mikate na nyama.
Wengi wetu katika Afrika tunapenda ugali hasa wa mahindi,wengine huita ugali wa sembe na majina mengineyo.Hata wakiwa maraisi na mawaziri wakifika ugenini huuweweseka ugali.
Ufanisi wa sera ya KILIMO KWANZA ni wa mashaka iwapo hatutobadili vipaumbele vya vyakula tunavyokula.Bahati mbaya sera hiyo katika nguzo yake ya 4 ya mpango wa utekelezaji, bado inataja mahindi ambayo hutoa ugali, kama zao la mwanzo katika mazao muhimu ya chakula.Mimi ndio wale wa wali kwa kuku kama chakula kikuu cha siku.Inapokuwa si wakati wa njaa na ukame, huna cha kuniambia mbele ya chakula hiki.Upishi wake huweza kutofautiana.Kwa bahati niko karibu na mafundi wa upishi wake.Ningependa watu wote wajizoeshe chakula changu cha wali,hata ikiwa ni kwa samaki.
Vyakula vyengine ninavyopendelea kula kwa ajili ya kifungua kinywa na chai ya usiku, ni jamii ya mikate na mboga mboga za majani zilizotiwa viungo mbali mbali.Nikijiweza zaidi ni supu ya mbuzi inayonukia viungo vya kiasili vya kiEshia.
Aagh achaneni na NGUNA (UGALI) nyieeeee. Ukiwa Morogoro songa Ugali halafu lumangia na kipande cha NGURUKA, mkuu waweza jng'ata. Ukiwa A-town (Arusha) vile vile pika UGALI wako halafu nunua wale samaki wanaokaangwa na akina mama kwenye magenge, wale samaki wanatoka bwawa la nyumba ya Mungu ni balaa tupu. Ukiwa Dar kula ugali na Kipande cha Papa, Kibua au changu wallahi utasahau km kuna kitu chaitwa NYAMA. Ukiwa Nyumbi hii bombi hii (SONGEA) kula Ugali na Dagaa nyasa au samaki wa ziwa nyasa wanaitwa Mbelele au MBASA mamaaaaaaaaaaaaaaaaa usisahau na lidelele (mlenda). Hahaha Ukiwa Sumbawanga kula Ugali kwa NSWA (kumbikumbi) hahahaha mambo hayoo wadau UGALI MTAMU BANA, uwe sembe au dona whatever MAN!!!!!!!!!!!.
nyinyi wanafalsafa mnaongelea ugali au kuna kitu kipo ndani ya ugali
Kwa kufupisha hii mada ili imalizike kwa vile wasioelewa wameanza kuchoka;ni kuwa vyakula wanavyokula wachina,wahindi na wengine wasiokumbwa na njaa mara kwa mara baadhi huoteshwa kwenye vieneo vidogo hata kwenye hali ngumu ya hali ya hewa,na kutoa mazao mengi. Jambo hili kwa mahindi ni nadra kutokea.Mazao mengine huota kwenye vivuli vya miti na kwa kutambaa miti wenzao ambayo nayo hutoa mazao yake yenyewe.ugali,mchele blaah blaaah blaaaaaaaaaaaaaaaaaah blaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah,mpaka njaa inauma,ngoja nikale kiporo changu cha ugali mie.
Nakiri tumeishiwa thread za kuanzisha
Wanao haribu ladha ya JAMII FORUMS ni wana forum wenyewe.
Kisha tukiambiwa kuwa JF imevamiwa tunakuwa wakali.