Stroke
JF-Expert Member
- Feb 17, 2012
- 38,560
- 48,906
Wakosoaji na wachambuzi wa maswala ya kisiasa wanatuhumu kwamba Baraza la Mawaziri lililotangazwa na Ndugu Rais lina mkono wa Chama na si mapendekezo yake.
Usahihi ama makosa ya hiyo kauli yanafahamika na Ndugu Rais mwenyewe na waliohusika katika mchakato mzima wa upatikanaji wa baraza lenyewe.
Tunachokiona tu wengine ni kushukuru kwa upatikanaji wake ambao utampunguzia mzigo mzito ndugu Rais wa kukimbia huku na kule.
Ila ukijaribu kuangalia kwa upande mwingine, utaona kwamba, Ndugu Rais anajiondoa na lawama za manazi na wakongwe katika chama kwa kutoa nafasi kwa walioteuliwa ili juhudi na uchapakazi wao ndio ziwahukumu wao na si iwe yeye aliyewahukumu kabla ya kupata nafasi.
Ni utendaji kazi pekee ndio utawabakiza au utawaondoa, katika nafasi zilizopo. Ingawa nia ya dhati kabisa ya kuja na sura mpya katika duru za siasa za nchi hii inaonekana, na hili litatimizwa.
Katika kipindi cha miaka miwili toka sasa, tarajia kuona sura mpya kabisa katika baraza na zilizojaa wachapakazi ambao watalipeleka Taifa hili katika hatua nyingine kabisa.
Sina haja ya kusema kwamba uteuzi ulikua wa fadhila kwa chama, hapana, bali ni hatua ya kwanza muhimu ya kuelekea kule Ndugu Rais anapopataka.
Nasubiri tukijaliwa, kuona hili baada ya miaka miwili.
Usahihi ama makosa ya hiyo kauli yanafahamika na Ndugu Rais mwenyewe na waliohusika katika mchakato mzima wa upatikanaji wa baraza lenyewe.
Tunachokiona tu wengine ni kushukuru kwa upatikanaji wake ambao utampunguzia mzigo mzito ndugu Rais wa kukimbia huku na kule.
Ila ukijaribu kuangalia kwa upande mwingine, utaona kwamba, Ndugu Rais anajiondoa na lawama za manazi na wakongwe katika chama kwa kutoa nafasi kwa walioteuliwa ili juhudi na uchapakazi wao ndio ziwahukumu wao na si iwe yeye aliyewahukumu kabla ya kupata nafasi.
Ni utendaji kazi pekee ndio utawabakiza au utawaondoa, katika nafasi zilizopo. Ingawa nia ya dhati kabisa ya kuja na sura mpya katika duru za siasa za nchi hii inaonekana, na hili litatimizwa.
Katika kipindi cha miaka miwili toka sasa, tarajia kuona sura mpya kabisa katika baraza na zilizojaa wachapakazi ambao watalipeleka Taifa hili katika hatua nyingine kabisa.
Sina haja ya kusema kwamba uteuzi ulikua wa fadhila kwa chama, hapana, bali ni hatua ya kwanza muhimu ya kuelekea kule Ndugu Rais anapopataka.
Nasubiri tukijaliwa, kuona hili baada ya miaka miwili.