talentbrain
JF-Expert Member
- Oct 5, 2009
- 1,187
- 760
Habari za weekend wadau wote na wazalendo wote wa nchi hii. Niwatakie weekend jema.
Nikiwa nimetulia leo nyumbani, nimepitia thread tofauti hapa na kuguswa na jinsi Mungu alivyoijalia nchi yetu na vivutio lukuki tena zaidi ya viwili kwa kila mkoa.
Bahati mbaya ni kwamba si kuwa havifahamiki nje ya nchi tu bali hata kwa watanzania. Baada ya kuguswa na hali hii, na kubaini fursa ya kiuchumi inayoweza kupatikana kwa nchi yetu kama tutavitangaza vivutio vyetu kimataifa nikaona nije na hoja kadhaa na wadau mtaongeza kwa kadri mtavyoona inafaa.
1. Tutumie thread hii kuotodhesha na ni vema tukaweka picha na maelezo ya kujitosheleza kwa vivutio vyetu.
2. Watanzania na hasa wazalendo tukajiunga na forums za kimataifa na kuaza kuvitangaza vivutio tutavyoviorodhesha hapa. Mfano. Wakijitokeza watu 20 wakajiunga na forums kubwa ulimwenguni na kupost post mbili kila siku ni wazi tutafikia malengo.
3. Tuelekezane links za vivutio vyetu na kama hakuna website nzuri za utalii ni fursa sasa kwa wenye interest kwa biashara hii kuzianzisha na watafaidika sana kwakuwa industry hii inakuwa kwa speed sana.
Niwaombe wadau tuchangie mawazo na hata kuweka vivutio hapa na pia mwenye link ya forums au website za kimataifa zenye kuruhusu comments waziweke hapa. Nimepitia website nyingi na kubaini jinsi wenzetu Kenya na Nigeria walivyo aggressive kwenye kuitangaza nchi yao.
Ni muda sasa tuitangaze nchi yetu popote bila aibu. Tukumbuke kuwa neema tunayoitaka tutaipata kama serikali na wananchi watapata kipato.
Wasallam. Weekend njema.
Nikiwa nimetulia leo nyumbani, nimepitia thread tofauti hapa na kuguswa na jinsi Mungu alivyoijalia nchi yetu na vivutio lukuki tena zaidi ya viwili kwa kila mkoa.
Bahati mbaya ni kwamba si kuwa havifahamiki nje ya nchi tu bali hata kwa watanzania. Baada ya kuguswa na hali hii, na kubaini fursa ya kiuchumi inayoweza kupatikana kwa nchi yetu kama tutavitangaza vivutio vyetu kimataifa nikaona nije na hoja kadhaa na wadau mtaongeza kwa kadri mtavyoona inafaa.
1. Tutumie thread hii kuotodhesha na ni vema tukaweka picha na maelezo ya kujitosheleza kwa vivutio vyetu.
2. Watanzania na hasa wazalendo tukajiunga na forums za kimataifa na kuaza kuvitangaza vivutio tutavyoviorodhesha hapa. Mfano. Wakijitokeza watu 20 wakajiunga na forums kubwa ulimwenguni na kupost post mbili kila siku ni wazi tutafikia malengo.
3. Tuelekezane links za vivutio vyetu na kama hakuna website nzuri za utalii ni fursa sasa kwa wenye interest kwa biashara hii kuzianzisha na watafaidika sana kwakuwa industry hii inakuwa kwa speed sana.
Niwaombe wadau tuchangie mawazo na hata kuweka vivutio hapa na pia mwenye link ya forums au website za kimataifa zenye kuruhusu comments waziweke hapa. Nimepitia website nyingi na kubaini jinsi wenzetu Kenya na Nigeria walivyo aggressive kwenye kuitangaza nchi yao.
Ni muda sasa tuitangaze nchi yetu popote bila aibu. Tukumbuke kuwa neema tunayoitaka tutaipata kama serikali na wananchi watapata kipato.
Wasallam. Weekend njema.