mkwapuaji
Member
- Jan 6, 2012
- 49
- 20
Tanzania tuseme yatosha kuburuzwa na Kenya kwa mazao ya kilimo. Tuifanye Tanzania iwe Tanzania kwa sasa.
Hivi tumeacha biashara yetu ikatawaliwa na Kenya kwa makusudi au ni bahati mbaya, hasa ya kupeleka mazao ya kilimo nje ya nchi na bara la Afrika.
Bei za mazao yetu ya kilimo zinapagwa na wakenya huko Kenya na ikiwa hawatakuja kuychukua basi bei hudorora mfano Mbaazi, Mahindi n.k Ukienda Mang'ola kwenye vitunguu ni gari za Kenya utazikuta mpaka unaweza kufikiri upo Kenya yaani mpaka huwa najiuliza tumeiacha nchi yetu holela namna hii...
Kuna haja ya kuchukua hatua za haraka kulizuia hili kwani kila siku mkulima wa Tanzania ataendelea kugandamizwa na mawakala na madalali wa kutokea Kenya
1/ Yafaa sasa tuweke kodi kwenye mazao yetu na bidhaa zetu ziendazo Kenya na nchi jirani. Hii imekuwa ikiwarahisishia wanunuzi wa nje kuja kuchukua mazao kwani yamekuwa yakipatikana kwa bei rahisi na hata wakiyafikisha kwao gharama bado inakuwa ndogo na hivyo kuyauza kwa bei sawa na mazao yao.
2/ Kuanzisha mfumo wa udhibiti holela wa uuzaji mazao kwa wakulima. Nadhani kunapaswa kuwa na chombo kinachowasaidia wakulima wetu kuuza na kupanga bei za mazao yao. Hii itasaidia kuzuia wachuuzi hasa wa nje kwenda moja kwa moja mashambani kumlaghai mkulima.
3/ Kutanua wigo wa masoko kwa mazao ya kilimo ya Tanzania nje ya mipaka yetu. Tumekuwa na utegemezi wa soko moja hasa Kenya kwa mazao yetu. Sasa ni wakati tunapaswa kuwaza nje kabisa ya Afrika Mashariki kibiashara. Kahawa ya Tanzania ipelekwe USA, UK, SAUD ARABIA, GERMANY.... na watanzania sio wakenya. Kahawa ya Tanzania ipewe mlinganyo sahihi na bidhaa za nchi nyingine sio kama bidhaa ya Kenya. Mbaazi za Tanzania zipelekwe India na makampuni ya Tanzania sio kama sasa wanavyoamini kuwa ni bidhaa ya Kenya
4/ ATCL ianzishe ndege za mizigo. Hapa ndio pia wenzetu walipotuacha. Makampuni makubwa ya ndege za mizigo yanatua katika viwanja vya Kenya. Hii imesababisha karibia kila bidhaa muhimu kwa wenzetu basi kuna haja ya kuipeleka Kenya ili iweze kupelekwa nje ya bara Afrika kwa haraka. Rai yangu kwa Mheshimiwa rais afikirie pia kununua ndege za mizigo ili hata kama makampuni ya wenzetu hayapendi kutua kwetu basi tubebe vyetu wenyewe na kuvipeleka.
5/ Watanzania tuache fikra mgando ya kuona kuwa nchi za wenzetu hatuaminiki kama wakenya. Wafanyabiashara wa Tanzania pia wao ndio wamekuwa chanzo cha kuifanya Kenya kutufanyia kila kitu. Leo pesa nyingi za kigeni huingia Kenya kwa bidhaa zinazoenda nje ya nchi hiyo japo zimetoka Tanzania. Uchumi wa nchi yetu umekuwa ukidorora kila wakati huku wanaouua ni watanzania mwenyewe na sio setikali yao kama wanavyodhani.
Ifike wakati Taifa la Tanzania Liishi, liwaze, na liamue kama TANZANIA
Hivi tumeacha biashara yetu ikatawaliwa na Kenya kwa makusudi au ni bahati mbaya, hasa ya kupeleka mazao ya kilimo nje ya nchi na bara la Afrika.
Bei za mazao yetu ya kilimo zinapagwa na wakenya huko Kenya na ikiwa hawatakuja kuychukua basi bei hudorora mfano Mbaazi, Mahindi n.k Ukienda Mang'ola kwenye vitunguu ni gari za Kenya utazikuta mpaka unaweza kufikiri upo Kenya yaani mpaka huwa najiuliza tumeiacha nchi yetu holela namna hii...
Kuna haja ya kuchukua hatua za haraka kulizuia hili kwani kila siku mkulima wa Tanzania ataendelea kugandamizwa na mawakala na madalali wa kutokea Kenya
1/ Yafaa sasa tuweke kodi kwenye mazao yetu na bidhaa zetu ziendazo Kenya na nchi jirani. Hii imekuwa ikiwarahisishia wanunuzi wa nje kuja kuchukua mazao kwani yamekuwa yakipatikana kwa bei rahisi na hata wakiyafikisha kwao gharama bado inakuwa ndogo na hivyo kuyauza kwa bei sawa na mazao yao.
2/ Kuanzisha mfumo wa udhibiti holela wa uuzaji mazao kwa wakulima. Nadhani kunapaswa kuwa na chombo kinachowasaidia wakulima wetu kuuza na kupanga bei za mazao yao. Hii itasaidia kuzuia wachuuzi hasa wa nje kwenda moja kwa moja mashambani kumlaghai mkulima.
3/ Kutanua wigo wa masoko kwa mazao ya kilimo ya Tanzania nje ya mipaka yetu. Tumekuwa na utegemezi wa soko moja hasa Kenya kwa mazao yetu. Sasa ni wakati tunapaswa kuwaza nje kabisa ya Afrika Mashariki kibiashara. Kahawa ya Tanzania ipelekwe USA, UK, SAUD ARABIA, GERMANY.... na watanzania sio wakenya. Kahawa ya Tanzania ipewe mlinganyo sahihi na bidhaa za nchi nyingine sio kama bidhaa ya Kenya. Mbaazi za Tanzania zipelekwe India na makampuni ya Tanzania sio kama sasa wanavyoamini kuwa ni bidhaa ya Kenya
4/ ATCL ianzishe ndege za mizigo. Hapa ndio pia wenzetu walipotuacha. Makampuni makubwa ya ndege za mizigo yanatua katika viwanja vya Kenya. Hii imesababisha karibia kila bidhaa muhimu kwa wenzetu basi kuna haja ya kuipeleka Kenya ili iweze kupelekwa nje ya bara Afrika kwa haraka. Rai yangu kwa Mheshimiwa rais afikirie pia kununua ndege za mizigo ili hata kama makampuni ya wenzetu hayapendi kutua kwetu basi tubebe vyetu wenyewe na kuvipeleka.
5/ Watanzania tuache fikra mgando ya kuona kuwa nchi za wenzetu hatuaminiki kama wakenya. Wafanyabiashara wa Tanzania pia wao ndio wamekuwa chanzo cha kuifanya Kenya kutufanyia kila kitu. Leo pesa nyingi za kigeni huingia Kenya kwa bidhaa zinazoenda nje ya nchi hiyo japo zimetoka Tanzania. Uchumi wa nchi yetu umekuwa ukidorora kila wakati huku wanaouua ni watanzania mwenyewe na sio setikali yao kama wanavyodhani.
Ifike wakati Taifa la Tanzania Liishi, liwaze, na liamue kama TANZANIA