Mkulima na Mfugaji
JF-Expert Member
- Jul 26, 2013
- 1,013
- 1,634
Mimi nakupa uzoefu wangu wa field,
Robo tatu ya ekari ni eneo kubwa sana kwa kilimo cha papai, kama atakuwa serious na akapoteza muda wake mwingi na nguvu zake huwenda asitamani tena ajira ya mtu.
Habari wakulima na wafugaji wenzangu, kumekuwa na malalamiko mwengi siku hizi kwa wakulima wanaotaka kuwekeza kwenye kilimo cha papai kwamba wanakutana na mipapai dume mingi pindi wanaponunua miche ya mipapai kutoka kwa wazalishaji wa vitalu ya miche hiyo.
Siku hizi watu wamekuwa sio waaminifu, mtu anaweza kununua papai sokoni bila kujua aina ya mbegu akaja akaotesha miche kisha akaipachika jina lolote analojua yeye halafu akauzia watu, papai likishachakachuliwa mara nyingi lazima lipungue ubora na pia lazima upate mipapai dume mingi hata 50 kwa 50 kwani mbegu hybrid lazima ipatikane mbegu yenye sifa ya kike na ya kiume kwa hiyo kama itachakachuliwa sana inarudi kwenye sifa zake za awali.
NINI CHA KUFANYA?
Kama unataka kuwekeza kwenye kilimo cha papai na uwezo wako ni mdogo, nenda kwenye duka la pembejeo linaloeleweka nunua mbegu chotara inayojulikana hata ya Tsh 15,000 kisha otesha miche yako mwenyewe uitunze kwa uangalifu, ikishaanza kuzaa hapo unaweza kuchagua mipapai bora ukaotesha kitalu chako unachohitaji na idadi ya miche yoyote unayotaka. Hapo miche yako itakuwa ni bora kwani huo ni uzazi wa kwanza hivyo inakuwa haijapoteza ubora wake kwa kiasi kikubwa.
JINSI YA KUPANDA MICHE YA PAPAI SHAMBANI
Chimba shimo la Futi mbili upana na Futi mbili urefu
Weka mbolea yako ya samadi angalau ndoo ndogo mbili kila shimo
panda mche wako wa papai
Kama eneo lako halina maji ya kutosha panda miche yako wakati wa masika
MAKADILIO YA MAPATO
Robo Tatu ya ekari inaingia miche 750 kama shamba limepandwa Kitaalamu ila kwa mashamba yetu ya uswahilini kadilia miche 500
Chukulia mche mmoja umezaa papai 20 ingawa Kitaalamu ni miche 40
20 *500 =10000
Chukulia umeuza papai moja Tsh 300 hapo hapo shambani
10000 *300 =3000000
Kumbuka huo ni kwa uzao mmoja na tumeweka papai 20
Kumbuka kwa Mwaka inaweza kuzaa hata mara 3
Huu utaalam ni wa field mimi mwenyewe ndio nimeanza kilimo hiki
Sent using Jamii Forums mobile app
Robo tatu ya ekari ni eneo kubwa sana kwa kilimo cha papai, kama atakuwa serious na akapoteza muda wake mwingi na nguvu zake huwenda asitamani tena ajira ya mtu.
Habari wakulima na wafugaji wenzangu, kumekuwa na malalamiko mwengi siku hizi kwa wakulima wanaotaka kuwekeza kwenye kilimo cha papai kwamba wanakutana na mipapai dume mingi pindi wanaponunua miche ya mipapai kutoka kwa wazalishaji wa vitalu ya miche hiyo.
Siku hizi watu wamekuwa sio waaminifu, mtu anaweza kununua papai sokoni bila kujua aina ya mbegu akaja akaotesha miche kisha akaipachika jina lolote analojua yeye halafu akauzia watu, papai likishachakachuliwa mara nyingi lazima lipungue ubora na pia lazima upate mipapai dume mingi hata 50 kwa 50 kwani mbegu hybrid lazima ipatikane mbegu yenye sifa ya kike na ya kiume kwa hiyo kama itachakachuliwa sana inarudi kwenye sifa zake za awali.
NINI CHA KUFANYA?
Kama unataka kuwekeza kwenye kilimo cha papai na uwezo wako ni mdogo, nenda kwenye duka la pembejeo linaloeleweka nunua mbegu chotara inayojulikana hata ya Tsh 15,000 kisha otesha miche yako mwenyewe uitunze kwa uangalifu, ikishaanza kuzaa hapo unaweza kuchagua mipapai bora ukaotesha kitalu chako unachohitaji na idadi ya miche yoyote unayotaka. Hapo miche yako itakuwa ni bora kwani huo ni uzazi wa kwanza hivyo inakuwa haijapoteza ubora wake kwa kiasi kikubwa.
JINSI YA KUPANDA MICHE YA PAPAI SHAMBANI
Chimba shimo la Futi mbili upana na Futi mbili urefu
Weka mbolea yako ya samadi angalau ndoo ndogo mbili kila shimo
panda mche wako wa papai
Kama eneo lako halina maji ya kutosha panda miche yako wakati wa masika
MAKADILIO YA MAPATO
Robo Tatu ya ekari inaingia miche 750 kama shamba limepandwa Kitaalamu ila kwa mashamba yetu ya uswahilini kadilia miche 500
Chukulia mche mmoja umezaa papai 20 ingawa Kitaalamu ni miche 40
20 *500 =10000
Chukulia umeuza papai moja Tsh 300 hapo hapo shambani
10000 *300 =3000000
Kumbuka huo ni kwa uzao mmoja na tumeweka papai 20
Kumbuka kwa Mwaka inaweza kuzaa hata mara 3
Huu utaalam ni wa field mimi mwenyewe ndio nimeanza kilimo hiki
Sent using Jamii Forums mobile app