Tusaidiane kuhusu kilimo cha bustani ya mipapai

Mkulima na Mfugaji

JF-Expert Member
Jul 26, 2013
1,013
1,634
Mimi nakupa uzoefu wangu wa field,

Robo tatu ya ekari ni eneo kubwa sana kwa kilimo cha papai, kama atakuwa serious na akapoteza muda wake mwingi na nguvu zake huwenda asitamani tena ajira ya mtu.

Habari wakulima na wafugaji wenzangu, kumekuwa na malalamiko mwengi siku hizi kwa wakulima wanaotaka kuwekeza kwenye kilimo cha papai kwamba wanakutana na mipapai dume mingi pindi wanaponunua miche ya mipapai kutoka kwa wazalishaji wa vitalu ya miche hiyo.

Siku hizi watu wamekuwa sio waaminifu, mtu anaweza kununua papai sokoni bila kujua aina ya mbegu akaja akaotesha miche kisha akaipachika jina lolote analojua yeye halafu akauzia watu, papai likishachakachuliwa mara nyingi lazima lipungue ubora na pia lazima upate mipapai dume mingi hata 50 kwa 50 kwani mbegu hybrid lazima ipatikane mbegu yenye sifa ya kike na ya kiume kwa hiyo kama itachakachuliwa sana inarudi kwenye sifa zake za awali.

NINI CHA KUFANYA?
Kama unataka kuwekeza kwenye kilimo cha papai na uwezo wako ni mdogo, nenda kwenye duka la pembejeo linaloeleweka nunua mbegu chotara inayojulikana hata ya Tsh 15,000 kisha otesha miche yako mwenyewe uitunze kwa uangalifu, ikishaanza kuzaa hapo unaweza kuchagua mipapai bora ukaotesha kitalu chako unachohitaji na idadi ya miche yoyote unayotaka. Hapo miche yako itakuwa ni bora kwani huo ni uzazi wa kwanza hivyo inakuwa haijapoteza ubora wake kwa kiasi kikubwa.

JINSI YA KUPANDA MICHE YA PAPAI SHAMBANI

Chimba shimo la Futi mbili upana na Futi mbili urefu

Weka mbolea yako ya samadi angalau ndoo ndogo mbili kila shimo

panda mche wako wa papai

Kama eneo lako halina maji ya kutosha panda miche yako wakati wa masika

MAKADILIO YA MAPATO

Robo Tatu ya ekari inaingia miche 750 kama shamba limepandwa Kitaalamu ila kwa mashamba yetu ya uswahilini kadilia miche 500

Chukulia mche mmoja umezaa papai 20 ingawa Kitaalamu ni miche 40

20 *500 =10000

Chukulia umeuza papai moja Tsh 300 hapo hapo shambani

10000 *300 =3000000

Kumbuka huo ni kwa uzao mmoja na tumeweka papai 20

Kumbuka kwa Mwaka inaweza kuzaa hata mara 3

Huu utaalam ni wa field mimi mwenyewe ndio nimeanza kilimo hiki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nakupa uzoefu wangu wa field,

Robo tatu ya ekari ni eneo kubwa sana kwa kilimo cha papai, kama atakuwa serious na akapoteza muda wake mwingi na nguvu zake huwenda asitamani tena ajira ya mtu.

Habari wakulima na wafugaji wenzangu, kumekuwa na malalamiko mwengi siku hizi kwa wakulima wanaotaka kuwekeza kwenye kilimo cha papai kwamba wanakutana na mipapai dume mingi pindi wanaponunua miche ya mipapai kutoka kwa wazalishaji wa vitalu ya miche hiyo.

Siku hizi watu wamekuwa sio waaminifu, mtu anaweza kununua papai sokoni bila kujua aina ya mbegu akaja akaotesha miche kisha akaipachika jina lolote analojua yeye halafu akauzia watu, papai likishachakachuliwa mara nyingi lazima lipungue ubora na pia lazima upate mipapai dume mingi hata 50 kwa 50 kwani mbegu hybrid lazima ipatikane mbegu yenye sifa ya kike na ya kiume kwa hiyo kama itachakachuliwa sana inarudi kwenye sifa zake za awali.

NINI CHA KUFANYA?
Kama unataka kuwekeza kwenye kilimo cha papai na uwezo wako ni mdogo, nenda kwenye duka la pembejeo linaloeleweka nunua mbegu chotara inayojulikana hata ya Tsh 15,000 kisha otesha miche yako mwenyewe uitunze kwa uangalifu, ikishaanza kuzaa hapo unaweza kuchagua mipapai bora ukaotesha kitalu chako unachohitaji na idadi ya miche yoyote unayotaka. Hapo miche yako itakuwa ni bora kwani huo ni uzazi wa kwanza hivyo inakuwa haijapoteza ubora wake kwa kiasi kikubwa.

JINSI YA KUPANDA MICHE YA PAPAI SHAMBANI

Chimba shimo la Futi mbili upana na Futi mbili urefu

Weka mbolea yako ya samadi angalau ndoo ndogo mbili kila shimo

panda mche wako wa papai

Kama eneo lako halina maji ya kutosha panda miche yako wakati wa masika

MAKADILIO YA MAPATO

Robo Tatu ya ekari inaingia miche 750 kama shamba limepandwa Kitaalamu ila kwa mashamba yetu ya uswahilini kadilia miche 500

Chukulia mche mmoja umezaa papai 20 ingawa Kitaalamu ni miche 40

20 *500 =10000

Chukulia umeuza papai moja Tsh 300 hapo hapo shambani

10000 *300 =3000000

Kumbuka huo ni kwa uzao mmoja na tumeweka papai 20

Kumbuka kwa Mwaka inaweza kuzaa hata mara 3

Huu utaalam ni wa field mimi mwenyewe ndio nimeanza kilimo hiki

Sent using Jamii Forums mobile app
Wastani wa umbali kati ya mche na mche au sio muhimu?
 
Robo tatu ya heka inaingia miche 750? umbali toka mche hadi mche ni upi? Pia umetuchanganya unaposema Bustani ya mipapai? fafanua kwa nini Bustani na siyo Shamba.?
 
Maisha hayapo simple hivyo

Kilimo hakipo simple hivyo

Kama ni hivyo watu wangeshakuwa mabilionea na wangelima sana papai

Umeweka Assumptions bila Challenges ambazo ni nyingi na critical

Kwa mfano tatizo kubwa sana ni SOKO na MAGONJWA

Tuulize wakulima tukuambie...utajaza mapapai hata vyumba vitatu yaoze tu

Na sasahivi tena na Corona hata Kenya tu hupeleki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom