Tundu Lissu chagua moja, siasa au urais wa TLS unatuchanganya

gstar

JF-Expert Member
Jun 19, 2011
790
1,372
Mheshimiwa Tundu Lissu salaam sana ama baada ya salamu. Mimi ni shabiki wako namba moja pia ni mwanachama wa chama chetu pendwa cha CHADEMA.

Nakuandikia barua hii nikiomba upokee ushauri wangu kwamba ama ujiuzulu nafasi yako ya ubunge wa kuchaguliwa na wananchi na ubaki kuwa huru au ujitoe katika kinyang'anyiro cha uraisi wa TLS.

Mheshimiwa Lissu, ulichaguliwa na wananchi wa Singida Mashariki ili uweze kuwatumikia kwa moyo wako wote na kwa nguvu zako zote lakini badala yake hao umewasahau kabisa na sasa umeamua kujiingiza kwenye mambo mengine yanayo kupotezea muda na kukufanya usahau wananchi wako walio kuchagua.

Je, mheshimiwa unaweza kueleza ni kwa namna gani unaweza kujigawa kufanya kazi kwa pandezote tatu yaani Ubunge wa singida mashariki, uwanasheria wa chadema na mwisho uraisi wa TLS? Bila shaka ni lazima kuna nafasi moja hutoitendea haki kwa maana huwezi kuwa na muda wa kutosha kutekeleza yote haya.

Mheshimiwa Lissu, Pamoja na ushauri wote uliopewa na viongozi wakubwa wa nchi akiwemo Dokta Harisson Mwakyembe kwamba ili kuepusha chama cha sheria kuonekana kuwa kinavamiwa nawanasiasa ni vyema wewe ukajiepusha kujihusisha nacho lakini wewe uliendelea kukaidi na kuhisi kwamba unaonewa!

Mheshimiwa nilidhani kwamba ungejipima tu kuwa hufiti katika nafasi hiyo kwasababu tayari wewe unamaslahi na mrengo fulani wa siasa kwa hilo tu linakuondolea sifa. Ni vyema sasa ukajipima na kuamua kukaa pembeni kwa kuwa hata kama ukishinda kuwa kiongozi mkuu wa TLS bado maamuzi yoyote utakayo yatoa yatakuwa na vikwazo vingi pia yatahusishwa na mrengo wako wa kisiasa.

Mwisho kabisa naomba nikuombe mheshimiwa ujipime tena katika hilo na pia naomba utambue thamani kubwa na heshima ambayo wanachi wako wa Singida Mashariki wamekupa kuwa mwakilishi wao Bungeni. Watumikie wao kwa nguvu zako zote maana wakichukia mwaka 2020 watakupiga chini.

Wako mwaminifu

Gstar
 
Mheshimiwa Tundu Lissu salaam sana ama baada ya salamu. Mimi ni shabiki wako namba moja pia ni mwanachama wa chama chetu pendwa cha CHADEMA.

Nakuandikia barua hii nikiomba upokee ushauri wangu kwamba ama ujiuzulu nafasi yako ya ubunge wa kuchaguliwa na wananchi na ubaki kuwa huru au ujitoe katika kinyang'anyiro cha uraisi wa TLS.

Mheshimiwa Lissu, ulichaguliwa na wananchi wa Singida Mashariki ili uweze kuwatumikia kwa moyo wako wote na kwa nguvu zako zote lakini badala yake hao umewasahau kabisa na sasa umeamua kujiingiza kwenye mambo mengine yanayo kupotezea muda na kukufanya usahau wananchi wako walio kuchagua.

Je, mheshimiwa unaweza kueleza ni kwa namna gani unaweza kujigawa kufanya kazi kwa pandezote tatu yaani Ubunge wa singida mashariki, uwanasheria wa chadema na mwisho uraisi wa TLS? Bila shaka ni lazima kuna nafasi moja hutoitendea haki kwa maana huwezi kuwa na muda wa kutosha kutekeleza yote haya.

Mheshimiwa Lissu, Pamoja na ushauri wote uliopewa na viongozi wakubwa wa nchi akiwemo Dokta Harisson Mwakyembe kwamba ili kuepusha chama cha sheria kuonekana kuwa kinavamiwa nawanasiasa ni vyema wewe ukajiepusha kujihusisha nacho lakini wewe uliendelea kukaidi na kuhisi kwamba unaonewa!

Mheshimiwa nilidhani kwamba ungejipima tu kuwa hufiti katika nafasi hiyo kwasababu tayari wewe unamaslahi na mrengo fulani wa siasa kwa hilo tu linakuondolea sifa. Ni vyema sasa ukajipima na kuamua kukaa pembeni kwa kuwa hata kama ukishinda kuwa kiongozi mkuu wa TLS bado maamuzi yoyote utakayo yatoa yatakuwa na vikwazo vingi pia yatahusishwa na mrengo wako wa kisiasa.

Mwisho kabisa naomba nikuombe mheshimiwa ujipime tena katika hilo na pia naomba utambue thamani kubwa na heshima ambayo wanachi wako wa Singida Mashariki wamekupa kuwa mwakilishi wao Bungeni. Watumikie wao kwa nguvu zako zote maana wakichukia mwaka 2020 watakupiga chini.

Wako mwaminifu

Gstar
Tunahitaji strong TLS,mwache agombee anayohaki kama mwanachama wa TLS,na hagombei sabbau ni mwanachama wa CDM bali sababu anayo haki na ni mwanachama hai wa TLS.

Kama kweli wewe ni CDM basi ungeisupport move ya TL.Kama Taifa tunahitajila strong TLS na si TLS tawi la CCM
 
Watu mna 'mahaba niue' hata viongozi wenu wakikosea mnaona sawa tu
 
Unamshauri ajiuzulu ubunge kwa kuwa unajua kuwa nafasi itakuwa wazi ili mumuweke mgombea wenu na hujamshauri kujiuzulu uwanasheria Mkuu wa CHADEMA kwa kuwa unajua kuwa hamuwezi kumuweka mgombea wenu.
 
ila kweli...TLS ..inaingia kwenye siasa jambo ambalo ni hatari kwa masuala ya kusimamia sheria maana itaendeshwa kimlengo wa upande fulani wa kisiasa....tofati na awali...

NAUNGA MKONO HOJA...
Lissu achague moja....

(povu)...
 
Back
Top Bottom