Tundu Lissu achangiwa milioni 17 ndani ya masaa 24

ChekoFagia

Senior Member
Joined
Sep 20, 2025
Posts
115
Reaction score
339
Kampeni iliyoanzishwa na wanachama na wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na na Maendeleo (CHADEMA) ya kumchangia Mwenyekiti wa Chama hicho Tundu Lissu ambaye amekuwa kizuizini kwa zaidi ya siku 250 imeendelea kushika kasi na zaidi ya shilingi million 17 imechangwa ndani kwa siku Moja.

Kampeni hiyo iliyopewa jina la "Funga Mwaka na Tundu Lissu" ilianzishwa kwa lengo la kuchangisha fedha takribani shilingi milioni 20 ndani ya masaa 48.

Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa na waanzilishi wa kampeni hiyo akiwemo Edson Mwakalebela(Sativa) na Godilisten Malisa wamthibitisha kupatikana kwa kiasi hicho cha fedha ambazo zimekuwa zikiwekwa katika akaunti za kaka wa Lissu Alute Mughwai Lissu.

Waendeshaji wa michango hiyo wameeleza fedha hizo ni ili kuinysha upendo na kumuunga mkono Lissu lakini pia kuiwezesha familia na wale waoweza kumfikia Lissu gerezani wasikwame kokote katika kumhudumia Lissu.

Godilisten Malisa ameandika “Jana GenZ walipotuambia wanataka kumchangia Lissu 20M kwa masaa 48 tuliona kama wanafanya mzaha. Lakini tukawakubalia. Tukasema hata isipotimia ndani ya masaa 48 basi tutaongeza muda. Tukaongea na mzee Alute (kaka yake Lissu) ili akubali ombi la GenZ apokee michango. Sasa hata masaa 24 hayajaisha tayari mzigo ushasoma 17M. Aisee nimewavulia kofi”.

 
..Mama Abduli alikusanya matajiri wakamchangia BILLION 100 ndani ya masaa manne.
 
Ala bure mahabusu,pesa za nini?..watu waliwa
 
..Mama Abduli alikusanya matajiri wakamchangia BILLION 100 ndani ya masaa manne.
Sasa utamfananishaje The Mother of Modern Tanzania na hako kachiba kaongo, kazushi na kenye chuki na watu waliomzidi?!!!
 
Sasa utamfananishaje The Mother of Modern Tanzania na hako kachiba kaongo, kazushi na kenye chuki na watu waliomzidi?!!!

..huwezi kuwalinganisha Mama Abduli na Baba Agustino.

..mmoja ni akili kubwa mwanazuoni, muandishi, mwalimu, mwingine hata kusoma alichoandikiwa ni mtihani mkubwa.
 
..huwezi kuwalinganisha Mama Abduli na Baba Agustino.

..mmoja ni akili kubwa mwanazuoni, muandishi, mwalimu, mwingine hata kusoma alichoandikiwa ni mtihani mkubwa.
Endeleeni kujifariji haters. Nyie endeleeni kumpigia makofi yule lofa anayeenda mahakamani na gunia lililojaa vitabu kama bwege
 
Mpaka imefikia hela hiyo waliotuma itakua ni wengi sana maana waliotuma wengi maskini wapo waliotuma hadi 100 wengine 200
 
Endeleeni kujifariji haters. Nyie endeleeni kumpigia makofi yule lofa anayeenda mahakamani na gunia lililojaa vitabu kama bwege

..haters ni wale wanaotaka kumfunga TL bila hatia yoyote.

..wana vyeo vikubwa, mali zisizo na hesabu, lakini bado wanajiona wamepungukiwa mbele ya TL, na ndio sababu ya kumtesa.
 
..haters ni wale wanaotaka kumfunga TL bila hatia yoyote.

..wana vyeo vikubwa, mali zisizo na hesabu, lakini bado wanajiona wamepungukiwa mbele ya TL, na ndio sababu ya kumtesa.
Inamtesa hulka yake ya kutaka sifa za kijinga kutoka kwa malofa.
 
Hizi taarifa za kuchangia zinapatikana wapi ili na wengine wachangie?
 
Inamtesa hulka yake ya kutaka sifa za kijinga kutoka kwa malofa.
Hulka ya ulaghai, uongo na uovu inayomhusu Samia Suluhu Hassan ambayo sasa ipo wazi kabisa unaizungumziaje wewe?
Huoni kuwa tayari inamtesa huyu mwanamke hata kabla ya kufikishwa mbele ya haki?
 
Wekeni namba hapa tutume chochote kitu kabla mwaka mpya haujaingia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…