Simba wanajua ku deal na soka la kisasa. Yanga wako too local ... hawana utaratibu wa kuuza au kuruhusu wachezaji wao muhimu kwenda kutafuta maisha nje. Walikuwa radhi hata kuweka Walinzi Airport kuzuia wasitoroke. Yanga ni wabinafsi sana.
Hata Nonda Shabani, aliamua kutoroka kwenda South Africa baada ya kubaniwa. Ndo maana Yanga waliambulia patupu alipoenda kucheza Ulaya ilhali wao ndio walimlea pale Yanga "B".
Sitasahau walichomfanyia Edibilily Lunyamila baada ya kupata dili la Kucheza Bundesliga! Kisa tu walikuwa na mechi na watani wao, hivyo walitaka Lunyamila acheze kwanza hiyo game halafu wamruhusu kuondoka. Baada ya game hiyo, Wajerumani wakamwambia nafasi yako tumeshaiziba tayari.
Hata Ngasa, kwenda West Ham kufanya majaribio ilikuwa taabu sana ... Kijana wa watu akakonda kwa stress, alipofika kule akaambiwa huna fitness ya kucheza EPL kwa sababu mwili wake ulionekana kukosa lishe. Yanga bhana ...!
Ngoja niishie hapa ...! Watani zangu msinirushie mawe, kuweni professional jamani!!!