Tunakoelekea uchumi unaenda kufa

Tunakoelekea uchumi unaenda kufa

Mpendakukimbiakimbia

Senior Member
Joined
May 18, 2018
Posts
151
Reaction score
274
Kila dalili zinaonesha tunaingia kwenye socialist ecomic system ambayo inaua uchumi. Baadhi ya disadvantages za socialist au comand au plannd economy ni zifuatazo.
1. No political freedom
2. Slow envestments and slow economic growth
3. No individual initiatives
4. No interaction of economic variables nk

Hii inatokana na kwamba sasa hivi matamko ndo yanaongoza uchumi hivyo hata wale wawekezaji wachache waliotaka kuwekeza wataogopa mana lolote linaweza kutokea na hii nimbaya sana inaitwa risk kwa mwekezaji. Hamna mtu ambaye atakuwa inovative tena mana unaweza kupotzwa. Hakutakuwa na mzunguko mzuri wa pesa na comfities yaan velocity of currency na transaction vitapungua which will eventually give rise to prive hence hype inflation. Sasa hivi tunaenjoy mfuko wa bei kupungua lakini ni at the expnse of people. Mbayw zaidi ni kwamba badala ya kusarpot watu wakue kibiashara serikali inafunga na kudiscourage kabisa kwa kigezo kwamba ni wezi. Ajira zimepungua ambapo consumption level inakeenda chini sikuhadi siku. Throgh paradox of thrift hata saving inakwenda chini maana yake ni kwamba baada ya mwaka au miwili hivi mabenk yatakosa ukwasi na kujifunga automatically.

Kwa wachumi wamenielewa. Ni hayo tu kwa leo nitaendela kutoa somo
 
Ma mdogo sio kila kitu unapinga,mi juzi kati nimeenda chalinze nikakuta yanajengwa makao makuu ya wilaya pamoja na stendi ya mabasi kama ya Mbezi.Nilivyoona hivyo nikashusha pumzi na kutabasamu,nikasema ngoja niende kwenye kijiji cha jirani ambapo kuna kiwanja-Shamba changu eka moja napo nikakuta wamejichanganya eti wanachimba msingi ili wajenge zahanati ya kijiji,wanachonga barabara ya kuelekea kijiji cha Wamasai.
kilichonifurahisha zaidi wamepima nguzo za umeme utakaoenda Zahanati ya kijiji mbele ya kiwanja changu.Mungu anipe nini mimi?Yaani hapa nimeutuliza mshono wangu na ntaendelea kuutuliza nikiwa nasubiri SGR ikamilike nikapandie NGERENGERE ili niwe nakuja Dar kufanya kazi na jioni kurudi Chalinze kwenye mjengo wangu.
Ushauri:Ma mdogo we tuliza tu mshono maana hamna namna na ukijichanganya kuleta makuzi Ninja anakuletea Defender kitaani kwenu
 
Last edited:
Ni kawaida na wengine tumeshazoea kutabiriwa mabaya,tuambie KIBUYU chako cha RAMLI kinasema lini uchumi utakufa?
 
Uko sawa kabisa, na hizi pesa tunazokopa kwa ajili ya hii miradi ya mtu apate sifa ndio tutakoma, nakumbuka enzi ya kukimbiza gari la ugawaji na bia za harusi unazifuata tbl soda keko cocacola halafu unazipakia pale kwenye yard yao za mooto unaziingiza holini ni chai kabisa kilichokosekana mkate maana ni ya shida.
Jinsi wanunuzi tunavyozidi kupungua lazima production ishuke na kusababisha scarcity, ndiko tunakoelekea lakini huwa inakua taaratibu, kwamba bandarini skuizi mizigo/meli zimepungua si siri ingawa takwimu zinafichwa sisi tunaoshinda humo tunaona, wenzetu waliovaa miwani ya mbao mpaka watakapo ivua ndio watajua tumedanganywa
 
Ma mdogo sio kila kitu unapinga,mi juzi kati nimeenda chalinze nikakuta yanajengwa makao makuu ya wilaya pamoja na stendi ya mabasi kama ya Mbezi.Nilivyoona hivyo nikashusha pumzi na kutabasamu,nikasema ngoja niende kwenye kijiji cha jirani ambapo kuna kiwanja-Shamba changu eka moja napo nikakuta wamejichanganya eti wanachimba msingi ili wajenge zahanati ya kijiji,wanachonga barabara ya kuelekea kijiji cha Wamasai.
kilichonifurahisha zaidi wamepima nguzo za umeme utakaoenda Zahanati ya kijiji mbele ya kiwanja changu.Mungu anipe nini mimi?Yaani hapa nimeutuliza mshono wangu na ntaendelea kuutuliza nikiwa nasubiri SGR ikamilike nikapandie NGERENGERE ili niwe nakuja Dar kufanya kazi na jioni kurudi Chalinze kwenye mjengo wangu.
Ushauri:Ma mdogo we tuliza tu mshono maana hamna namna na ukijichanganya kuleta makuzi Ninja anakuletea Defender kitaani kwenu
Stendi za magari na zahanati kujengwa ni kigezo cha uchumi kukuwa nifafanulie mkuu?
 
Musiba hua simkubali lakini juzi kuna pointi moja ameizungumza nikamuelewa vizuri .
Suala la Kuijenga CUF. Alishauri maalim Seif na Lipumba wakae meza moja waelewane. Wajenge Chama chao kiwe imara.
Nikagundua kumbe watu wengi wanapenda kuona vyama imara kitaasisi sio watu binafsi.

Mpaka sasa hatujawahi kutawaliwa na chama kingine wala watu wengine zaidi ya wale wale ambao miaka kumi wanatuendesha kijamaa ,miaka kumi inayofuata wanatuendesha kwa free market economy.
Tatizo linakuja wale wale Leo wanaoamini katika Ujamaa wa serikali kuhodhi njia zote za uchumi hao hao kesho watakuja na soko huria kwa mbwembwe nyingi .
Na wanafanya hivyo kwa kujua kua binadamu ana tabia ya kuchoka na Mara nyingine kuchoka kwa sababu zisizo za kitaalam na uelewa mdogo wa kundi kubwa la wapiga kura.

Sasa kinachotokea ni wale wale kushindwa kusimamia hiyo mifumo miwili inayotekelezwa na watu wale wale na chama kile kile. Matokeo yake wanafanya kwa ajili ya kupata kura zao na kuendelea kutawala milele.

Fursa hiyo wanaipata kwa sababu hakuna vyama imara kitaasisi.

Ni ukweli kabisa kuwa kama kwenye chaguzi CUF,Chadema ,NCCR Mageuzi na ACT maendeleo wakiungana kwa lengo moja la kushika dola na kuimarisha mifumo ya kutawala bora kwenye nchi hii hakika CCM itaanguka vibaya.
Lakini cha ajabu Kuna ubinafsi uliozidi kwenye vyama hivyo.
Maeneo yenye nguvu kwa CUF yapo wazi yanajulikana.
Chadema nayo pia inayo baadhi ya Maeneo japo sio ya kudumu sana mana nguvu yao ni mtu mmoja mmoja. Ndio maana Unakuta Maeneo kama Hai akitoka Mbowe jimbo linarudi CCM mana wapo kimzuka tu sio imani mana hawajui nini hasa Mrengo wa Chadema kulingana na uchumi wa dunia.
Lakini kama Chadema wangekubaliana kwa pamoja na CUF Hasa ile CUF ngangari na Vyama vingine wakasimamia Sera moja na lengo moja la kukingoa chama cha mapinzuzi kilichowaonea na kuwadhulumu kwa miaka 25 nadhani wangefanikiwa hasa wingi wa wabunge na madiwani na hata kushika dola.

Kwa sababu tunaongozwa kwa Sera za chama cha mapinduzi kwa nusu karne basi tuwaache wafanye wanavyoona watapata kura 2020 mana hakuna chama au Sera nyingine yenye lengo la kushika dola.
 
Last edited:
Wewe kama wewe umefungua biashara gani Serikali ikakufungia na kukuita mwizi?
Wavivu tu hao!
Ndiyo hao waliosema sitoki nje kuna mbweha mkubwa!
Sisi tuendelee kusonga mbele na nchi yetu!
 
Wavivu tu hao!
Ndiyo hao waliosema sitoki nje kuna mbweha mkubwa!
Sisi tuendelee kusonga mbele na nchi yetu!
Bila katiba mpya hii chama chetu pendwa kitaebdelea kutawala milele kama alivyosema Mwenyekiti wetu. Kama mungeweza wapinzani mngeidai hiyo ingeweza mubadilosha mambo. Vinginevyo ni kelele za mlango tuu ambazo cku zote hazimfanyi mwenye nyumba ashindwe kulala
 
Katiba mpya itasaidia nini kama hiyo iliyopo hajawahi kuheshimiwa wala hakuna mtu wa kuhoji inavyobinywa?
 
Katiba mpya itasaidia nini kama hiyo iliyopo hajawahi kuheshimiwa wala hakuna mtu wa kuhoji inavyobinywa?
Katiba mpya itasaidia wasababu iliyopo ni mbovu na mbinyaji wake nani wa kumgusa?

Mbinyaji mkuu mwenyewe, katiba iliyoko inamlinda yeye na ubinyaji wake na chochote atakachotaka kufanya akiwa madarakani, sasa kumuacha aendelee ndo solution?.Sijui watanzania mnafikriaje? Naona kama wengi hakuna uwezo wa kufikiri kabisa.
 
Kila dalili zinaonesha tunaingia kwenye socialist ecomic system ambayo inaua uchumi. Baadhi ya disadvantages za socialist au comand au plannd economy ni zifuatazo.
1. No political freedom
2. Slow envestments and slow economic growth
3. No individual initiatives
4. No interaction of economic variables nk

Hii inatokana na kwamba sasa hivi matamko ndo yanaongoza uchumi hivyo hata wale wawekezaji wachache waliotaka kuwekeza wataogopa mana lolote linaweza kutokea na hii nimbaya sana inaitwa risk kwa mwekezaji. Hamna mtu ambaye atakuwa inovative tena mana unaweza kupotzwa. Hakutakuwa na mzunguko mzuri wa pesa na comfities yaan velocity of currency na transaction vitapungua which will eventually give rise to prive hence hype inflation. Sasa hivi tunaenjoy mfuko wa bei kupungua lakini ni at the expnse of people. Mbayw zaidi ni kwamba badala ya kusarpot watu wakue kibiashara serikali inafunga na kudiscourage kabisa kwa kigezo kwamba ni wezi. Ajira zimepungua ambapo consumption level inakeenda chini sikuhadi siku. Throgh paradox of thrift hata saving inakwenda chini maana yake ni kwamba baada ya mwaka au miwili hivi mabenk yatakosa ukwasi na kujifunga automatically.

Kwa wachumi wamenielewa. Ni hayo tu kwa leo nitaendela kutoa somo
Uchumi wa kitapeli, rushwa , wizi, ufisadi ndio unakufaa mkuu
 
Back
Top Bottom