Tunahakiki qualifications au vyeti feki?

Huyo waaziri siku zote huwa ni mzigo mkubwa sana. Hajielewi hajui kuchambua hoja. Yeye siku zote huwa anasifia hoja, kauli, na matamko ya chama chake.

Hii imepelekea yeye kukosa namna ya kujenga hoja zenye mashiko. Ni mtu wa hovyo sana.
Ni mwanamama asiyejitambua. Sijui rangi ile ndo inawapumbaza?

Bado Mhagama na Mwalimu..yaani acha tu
 
Upande wa vyuo ni ngumu kidogo mpaka ufanywe na chuo alichosoma mhusika, chuo ndiyo kinatoa cheti na siyo TCU wala NACTE.
 
Ni kweli. Huyu nimemupoint coz JPM ana leta masihara kwa huyu dogo.


Hapana, si kweli.

Yupo toka mkuu wa Wilaya serikali ya Kikwete mpaka mkuu wa Mkoa serikali ya Magufuli hatujasikia kashfa ya vyeti, mlikuwa wapi siku zote? Mpaka alipotangaza vita vya madawa ya kulevya ndiyo hiyo silaha ya vyeti imeibuka?

Nachukulia kuwa hiyo ni silaha ya wahusika wa madawa ya kulevya mpaka dakika hii.
 
JK hakuwahi kufanya uhakiki wa vyeti.

JPM kaja na hili jambo na kama JPM hajiamini aache kuropoka vitu asivyo na uwezo navyo!!

Dada yangu, tambua vyeti na madawa ni vitu viwili tofauti. Vyeti ni jambo la dk 5 tu. Mm namuunga mkono kuwa kushughulikia wauza madawa. Ila siyo kugeuza madawa kama kitega uchumi chake cha kumiliki magari, viwanja, magorofa na samani mbalimbali za wauza madawa.

Vyeti kwanza.
 


Alifanya, uhakiki wa vyeti ulianza rasmi 2008, sema JK hakufanya kwa mkupuo wa kusimamisha shughuli zote mpaka uhakiki uishe, alikuwa akifanya kidogo kidogo na wengi uliwakumba kimya kimya.

Si unajuwa JK ni mwanadiplomasia wa hali ya juu na hakupenda kudhalilisha mtu, mtu anashikwa na vyeti feki anawachishwa kazi kimya kimya au anapelekwa mahakamani kimya kimya.

Unafikiri anaeachishwa kwa cheti feki atakwambia kuwa aliachishwa kwa vyeti feki? Thubutu.

Jakaya hata yule aliyewita dhaifu bungeni siku anafungua ujenzi wa chuo kikuu cha tiba Mloganzila alimpa mkasi huku anacheka anamwambia "bwana mii dhaifi hata mkasi unanishindam njoo kata utepe huu ufungue rasmi huu ujenzi". Huyo ndiye JK, hana kinyonggo hana tatizo na mtu, yeye nia yake ilikuwa maendeleo tu. Jikumbushe:

 
Hapo kwa JK kwa dipomasia, subira,na utu sina shaka nae kabisaaa.

Nashukuru kwa hili sikuwa nafahamu.
 
Umeandika vizuri lakini pale ulipoanza ushabiki wa kum pinpoint mtu mmoja nikahisi kama wewe ni muhusika wa madawa ya kulevya kwa namna moja nyingine.
Madawa ya Kulevya na vyeti feki vina uhusiano gani hapa wewe bibi??
 
Hivi Angela Kairuki humu yumo kweli!?
Wangethubutu kumuweka makonda ndalichako na kairuki wote wangetumvuliwa
 
Swali lako ni la msingi.
Kabla ya kujibu kuwa ni# 1 au 2 ninapenda nianze kueleza ifuatavyo:
Uhakiki uliofanywa ni wa vyeti vya form4 ku-compare na vyeti vya taaluma. Lakini cha msingi hapo ni cheti cha form4.
Ukitaka kumhakiki mtu hasa wafanyakazi mwambie akuoneshe vyeti vifuatavyo. Cheti cha kuzaliwa, ubatizo kwa wakristo, cha la7, form4,6,chuo na taaluma na living certificate zake.
Kwa suala la kughushi, vyote hivyo nilivyovitaja akivitoa kwa pamoja lazima umfume na disari.
Akitoa maelezo ya kukosa cha ngazi ya chini, mf;kama ana elimu ya chuo akakosa cha A level ama O level, muulize loss report ya polisi. Kama hana elewa, huyo aligawa ama kuuza cheti hicho alipofaulu ama alipomaliza elimu ngazi ya juu.
Vyote viangaliwe uhalali wake.
Kama ulivyouliza, kuna mtu kasoma hadi O level, akafeli. Akanunua cheti cha mtu cha pass akaendelea na masomo ya A level kwa cheti hicho na akamaliza na kufaulu kwenda chuo.
Hapo ndiyo kwenye utata. Aliyefaulu hakusoma, aliyefeli kasoma hadi chuo kikuu.
Mwenye jina halisi kaishia form4. Aliyeghushi kasoma hadi chuo!
Mfano wa pili, kuna watu hawakusoma kabisa. Walinunua vyeti halali na kutafutia ajira. Hawa kwa sasahivi wanaonekana kama wana vyeti halali na wamesoma.
Mfano wa tatu ni kwa watu waliofeli ama hawakusoma, ila waliazima vyeti vya watu na kuvi- scan kwa majina yao na kuombea ajira, pia wapo walionunua kwenye kiwanda kilichokamatwa karibu na posta kilichokuwa kinafyatua vyeti "orignal" .
Sasa hawa ndo serikali imewamulika mapema. Lakini wote waliobakizwa bila kumulikwa, si wote wenye elimu yenye sifa ya vyeti vyao.
Kikubwa hapa si kusomea taaluma. Kughushi nyaraka ni kosa la jinai.
Pia kwa wale walio wagawia ndugu zao ama kuviuza walitenda kosa la kusaidia uhalifu, nao pia wanastahili kushitakiwa.
 
Dhambi ni dhambi tu hakuna dhambi nyeupe au nyeusi
1. Mfano unaujua mziki Wa form 6, yaani two years sulba!
Then mshenzi tu et afoj chet cha form 6,
Na kuingia university, na kujinyakulia degree yake yake ya fedha kimagumash na kukamata kitego cha Fedha BOT kimagumashi, huyu ndo awe bora?
Are you crazy???
 

Duu, Mkuu hapo bold nimejiskia vibaya sana!! Wala sikuwa na lengo baya kabisaa
 
Kuwepo tangu Awamu ya Kikwete sio Utetezi,Na Kusema kwann hakutuhumiwa kabla ya kutangaza wauza madawa ya kulevya pia sio Utetezi,Nakukumbusha tu Kuwa Jinai haina Mwisho,UKIUA MTU hukuonekana hata ikipita miaka20 ndio ikija kuthibitika pasi Na shaka kuwa ulitenda kosa hilo unashitakiwa na hukumu utapewa hivyo Vita ya Madawa sio hoja Vita ya Madawa inatakiwa kupiganwa na Vita ya forgery pia inapiganwa! OTHERWAYS,ni doublestandard
 
Mm nafikir yatosha uhakiki kwa sasa ili vijana waajiriwe. Mana ukija uhakiki mwingine mwaka wa pil utaongezeka ktk zuio la ajira.
 


Kuna nani alikwambia hapa kuna anaetetewa?

Kila mtu atabeba msalaba wake.

Huyo mkuu wa mkoa si kisha-shtakiwa tume ya maadili na meya wa Kinondoni? Au hilo hukulisoma juu huko?
 
Mawazo kama haya yanaachwa yakiharibika, wahusika wanajifanya viziwi kwa lazima!!
 
Private Sector, waajiri wanajukumu la kujiridhisha na uhalali wa vyeti vya wafanyakazi wao.

Private Sector wanaangalia zaidi performance na delivery kuliko vyeti.

Napingana na wewe kuwa Tanzania hakuna uhaba wa ajira, eti tatizo ni watu wamekaa kwenye nafasi zisizo zao. Huu ni upotoshaji wa hali ya juu. Ndio maana hata wale 'vilaza' wa UDOM walikuwa wanashingilia eti izo nafasi watapewa wao.
 
Private sector ipi? Tupe mfano wa taasisi hiyo isiyo angalia vyeti?

Issue ajira, mf hizo nafasi 9932 zikitangazwa kutakuwa kuna uneployment kiasi gani tena?

Je uhakiki ukigusa private sector 2m employees na kubaini hata vyeti feki 30,000. Na nafsi zote 40,000 kutangazwa na kujazwa. Tatizo la ajira litatoka wapi tena Tz?
 
No situation is permanent. Juzi kati, nipo kwa long queue NMB MKOANI hapa Kibaha, akaja RC wa zamani enzi ya BEN, Mzee Nicodemus Banduka,kachoka mbaya, ni huruma sana! Cheo ni dhamana!
 
Nisome vizuri,sijasema Private Sector hawatakiwi kukagua vyeti, bali waajiri wenyewe kwenye Private Sector ndio wenye jukumu la kujiridhisha na uhalali wa vyeti vya wafanyakazi wao.
Lakini pia Private Sector, performance na delivery ni vitu muhimu zaidi kwao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…