Tuna siku tatu hatuna Umeme Kigamboni

Tuna siku tatu hatuna Umeme Kigamboni

Update: Nimecheki na Tanesco muda mfupi uliopita, umeme kurejea kabla ya saa sita mchana. Kazi ya ukarabati imeisha, wanafanya uhakiki kabla ya kuwasha umeme. Poleni kwa usumbufu.
Dkt Faustine Ndugulile-Mbunge
 
Update: Nimecheki na Tanesco muda mfupi uliopita, umeme kurejea kabla ya saa sita mchana. Kazi ya ukarabati imeisha, wanafanya uhakiki kabla ya kuwasha umeme. Poleni kwa usumbufu.
Dkt Faustine Ndugulile-Mbunge
Nimependa unavyokuwa karibu na wananch wako na kuwapatia majibu ya maswali yanaowatatiza,naiman mmbunge wangu iddy azan anapitaga hapa,namwomba akamtafute mkarandarasi alopewa kazi ya kutengeneza barabara za mitaani hasa kule kigogo,maji ya mvua yamezichimbua tena zile barabara na mashimo yamejitokeza sana.zile taa zilowekwa mitaan aziwak,na baadh ya nguzo moja kwenda nyengne nyaya hakuna,je mirad ya namna hii s ni kuchezea kod za wananch au hela za wafadhil kama barabara azimaliz hata miaka 2? embu tembelea kagua tena hii miradi ikiwemo kero ya umeme mdogo kwa baadh ya maeneo.
 
safi Mh. Mbunge kwa taarifa. Ila sina uhakika utendaji wa TANESCO unaenda sambamba na ahadi yao!!!
 
Update: Nimecheki na Tanesco muda mfupi uliopita, umeme kurejea kabla ya saa sita mchana. Kazi ya ukarabati imeisha, wanafanya uhakiki kabla ya kuwasha umeme. Poleni kwa usumbufu.
Dkt Faustine Ndugulile-Mbunge
Asante sana Mbunge wetu kwa updates, ni kweli umeme umerudi..na umerudi kabla ya saa sita mchana. Tunakushukuru kwa ufuatiliaji wa karibu kwa niaba ya wananchi wako.
 
Mheshimiwa sana mbunge, ninashukuru kwa taarifa. Ni kweli maeneo ya mji mwema...umeme umerudi.

Swali la nyongeza: TANESCO (M) Temeke wana mpango gani wa kukabiliana na tatizo hili wakati mwingine? Nina uhakika huu si mwisho wa mvua kubwa kunyesha.
 
mheshimiwa,hapa tuamoyo bado ni majanga,msaada tafadhari wapigie simu wape taarifa

Mh. Tunashukuru kwa ufuatiliaji wa karibu, lakini mpaka hivi sasa eneo la Toangoma hadi Kongowe kigamboni, umeme bado, sijui unaweza kuendelea kuwasiliana na Tanesco, maana tunajiona km sisi ndio hua wa mwisho kutatuliwa matatizo yetu.

Asante
 
Katika Jiji la DSM kuna kisiwa maarufu sana ambacho hata Serikali imefikiria kujenga mi mpya. Ni huko Kigamboni.


kwa siku ya tatu leo hakuna Umeme; mji huu mpya unategemea maji kutoka katika visima virefu (Hakuna maji ya kutoka RUVU) ambavyo lazima Pump itumike kuvuta maji.

Hivyo kutokana na ukosefu wa umeme siku ya tatu na haijulikani itaisha lini imekuwa ni kero kwa wakazi wa mji huo mpya.

hakuna Umeme, hakuna maji.....Siku ya tatu Giza, no kuoga, no kufua, vyoo vinanuka na hakuna mawasiliano ya simu kwani zimezima charge.


Jamani TANESCO FANYENI JUHUDI KUWARUDISHIA HUDUMA YA UMEME



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!

Na bado. Mtakaa gizani sana
 
Mh. mbunge imeme umerejea kinadharia sio kivitendo. Nilisema awali wanachosema TANESCO hakifanani na utendaji wao.!!!
 
Umeme umerudi kweli saa 7.umewaka dakika chache umekatika mpaka sasa hatuna umeme Mbagala.
 
Nitawapeni mrejesho kadri ninavyoupata toka kwa uongozi wa Tanesco. Poleni kwa usumbufu.

Asanteni.
Dkt Faustine Ndugulile-Mbunge Kigamboni
TANESCO hawatakiwi wakupe wewe mrejesho ili uje kutupa sisi mrejesho huku Jamiiforums.

Waambie wautangazie umma kwenye vyombo vipana vya habari nini kinaendelea.

Official public statement inatupa commitment juu ya wanachodai watafanya, sio mirejesho ya mawasiliano binafsi ya text message kati ya Mbunge na Meneja Masoko fulani na JF.
 
Update: Umeme umerejea. Nijulishe kama kuna maeneo ya Tarafa ya Kigamboni au Mbagala yasiyo na umeme. Asanteni.

Kwa hili unafanya vizuru ila yale mfanyayo pale Mwembe yanga sio sahihi. Kwa nini munawapotosha watu kuhusu huo muundo wa serikali ya Muungano? Kwanza Tume ilishapita na maoni wametoa sasa mikutano yamisimamo ya nini?


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Duh umeme ulikuwa gereshaeeee.....!!! Umewaka dakika 23 tu ukakatika aisee...hadi sasa holla!!!

Tanzania hii..mh!!!
 
Back
Top Bottom