Rais wa awamu ya 5 ajitahidi kurekebisha mfumo wa utendaji serikalini ili kuongeza ufanisi,kwani Wanasiasa wamekuwa wanaingilia utendaji wa Serikali.mfano Mwanasiasa(Waziri,Mkuu wa Mkoa,au Mkuu wa Wilaya) wamekuwa wanatoa maagizo bila kuzingatia mashauriano au bila kufuata taratibu na kanuni za uendeshaji wa Taasisi:
1.Utakuta Kiongozi wa siasa anatoa amri mbele ya jukwaa ili wananchi washangilie matamko,huku akijua kila kitu kinatekelezwa kulingana na bajeti.
2.Waziri Mkuu,Wakuu wa Mikoa,na Wakuu wa Wilaya kuwakataza Wakulima wasiuze mazao waliyolima kwa nguvu zao ili kupata kipato na chakula(jambo ambalo limewafanya wakulima kuwa masikini kwa miaka zaidi ya 50).
3.mfano Tanesco ni taasisi,lakini unakuta maagizo yanatoka kwa mwanasiasa bila kufuata taratibu hivyo kujikuta kila siku shirika linadhoofika.!!!
4.Rais wa awamu ya 5,asitumie maneno ya watangulizi wake,ambayo yaliendelea kuwafanya Watanzania kuwa wanyonge kila siku(mfano:"Tanzania ni nchi masikini","Wakulima msiuze chakula mtapata njaa","Pesa zote tumepeleka Halamshauri",'Kuna mchwa Halmshauri","ninawajua wezi","ninajua wauza madawa ya kulevya","tutawaomba wafadhili kutusaidia miradi ya maendeleo").
5.Kwa vile,kauli mbiu ya 'Hapa Kazi" imeshasikika na kupokelewa na wananchi,sasa fitina na unafiki uepukwe kwa kutokubali Viongozi wa siasa ambao ni wasimamizi wa watendaji kuwa na kauli zenye kuidhoofisha Serikali mbele ya wananchi,mfano hii kauli ya kusema "Watendaji ndio wanaosababisha ilani inashindwa kutekelezwa","Watendaji ndio wanaokiangusha chama"
6.Sheria/Waraka zinaweza kuongeza ufanisi ziboreshwe,mfano mwanasiasa ambaye sifa yake ni kujua kusoma na kuandika na kuandika anawezaje kumsimamia mtaalamu mwenye Diploma/Digrii?
7.Sasa utafiti ufanyike katika maeneo ambayo hayana ufanisi au ni kero kwa wananchi:Iweje Wakubwa watoto wao waende Shule za "English medium",lakini Serikali ishindwe kubadili mfumo wa Elimu unaoweza kuondea tofauti hii,mimi kwa matazamo wangu shule zote za Msingi zifundishe masomo yote kwa Kiingereza ili kuweza kushindana na ulimwengu wa sasa(Tuache unafiki kuwa Elimu itolewayo kwa masomo yote kwa kiswahili haina shida).
8.Mfumo wa kuendesha Halamshauri urekebishwe mfano suala la mipango miji uangaliwe upya ikiwezekana kuendelea kuunda "Agency" kwa baadhi idara zilizopo Halamshauri ili kuharakisha maendeleo kwa wananchi na vile vile kuepusha baadhi ya shughuli ambazo zinakwamishwa na urasimu wa siasa za ngazi ya madiwani ambao wengine hata darasa la saba hawakumaliza!!!
8.Yapo mengi ya kurekebisha kwa kuzingatia sekta mbalimbali,mimi kwa sasa niishie hapo wananchi na watumishi wa umma huwa wanasubiri kutekeleza maagizo na kauli za viongozi.