Tumia Router za Fiberhome kama Access Point (AP)

Tumia Router za Fiberhome kama Access Point (AP)

QasraNet

Member
Joined
Jan 3, 2018
Posts
38
Reaction score
50
Baada ya research ya muda mfupi iliyosababishwa na kuongezeka kwa bei za Access Point nimekuja na suluhu ya bei rahisi, salama na yenye uwezo sawa na ule wa special Access points devices.

Kuna hizi router zinazotumiwa na watoa huduma wa fiber, hizi router zimetengezwa maalum kwa matumizi ya fiber kutoka kwa ISP iwe kama WAN. Hapa nitaongelea hizi za Fiberhome. Hauna haja ya kwenda kuhangaika YouTube na kufanya research tena. Soma ukiona umeelewa na unaweza kufanya basi unyama kafanye.

Router Models (ambazo zinapatikana kwa wingi kariakoo):
1. Fiberhome HG6145D2
2. Fiberhome HG6143D4

Specifications Muhimu:
Wi-Fi 5
(802.11ac): Supports faster wireless speeds with dual-band (2.4GHz & 5GHz) for better coverage and capacity.
AC1200: The theoretical max Wi-Fi speed is around 1200 Mbps (e.g., 300 Mbps on 2.4GHz + 867 Mbps on 5GHz).

Bei ya mtumba pale kariakoo (pia unaweza kupata mpya):
TZS. 30,000 unaweza kushuka hadi 20,000 ukinunua nyingi hata kwa 18,000. Wanauza bila power adapter.

Namna ya kufanya Setup:
• Hakikisha una kifaa chenye uwezo wa kuConnect na wifi au kuchomekwa waya wa LAN. Mfano: 📱Smartphone, 💻Laptop, 🖥️Desktop au Tablet.
• Hakikisha una Adapter au Powerbank inayotoa DC 12V 2A au 12V 1.5A (Soma nyuma ya Router utajua adapter inayohitajika).
• Hakikisha una Ethernet Cable (RJ45) ya kuConnect kutoka kwenye Hii router yetu tunayoenda kuifanya iwe AP ---->> waya uende kwenye switch au router itakayokuwa inatoa internet. Urefu wa waya utaangalia mahitaji yako na matumizi yako. Unaweza ukawa unataka uifunge ofisini ambako waya wa internet umefika ila wifi haifiki n.k.

Cha kufanya:
Connect Fiberhome Router kwenye adapter then chomeka kwenye umeme (kiufupi ipe power) ---->>> Baada ya taa za Router kuwaka subiri dakika 1 kisha Chukua peni au sindano ingiza kwenye tundu ndogo ya Router iliyoandikwa Reset au RESET ---->>>> Bonyeza kwa sekunde kadhaa kisha Taa zina Blink router itazima na kuanza kuwaka upya taa 1 tuu, hapo itakuwa tayari umeReset hiyo Router ---->>>> Chukua simu yako au laptop then tafuta jina la wifi mpya yenye jina sawa na jina la wifi lililoandikwa nyuma ya Fiberhome Router yako, tazama password zake hapo hapo nyuma kisha connect to it. Itakwambia no internet wewe connect tuu aidha always au connect anyway kama ni desktop na haina wifi basi tumia lan cable connect from pc to Fiberhome Router ---->>>> fungua browser yako kisha andika 192.168.1.1 itakuletea login ingie kisha fanya settings za SSID (Wifi name) na Password then just save. ---->>>> connect kwenye wifi yenye jina uliloSet (itakwambia no internet) just connect; then chukua waya wa Ethernet utoe kwenye Router yako (sources of internet) kisha chomeka kwenye LAN 3 ya Fiberhome Router yako. LAN 3 ina act kama WAN so itaConnect internet. ---->>>> Utakuwa umemaliza.

Superadmin Login credentials
username
: adminSuper
password: %0|F?H@f!berhO3e
au
username
: admin
password: %0|F?H@f!berhO3e

Hizi Router zinauzwa kariakoo (Katikati ya makutano ya Uhuru/Kongo na Uhuru/Msimbazi) hapa kati hapa. 😁

📍Kwa location ya Google Map bonyeza hapa.
 

Attachments

  • 20251218_123140.jpg
    20251218_123140.jpg
    579.1 KB · Views: 14
  • 20251218_122942.jpg
    20251218_122942.jpg
    612.3 KB · Views: 9
  • 20251218_123037.jpg
    20251218_123037.jpg
    727.2 KB · Views: 12
  • 20251218_123127.jpg
    20251218_123127.jpg
    383.2 KB · Views: 13
  • 20251218_122951.jpg
    20251218_122951.jpg
    523.9 KB · Views: 13
  • 20251218_123114.jpg
    20251218_123114.jpg
    418.4 KB · Views: 14
  • images (22).jpeg
    images (22).jpeg
    21.8 KB · Views: 13
Hapa sasa unakuwa unapata huduma kutoka kwenye mtandao upi? na unalipia vipi?
 
Hapa sasa unakuwa unapata huduma kutoka kwenye mtandao upi? na unalipia vipi?
Mkuu, tunaposema AP (Access Point) inamaana ya WiFi device ambayo itaAct kama extender ya network yako kuifikisha sehemu fulani kuwezesha watu kujiunga na kuAccess internet yako. Hivyo hiyo internet inachukuwa kwenye Router yoyote kupitia Ethernet Port 3. Uwe unachukua internet kutoka TTCL, Airtel, Vodacom, Yas, Halotel, Savannah n.k as long as router za hao watoa huduma wako zina port ya Ethernet basi unaweza kuchomeka kutoka kwenye huyo mtoa huduma wako kwenda kwenye access point yako.

** Ila kwakuwa hukuelewa tangu pale awali, usipoelewa na hapo kaka basi ujue tunaongea kitu nje ya utawala wako. 🙏🏻
 
Mkuu, tunaposema AP (Access Point) inamaana ya WiFi device ambayo itaAct kama extender ya network yako kuifikisha sehemu fulani kuwezesha watu kujiunga na kuAccess internet yako. Hivyo hiyo internet inachukuwa kwenye Router yoyote kupitia Ethernet Port 3. Uwe unachukua internet kutoka TTCL, Airtel, Vodacom, Yas, Halotel, Savannah n.k as long as router za hao watoa huduma wako zina port ya Ethernet basi unaweza kuchomeka kutoka kwenye huyo mtoa huduma wako kwenda kwenye access point yako.

** Ila kwakuwa hukuelewa tangu pale awali, usipoelewa na hapo kaka basi ujue tunaongea kitu nje ya utawala wako. 🙏🏻
Asante kwa maelezo mkuu nimekupata
 
Baada ya research ya muda mfupi iliyosababishwa na kuongezeka kwa bei za Access Point nimekuja na suluhu ya bei rahisi, salama na yenye uwezo sawa na ule wa special Access points devices.

Kuna hizi router zinazotumiwa na watoa huduma wa fiber, hizi router zimetengezwa maalum kwa matumizi ya fiber kutoka kwa ISP iwe kama WAN. Hapa nitaongelea hizi za Fiberhome. Hauna haja ya kwenda kuhangaika YouTube na kufanya research tena. Soma ukiona umeelewa na unaweza kufanya basi unyama kafanye.

Router Models (ambazo zinapatikana kwa wingi kariakoo):
1. Fiberhome HG6145D2
2. Fiberhome HG6143D4

Specifications Muhimu:
Wi-Fi 5
(802.11ac): Supports faster wireless speeds with dual-band (2.4GHz & 5GHz) for better coverage and capacity.
AC1200: The theoretical max Wi-Fi speed is around 1200 Mbps (e.g., 300 Mbps on 2.4GHz + 867 Mbps on 5GHz).

Bei ya mtumba pale kariakoo (pia unaweza kupata mpya):
TZS. 30,000 unaweza kushuka hadi 20,000 ukinunua nyingi hata kwa 18,000. Wanauza bila power adapter.

Namna ya kufanya Setup:
• Hakikisha una kifaa chenye uwezo wa kuConnect na wifi au kuchomekwa waya wa LAN. Mfano: 📱Smartphone, 💻Laptop, 🖥️Desktop au Tablet.
• Hakikisha una Adapter au Powerbank inayotoa DC 12V 2A au 12V 1.5A (Soma nyuma ya Router utajua adapter inayohitajika).
• Hakikisha una Ethernet Cable (RJ45) ya kuConnect kutoka kwenye Hii router yetu tunayoenda kuifanya iwe AP ---->> waya uende kwenye switch au router itakayokuwa inatoa internet. Urefu wa waya utaangalia mahitaji yako na matumizi yako. Unaweza ukawa unataka uifunge ofisini ambako waya wa internet umefika ila wifi haifiki n.k.

Cha kufanya:
Connect Fiberhome Router kwenye adapter then chomeka kwenye umeme (kiufupi ipe power) ---->>> Baada ya taa za Router kuwaka subiri dakika 1 kisha Chukua peni au sindano ingiza kwenye tundu ndogo ya Router iliyoandikwa Reset au RESET ---->>>> Bonyeza kwa sekunde kadhaa kisha Taa zina Blink router itazima na kuanza kuwaka upya taa 1 tuu, hapo itakuwa tayari umeReset hiyo Router ---->>>> Chukua simu yako au laptop then tafuta jina la wifi mpya yenye jina sawa na jina la wifi lililoandikwa nyuma ya Fiberhome Router yako, tazama password zake hapo hapo nyuma kisha connect to it. Itakwambia no internet wewe connect tuu aidha always au connect anyway kama ni desktop na haina wifi basi tumia lan cable connect from pc to Fiberhome Router ---->>>> fungua browser yako kisha andika 192.168.1.1 itakuletea login ingie kisha fanya settings za SSID (Wifi name) na Password then just save. ---->>>> connect kwenye wifi yenye jina uliloSet (itakwambia no internet) just connect; then chukua waya wa Ethernet utoe kwenye Router yako (sources of internet) kisha chomeka kwenye LAN 3 ya Fiberhome Router yako. LAN 3 ina act kama WAN so itaConnect internet. ---->>>> Utakuwa umemaliza.

Superadmin Login credentials
username
: adminSuper
password: %0|F?H@f!berhO3e
au
username
: admin
password: %0|F?H@f!berhO3e

Hizi Router zinauzwa kariakoo (Katikati ya makutano ya Uhuru/Kongo na Uhuru/Msimbazi) hapa kati hapa. 😁

📍Kwa location ya Google Map bonyeza hapa.
Ingekuwa unyama zaidi ungetafuta router inayoweza kuwekwa system ya Open Wrt.

Kuna jamaa anayo kaweka vpn humo humo ndani hakuna haja ya kuwasha vpn kwenye vifaa
 
hii kitu nimefanya mimi,kuna tatizo lipo sijajua linatokana na hii extrnal router au ni company yenyewe ya fiber ndio wamelimi...ipo hivi mimi nina tumia fiber ya hawa netsolution na extrnal router natumia ya airtel zile za kwanza..issue inakuja ili niweze kulog in kwa hii router ya pembeni lazima nijidisconect kwenye main router kwanza ndio napata acces ya kuingia.. then nikishamaliza ndio ni restart hii kitu inaniboaa mbaya.. je ndivyo inavyotakiwa iwe???
 
Back
Top Bottom