Tumekosea hapa

Tumekosea hapa

Edobeny

Senior Member
Joined
Nov 26, 2014
Posts
143
Reaction score
29
Kati ya mambo ambayo yamestua wengi kipindi cha karibuni ni kushuka kwa shilingi ya Tanzania kilinganisha na dola ya USA hadi kufikia £=2000 na kitu. Huku tukiwa tunamtafuta mchawi ni nani aliyeturoga, kuna vitu vya msingi ambavyo vimeachwa holela tu, vinachangia kwa kiasi kikubwa kuididimiza hela yetu chini zaidi na zaidi.

1. Ingia kwenye basi lolote la mkoani halafu jaribu kuuliza abiria wengine tiket wamekata kwa kiasi gani utashangaa. Kila mtu na bei yake lakini safari ni ile ile na basi ni lile lile. Kwa hapa bongo ukiondoa safar za morogoro, mikoa mingine yote haina fixed fare au nauli.

2. Nenda kariakoo, fanya utafiti mdogo tu ingia maduka matatu tofauti na ilizia bei ya kiatu au suruali ya aina ile ile. Bei utakazokuta utashangaa mwenyewe kila duka na bei yake kwa kitu kile kile. Hii maana yake nn? Kila mtu ana uamuzi wa kufanya kile anachotaka bila ya kuulizwa kwahiyo mzunguko wa hela unakuwa mdogo maana hela inabaki kwa wachache.

3. Cement za bongo mfuko mmoja ni 13500/= mpaka 14000/=, wakati kuna cement za pakistan pamoja na usafiri kutoka huko na kodi za bandari bado mfuko ni 10000/= mpaka 12000/=.

Viwanda vya ndani vinawakamua watanzania hata ukija kwenye bei ya sukari hailingani na uwepo wa viwanda vinne vya sukar nchini.

4. Bei ya nyumba za kupanga nalo ni tatizo, mwenye nyumba akiamka tu vibaya utasikia kuanzia Januari kodi inapanda hutaki unahama na ukihama leo kesho mwenzako ameingia wenye nyumba wamekuwa miungu watu. Mpangaji akajitetee wapi, hakuna vyombo vinavyoregulate kodi za nyumba, hakuna mtu anaesimamia. Je hizi nyumba zinalipa kodi maana ile ni biashara kama biashara nyingine, no one care.

5. Tofauti ya mishahara kati ya kima cha chini na cha juu. Tofauti ya mishahara kati ya wizara za serikali na mashirika ya umma hapa ndo unaweza kulia kabisa kama huna moyo wa jiwe.

Ukiangalia mshahara wa karani anaenza kazi kwenye halmashauri na yule anaenza kazi labda kwenye mfuko wa hifadhi wa umma tofauti ni kubwa sana.

Turekebishe ratio za mishahara atleast ifike 1:3 kati ya kima cha chini na kima cha juu.
 
Tusaidie sasa ku-relate/ conceptualise kila sababu ulioitoa to mdororo wa shilingi ili kila mtu akuelewe vzr mtaalam.
 
Nini kifanyike ?

jibu: Kuiondoa ccm madarakani october
 
Labda tubadilishe jina isiitwe Tanzania tena, iitwe Tanzanite Country, huenda matatizo haya yote yataisha, kila siku Tanzania Tanzania tangu uhuru hadi leo ni shida.
 
Kwa hili la nyumba umenena kwani mwenye nyumba ukimnyima chunvi basi kodi juu hata mkeo akimnyima basi utasikia hama tafuta nyumba ingine niachie nyumba yangu.
 
Tusaidie sasa ku-relate/ conceptualise kila sababu ulioitoa to mdororo wa shilingi ili kila mtu akuelewe vzr mtaalam.
Ili uchumi wa nchi uwe stable ni lazima kuwe kuna regulator inaweza kuwa ni chombo maalum nje ya BOT ambacho kitakuwa kinashughilika na kila nyanja ya au secta ya uchumi hii ni pamoja na kudhibiti bei ya bidhaa iwe sahihi. Vinginevyo kila mtu akiamua kuuza anavyotaka kutegemeana na mteja amekujaje au ni wa aina gani hii ni hatari hela itakuwa mikononi mwa wachache ambao watakuwa wanazihifadhi nje ya nchi na majority watakuwa hawana hela maana mzunguko ni mdogo. Labda nitoe mfano hapa suruali ya elfu 10, ikawa inauzwa kwa elfu 30-35. Hii ni mara tatu ya bei halisi maana yake kama ungenunua kwa elfu 10. Hela iliyobaki elfu 20 au 25 ingeingia kwenye mzunguko na wengine wangenufaika na hiyo tofauti na kupigwa 35 ikamnufaisha mtu mmoja ambae anaenda kuweka benki zikae zitulie. Matokeo yake BOT inabidi iingize tena hela kwenye mzunguko.
 
Ushauri wangu tubadilike sisi wenyewe tabia tulionayo si nzuri kubadilisha chama si sulishoni hivyo vyama vingine ni matatizo zaidi ni kama washangiliaji mpira kujifanya wanakosowa mchezaji wakati hata kupiga danadana hawazi
 
Kwa hili la nyumba umenena kwani mwenye nyumba ukimnyima chunvi basi kodi juu hata mkeo akimnyima basi utasikia hama tafuta nyumba ingine niachie nyumba yangu.
Nyumba zote za kupangisha zisajiliwe kama magari vile na ziwe na namba kulingana na mkoa au wilaya au mtaa . Vitu vya kuzingatia hali ya nyumba na gharama za upangaji ziwe fixed sio kiholela tu. Kwa hali hii hatuwezi kufika na tutasota sana maana always Landlords watamiliki uchumi na mwishowe wengi watakuwa masikini.
 
Ushauri wangu tubadilike sisi wenyewe tabia tulionayo si nzuri kubadilisha chama si sulishoni hivyo vyama vingine ni matatizo zaidi ni kama washangiliaji mpira kujifanya wanakosowa mchezaji wakati hata kupiga danadana hawazi
Hahaha! Wenye nyumba ndo wanasiasa, wafanya biashara ndo wanasiasa, wenye vyombo vya usafiri ndo hao hao basi ni kazi tu. Mm naamini haya yanaeleweka lakini nani atekeleze? Nani asimamie? Nani afuatilie? Kuna ugumu hapa mtu hawezi kujizibia mirija yeye mwenyewe.
 
Back
Top Bottom