Lole Gwakisa
JF-Expert Member
- Nov 5, 2008
- 4,728
- 2,259
Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanganyika, halafu Tanzania huru, rushwa inatolewa nje nje.
Tumeichekea na kuomba na kusali itokomee yenyewe bila kuchukua hatua madhubuti, tukifikiri Mola huko juu atasikia kilio hiki.
Leo rushwa imeingia Bungeni, tena kwa mbwembwe.
Safari hii maafisa waandamizi wa Serikali WAMEDIRIKI kuwapa rushwa wawakilishi wa wananchi ili wasiwatetee na kuupigia kelele uozo ndani ya dola.
Hili limetushtua sana, tena sana.
Imenichukua karibu masaa 12 hili litulie akilini na kuelewa maana yake halisi.
Si vizuri kuchimba mtu lakini lilotokea si la kawaida kabisa.
David Jairo ni Afisa mwandamizi mwenye mizizi iliyokomaa ndani ya Ikulu.Amekuwa na kulelewa enzi za Kambarage.
Leo kuyaona haya kwa tunaomfahamu, hili linatushangaza sana.
Lakini tata jilaumu wenyewe kwa vile rushwa leo imekuwa mchezo wa kuigiza, sasa hodi limefika sebuleni.
Tumeichekea na kuomba na kusali itokomee yenyewe bila kuchukua hatua madhubuti, tukifikiri Mola huko juu atasikia kilio hiki.
Leo rushwa imeingia Bungeni, tena kwa mbwembwe.
Safari hii maafisa waandamizi wa Serikali WAMEDIRIKI kuwapa rushwa wawakilishi wa wananchi ili wasiwatetee na kuupigia kelele uozo ndani ya dola.
Hili limetushtua sana, tena sana.
Imenichukua karibu masaa 12 hili litulie akilini na kuelewa maana yake halisi.
Si vizuri kuchimba mtu lakini lilotokea si la kawaida kabisa.
David Jairo ni Afisa mwandamizi mwenye mizizi iliyokomaa ndani ya Ikulu.Amekuwa na kulelewa enzi za Kambarage.
Leo kuyaona haya kwa tunaomfahamu, hili linatushangaza sana.
Lakini tata jilaumu wenyewe kwa vile rushwa leo imekuwa mchezo wa kuigiza, sasa hodi limefika sebuleni.