Tume ya Taifa imeitangazia Zanzibar uhuru?

Tume ya Taifa imeitangazia Zanzibar uhuru?

Izack Mwanahapa

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2011
Posts
497
Reaction score
236
KUMTANGAZA RAIS WA TANZANIA BILA MUSTAKABALI WA KURA ZA WAZANZIBARI NI KUITANGAZA ZANZIBAR HURU


Nianze kwa kurekebisha kauli ya mwenyekiti wa tume ya Taifa ya uchaguzi NEC alipokuwa akijaribu kuziokoa kura za Rais wa Jamuhuri ya muungano zilizopigwa na kuhesabiwa huko Zanzibar kwa kusema kwamba "Kuahirishwa kwa uchaguzi wa Zanzibar hakutaathiri mchakato wa uchaguzi Tanzania Bara" la hasha uchaguzi wa Zanzibar haujaahirishwa bali umefutwa na raisi anayetafutwa si Rais wa Tanzania bara bali Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.


katika hali kama hii dosari zilizotajwa na Mwenyekiti wa ZEC wakati akitangaza kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar ikiwemo ile ya Wapigakura kuwa wengi kuliko watu waliojiandikisha kwenye daftari inaathiri pia kura zilizopigwa na Wazanzibari kumchagua Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwasababu waliopiga kura ni watu walewale, kwa idadi ileile katika vituo vilevile na maboksi yaleyele.


Kwenye uchaguzi wa Zanzibar Maboksi yalikuwa matano kwa maana ya mabox ya kumchagua Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, mabox ya kumchagua Rais wa Zanzibar, Mabox ya kuchagua wabunge, mabox ya kuchagua wawakilishi na mabox ya kuchagua masheha katika hali kama hii athari yoyote inayojitokeza kwenye vituo vya kura inahusu kura zote.


The principle of non contradiction says "Nothing can be and not be at the same time in the same sense" hivyo haiwezekani kura zilizopigwa na watu walewale kwenye vituo vile vile zikawa na uhalali upande mmoja wa muungano (Tanzania bara) na zisiwe na uhalali upande mwingine wa muungano (Zanzibar).


Uhalali wa kura za Zanzibar kwa mgombea urais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania ungetokana na ama kuondoa kauli ya kufuta uchaguzi na matokeo yake kule Zanzibar ama kusubiri matokeo ya kura za Wazanzibari baada ya uchaguzi kurudiwa ndipo mshindi wa urais wa Jamuhuri ya muungano atangazwe.


Suala hili ni la kitaifa na ni zaidi ya ushabiki wa kisiasa Kinachopaswa kuangaliwa hapa si wingi au uchache wa kura za wazanzibari bali tuangalie haki za kila upande wa muungano kwani Tanzania ni zao la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hivyo sio busara kuubeza upande wowote kwa kigezo cha wingi au uchache wa watu au idadi ya kura.


Kwa hali ilivyo sasa ni kama vile upande mmoja wa muungano (Zanzibar) haujashiriki kumchagua Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania hali itakayopelekea mgogoro mkubwa wa kimuungano kwani Rais wa Jamuhuri ya Muungano atakosa uhalali wa kisiasa na kisheria kwa upande wa Zanzibar hali itakayowaongezea hari na kasi ya ushindi wale wanaotaka Zanzibar Huru.


Na: Izack Mwanahapa
 
Ujanja mwingi mwisho giza hili wanalo lazima liwakomoe!
 
Mkuu hawa jamaa wanajua ukweli vizuri ila wanachofanya ni kujitoa ufahamu tu.
Kushinda kwa CCM ni afe beki afe kipa goli lazima lipatikane.
 
...wampe Seif nchi yake,nothing else.!!
 
Aliyewashauri CCM kuufuta uchaguzi wa Zanzibar aliwakomoa kwa kujua ama kutojua!

Sasa kwenda mbele shida kurudi nyuma shida!
Kubalini matokeo ndio muda wenyewe umefika!
 
Sasa kuingia katika mgogoro wa kikatiba
 
Mkuu Isack;
Nimefurahi saana na maneno yako haya; katika hali kama hii dosari zilizotajwa na Mwenyekiti wa ZEC wakati akitangaza kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar ikiwemo ile ya Wapigakura kuwa wengi kuliko watu waliojiandikisha kwenye daftari inaathiri pia kura zilizopigwa na Wazanzibari kumchagua Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwasababu waliopiga kura ni watu walewale, kwa idadi ileile katika vituo vilevile na maboksi yaleyele.
Mtu mmoja kasema leo kuwa, kwa waliyo yafanya NEC ni sawa na kupika nyama ya kuku kwenye chungu kimoja na kiti moto halafu umwambie yule bibie FaizaFoxy wa JF, aje kwenye karamu ila yeye achague nyama ya kuku tu asile kiti moto.
Hao waliojitangazia uwezo wa kuufuta uchaguzi wa Zenj, je hawakuzisikia hizo sababu za wingi wa kura maruhani?? Sasa kama mtu mmoja alipiga kura 5. Iweje, za urais wa JMT na wabunge (Yaani pamoja na hizo maruhani) za Pemba ziwe halali bara lakini ziwe si Hallal ZEC?? Hapa, ni muuda tuu unavutwa. Labda aapishwe huyu wa bara
 
Shutup.Tumeishamaliza. Rais ni Dr John P Magufuli aliyechukia anywe sumu afe
 
KUMTANGAZA RAIS WA TANZANIA BILA MUSTAKABALI WA KURA ZA WAZANZIBARI NI KUITANGAZA ZANZIBAR HURU


Nianze kwa kurekebisha kauli ya mwenyekiti wa tume ya Taifa ya uchaguzi NEC alipokuwa akijaribu kuziokoa kura za Rais wa Jamuhuri ya muungano zilizopigwa na kuhesabiwa huko Zanzibar kwa kusema kwamba "Kuahirishwa kwa uchaguzi wa Zanzibar hakutaathiri mchakato wa uchaguzi Tanzania Bara" la hasha uchaguzi wa Zanzibar haujaahirishwa bali umefutwa na raisi anayetafutwa si Rais wa Tanzania bara bali Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.


katika hali kama hii dosari zilizotajwa na Mwenyekiti wa ZEC wakati akitangaza kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar ikiwemo ile ya Wapigakura kuwa wengi kuliko watu waliojiandikisha kwenye daftari inaathiri pia kura zilizopigwa na Wazanzibari kumchagua Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwasababu waliopiga kura ni watu walewale, kwa idadi ileile katika vituo vilevile na maboksi yaleyele.


Kwenye uchaguzi wa Zanzibar Maboksi yalikuwa matano kwa maana ya mabox ya kumchagua Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, mabox ya kumchagua Rais wa Zanzibar, Mabox ya kuchagua wabunge, mabox ya kuchagua wawakilishi na mabox ya kuchagua masheha katika hali kama hii athari yoyote inayojitokeza kwenye vituo vya kura inahusu kura zote.


The principle of non contradiction says "Nothing can be and not be at the same time in the same sense" hivyo haiwezekani kura zilizopigwa na watu walewale kwenye vituo vile vile zikawa na uhalali upande mmoja wa muungano (Tanzania bara) na zisiwe na uhalali upande mwingine wa muungano (Zanzibar).


Uhalali wa kura za Zanzibar kwa mgombea urais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania ungetokana na ama kuondoa kauli ya kufuta uchaguzi na matokeo yake kule Zanzibar ama kusubiri matokeo ya kura za Wazanzibari baada ya uchaguzi kurudiwa ndipo mshindi wa urais wa Jamuhuri ya muungano atangazwe.


Suala hili ni la kitaifa na ni zaidi ya ushabiki wa kisiasa Kinachopaswa kuangaliwa hapa si wingi au uchache wa kura za wazanzibari bali tuangalie haki za kila upande wa muungano kwani Tanzania ni zao la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hivyo sio busara kuubeza upande wowote kwa kigezo cha wingi au uchache wa watu au idadi ya kura.


Kwa hali ilivyo sasa ni kama vile upande mmoja wa muungano (Zanzibar) haujashiriki kumchagua Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania hali itakayopelekea mgogoro mkubwa wa kimuungano kwani Rais wa Jamuhuri ya Muungano atakosa uhalali wa kisiasa na kisheria kwa upande wa Zanzibar hali itakayowaongezea hari na kasi ya ushindi wale wanaotaka Zanzibar Huru.


Na: Izack Mwanahapa

Yote uliyoandika hapa yana logic. Rais wa JMT hutawala nchi upande wa Zanzibar kinadharia zaidi, akiwa visiwani huwa chini ya rais wa Zanzibar kivitendo! Hali hii ndiyo inayoitwa Tanganyika kuvaa koti la Muungano!
 
Back
Top Bottom